Skip to main content

Je Wajua Kilimo cha Nyanya kwenye Banda-kitalu




Kama ilivyo kwa vijana wengi wanaohangaikia maisha, Darius Cheruiyot wa Silibwet, Tarafa ya Bomet, amejaribu kushindana na maisha kwa njia nyingi, amejaribu ufundi makanika, udereva hadi kuwa dereva wa bodaboda. 

Huko kote hakukumfanikisha kimaisha hadi alipojishughulisha na kilimo. Darius (36) mkulima wa nyanya anapenda kuwashirikisha kwenye kilimo cha nyanya kwa kutumia banda kitalu (green-house). “ Wazo la kuanzisha banda kitalu ili kulima nyanya liliibuka mwaka 2012 baada ya kutembelea shamba la binamu yangu. Nilivutika sana na kile nilichokiona.” Cheriiyot alibainisha. Aliamua kulima kwa kilimo cha banda kitalu kwani alikuwa amejaribu kulima nyanya kwenye eneo la wazi; alipata hasara kwa kuwa nyanya zilishambuliwa na magonjwa na wadudu waharibifu.

Ili ajenge Banda kitalu ilimbidi kuuza pikipiki yake kwa Sh.55,000 ( sawa na Sh. 990,000 za Tanzania). Familia yangu ikaniongezea Sh. 25,000/- (sawa na Sh. 450,000/ za Tanzania) ambazo nilizitumia kujenga Banda kitalu. Pia nilinunua polithine na mabomba ambayo niliyatumia kwenye mradi huu.” Alisema Cheruiyot.

“Nilifanikiwa kujenga baada ya kupata maelekezo na vipimo toka kwenye ofisi ya kilimo. Alijenga banda kitalu la ukubwa wa 17m kwa 13m lililoweza kupandwa miche/ mashina 1,200. Mapema mnamo mwaka 2013, na hakufanikiwa sana kwa kuwa yalikuwa mazao yake ya kwanza. Hakutaka kuangalia nyuma kwani alijua ingemvunja moyo. “ Sikupanda kwa kuzingatia nafasi, miti ilirefuka lakini haikuzaa nyanya za kutosha. Aidha, nikagundua kwamba nilikuwa natumia kiasi kikubwa cha mbolea, hili lilinikamua kiuchumi, ilibidi nifanye jambo hapo.”

Na kabla sijapanda awamu iliyofuata, alihakikisha anatumia samadi kutoka kwenye mifugo ya familia yao. Alitumia samadi ya ng’ombe akaichanganya na udongo wa bandakitalu kabla ya kupanda nyanya. “Mboji ilinisaidia kupunguza matumizi ya mbolea ya viwandani , nilitumia majani makavu kila baada ya majuma mawili”.

Cheruiyot anasema alipata takribani Sh. 200,000/- (sawa na Sh.3,600,000/- za Tanzania) kwa miezi mine ya mavuno ya nyanya zake. Anavuna nyanya kila baada ya siku mbili, na anauza sanduku / kreti moja la nyanya kati ya Sh. 500 hadi Sh. 2,000/- (TSh.9,000 hadi 3,600/- )Wengi wa wateja wake huja kununua nyumbani kwake na huenda kuzilangua katika masoko ya Bomet, Libwet na Tenwek.

Wakulima ambao wanapenda kujishughulisha na mradi kama huu kwa faida, hawana budi kuwa na ujuzi fulani. “Kwanza, nyanya zinataka eneo la joto na jua, zinahitaji angalau masaa 8 ya kupata jua kila siku, zikikosa jua huzaa matunda machache. Udongo unahitaji uwe na pH 5.5 hadi 6.8, wenye maji ya kutosha na ulio na rutuba ya kutosha.

Cheriuyot anasema,”’Mbinu nyingine ni kwamba anatumia mkojo wa sungura kwenye mche wa nyanya kabla nyanya hazijatoa maua. Mkojo wa sungura unasaidia kuzuia wadudu na kusaidia kuotesha nyanya.”


Kila mradi wa kilimo unapoanzishwa haukosi changamoto. Awali, miche yake ilikauka mara tu ilipotoka kupandwa. 




Via standardmedia.co.ke

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...