Skip to main content

SIDO IRINGA YAWAKOPESHA WAJASIRIAMALI WADOGO ZAIDI YA SH MILIONI 229.9



Na Fredy Mgunda, Iringa

SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO), mkoani Iringa limetoa mikopo yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 229.9 kwa wajasiriamali wa mkoa huo, katika kipindi cha July mpaka Desembea mwaka jana.


Akizungumza na uhuru, Kaimu meneja wa SIDO mkoani Iringa, Niko Mahinya alisema lengo la mkopo huo ni kuwawezesha wajasiriamali wadogo kupata mitaji, na kuinua uchumi wao ili waondokane na umaskini.

Alisema mikopo hiyo ilitolewa kwenye vikundi mbalimbali vya wilaya zote za mkoa wa Iringa na wajasiriamali mmoja mmoja, ambao kupitia SIDO wamefanikiwa kiuchumi.

“SIDO imekuwa ikitoa mikopo kwa wajasiriamali kwa masharti naafuu tofauti na taasisi nyingine za kifedha ili na riba ndogo ili kukuza mitaji yao, ”alisema.

Alisema lengo la kutoa mikopo hiyo, ni kuwasaidia wajasiriamali na wananchi wasiokopesheka kwenye mabenki na taasisi nyingine za kifedha.

Alisema mikopo hiyo ni rahisi zaidi kwa vikundi kwa madai kuwa wanachama wamekuwa wakidhaminiwa na vikundi vyao, ambavyo ikiwa mwanachama huyo atakimbia basi kikundi hicho kitabeba mzigo wa kumlipia.

Alitaja changamoto kubwa inayowakabili hasa kwa wajasiriamali wa mijini kuwa ni kutorejesha mikopo yao, jambo ambalo linasababisha usumbufu kwa SIDO na kuwafanya wengine wasikopeshwe fedha hizo.

Hata hivyo alisema kuwa mbali na mikopo hiyo, SIDO imekuwa ikitoa mafunzo ya biashara kwa wajasiriamali, ili iwe rahisi kwao kufanya biashara kwa utaalam na kuweza kukuza biashara zao.

“Pamoja na mikopo tumekuwa tukitoa mafunzo kwa wajasiriamali wetu na kuwawezesha kushiriki kwenye maonyesho mbalimbali ndani na nje ya nchi, ili kutanua uelewa wa biashara zaidi,”alisema Mahinya.

Hata hivyo aliwataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kufanya kazi na SIDO ili waweze kuondokana na ugumu wa maisha ambao umekuwa ukiwakabili kwa kuamua kuwa wajasiriamali.

Alisema ikiwa vijana watajikita kwenye ubunifu wa biashara, itakuwa rahisi kuaminiwa na SIDO na hatimaye kupatiwa mikopo midogo midogo inayoweza kuwafikisha kwenye hatua ya kukopesheka na taasisi nyingine.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...