Skip to main content

SIKU YA WALEMAVU DUNIANI, YAFANA KITAIFA MKOANI IRINGA, WAZIRI MKUU ATOA AHADI


Waziri William Lukuvi akitoa tuzo kwa mmoja wa wakilishi wa taasisi zilizoshirikia maadhimisho ya siku ya walemavu duniani
John Ndumbaro naye akipokea tuzo kwa niaba ya wenzake
Akifurahia tuzo

Mtoto huyu alipokea tuzo na akalambishwa elfu kumi
Amina Molel alipokuwa akizungumzia changamoto za walemavu
Makada wa CCM nao walikuwepo
Nyagawa wa Maendeleo ya Jamii Mkoa wa Iringa naye alipata tuzo
Wakati wakishukuru
Baadhi ya wanafunzi wenye ulemavu walioshiriki maadhimisho hayo
Wengi walikuwepo
Wanafunzi
Kukawa pia na budurani ya mpira wa miguu
Baadhi ya viongozi waliookuwepo wakifuatilia kilichokuwa kikiendelea
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda amewaahidi walemavu kuwaondolea vikwazo vinavyowakabili katika suala zima la teknolojia ili waweze kushiriki ipasavyo kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ya uchumi na kijaamii.
Pinda aliyasema hayo kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani ambayo kitaifa yalifanyika katika viwanja vya Kichangani, mjini Iringa, jana.
Katika hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), William Lukuvi, Pinda alisema; “hapa Tanzania ustawi na maslai ya watu wenye ulemavu ndio sera ya serikali yetu kwa miaka mingi.”
Alisema kwa kupitia sheria ya watu wenye ulemavu ya mwaka 2010, serikali imeweka miongozo ya namna ya kutekeleza na kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu.
“Kwahiyo niwaahidi kwamba yapo mambo mengi ambayo serikali imefanya kwa kundi hilo na yako mengi tunayoendelea kuyafanya kwa ajili ya ustawi wao,” alisema.
Katika risala yao iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Amina Molel, jumuiya hiyo iliomba sheria ya haki za watu wenye ulemavu ya mwaka 2010 ifanyiwe marekebisho ili kuweza kulipa baraza la taifa la watu wenye ulemavu meno.
“Baraza linataka kuratibu, kusimamia na kutekeleza masuala yetu likiwa chombo huru badala ya kuwa chombo cha ushauri tu chini ya utendaji wa kamishna wa Idara ya Ustawi wa Jamii ambaye kwa nafasi yake ana majukumu mengi,” Molel alisema.
Molel alisema walemavu bado wanakabiliwa na changamoto nyingi lakini akazitaja sita alizosema zinahotaji kuchukuliwa hatua za haraka.
Kwa mujibu wa Molel, changamoto hizo ni pamoja na kutopatikana kwa taarifa muhimu katika mifumo iliyo rafiki kwa watu wenye ulemavu.
“Mfano ni kutokuwepo kwa ukalimani wa lugha ya alama kwenye vipindi vya luninga, mijadala ya vikao vya bunge na hotuba za viongozi mbalimbali,” alisema.
Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na vyombo vya usafiri vya umma na majengo yanayotoa huduma kwa umma kutozingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu, ruzuku ndogo kwa vyama vya watu wenye ulemavu ambayo kwa miaka mingi hajatolewa na kukosekana kwa uwakilishi katika vyombo vingi vya maamuzi na kisera.
Zingine ni kukosekana kwa ofisi ya kudumu ya shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu na kucheleweshwa utoaji ardhi huko Kibaha Pwani kwa lengo la kujenga chuo cha madereva na ufundi kwa watu wenye ulemavu.
Akiomba serikali izifanyie kazi changamoto hizo, Molel alitoa ombi kwa serikali iwapatie ofisi ya kudumu ya shirikisho lao ili kuepuka madhara yanayoweza kutokea pindi wafadhili wan je watakapositisha ufadhili wa pango la ofisi.
“Pia tunaomba ofisi za mikoa kupitia TAMISEMI wazipatie ofisi kamati zote za mikoa za SHIVYAWATA ili kuwezesha uratibu wa pamoja wa masuala yetu kwenye mikoa husika,” alisema katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya siasa na wawakilishi wa walemavu kutoka mikoa yote nchini.
Maadhimisho ya siku ya watu wenye ulemavu duniani ni moja ya jitihada za jumuiya ya kimataifa katika kuelimisha jamii kuhusu hali waliyonayo watu wenye ulemavu. (bongoleaks)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...