Skip to main content

JESCA: SIJASIMAMISHWA UANACHAMA MIMI BADO WANACHAMA...!



Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu amekanusha uvumi unaoenea mkoani hapa kuwa amesimamishwa uanachama pamoja kuvuliwa nafasi zote za uongozi leo wakati wa mkutano na waandishi wa habari ofisi za Iringa Press Club (IPC).



UTANGULIZI

Mtakumbuka kuwa tarehe 2/3/2015 kuna kauli ambayo ilitolewa na Katibu wa wilaya ya Mufindi Ndugu Mtaturu. Ambayo ilielekeza baadhi wanachama wetu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa uanachama kwa baadhi ya makada wetu. Akiwemo Shukuru Luhambati, Clara Shirima na Hosea Kaberege. Swala hili limeamusha malalamiko na mjadala miongoni mwa wanaCCM na wapenzi na wakereketwa wa CCM. Kila mtu akiwa na mtizamo wake kuhusu swala hili, ambalo pia kimepelekea kuamsha malumbano katika vyombo mbali mbali vya habari.

Lakini pia kumetokea wasi wasi mkubwa kwa baadhi ya wanachama ambao walihojiwa na kamati za maadili na kuwa na uvumi pia kuwa watafukuzwa au kunyang’anywa uanachama.

Hiyo pia imeleta uvumi kuwa Mimi Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Iringa pia nimesimamishwa uanachama na kuvuliwa nafasi zote za uongozi.

Moja, Sitofahamu iliyojitokeza kwa wale walioachishwa UANACHAMA: (Shukuru Luhambati, Clara Shirima na Hosea Kaberege)

Kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM. Toleo la 2010 zilizotolewa na Halmashauri Kuu ya Taifa. Fungu la Nne (8vi) pg 30 linalohusu adhabu mbali mbali kwa makosa yanayohusu ukiukwaji wa Maadili. Inasema katika kipengele hicho:

(vi) Kuachishwa Uanachama:

MwanaChama anayegundulika ana makosa ya Itikadi, yanayoathiri Uhai wa Chama, au ambaye ameshindwa huko nyuma kujirekebisha hata baada ya Karipio, wala haonyeshi dalili za kuweza kujirekebisha hata akipewa muda zaidi, basi Kamati ya Usalama na Maadili ya Taifa inaweza kupendekeza mbele ya Kamati Kuu mwanachama huyo aachishwe UANACHAMA. Ikiridhika, Kamati Kuu itapeleka shauri hilo mbele ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa uamuzi wa mwisho.

Adhabu ya kuachishwa Uanachama itatangazwa hadharani.



Pia Fungu la Tatu linalohusu: WAJIBU WA KUSIMAMIA TABIA, MWENENDO NA VITENDO VYA MWANACHAMA NA KIONGOZI;

Ni wa vikao vya Chama cha Mapinduzi vya Halmashauri kuu na Kamati zake za Siasa kwa kila ngazi kama ilivyoanishwa kikatiba.

Kwa swala la leo hapa: Ibara ya 93(8), (14) na (15), Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa:-…….(14) Kumwachisha au kumfukuza Uanachama Mwanachama ye yote endapo itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uanachama. Mwanachama anayeachishwa au kufukuzwa uanachama anaweza kukata rufaa kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa.

Hivyo basi, hakuna sababu yakuwa na hofu au mashaka. Wale ambao wanadhani hawajatendewa haki wanahaki ya kukataa rufaa vikao vya juu zaidi, kama Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa. 

Pili, Kuhusu Mwenyekiti wa CCM Mkoa kusimamishwa Uongozi sio kweli. Ibara 93 (15) fungu la tatu. Halmashauri Kuu ya Mkoa; Inaweza Kumwachisha au Kumfukuza Uongozi kiongozi ye yote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa.

Pia,Ibara 95(7) Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa; 

Kumsimamisha uongozi kiongozi ye yote wa ngazi ya wilaya endapo itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uongozi. Isipokuwa kwamba haitakuwa na uwezo wa kumsimamisha uongozi kiongozi ambaye uteuzi wake wa mwisho haukufanywa na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.

Kwa nafasi yangu mimi kama Mwenyekiti wa Mkoa siwezi kusimamishwa uongozi na ngazi ya Mkoa. Hata pia kwa nafasi ya Diwani lazima ipelekwe vikao vya ngazi ya Taifa.

Ingawa wilaya ya Iringa Mjini kupitia Katibu wake Zongo Lobe Zongo wamenipa Adhabu mimi Mwenyekiti wa Mkoa kwa Kupewa Adhabu ya Onyo Kali. Taratibu nyingine zitafuatwa kwa mujibu wa vikao.

Nina toa maelekezo pia kwa Kamati za Maadili zote katika ngazi zote za Mkoa wa Iringa kuzingatia kanuni, Katiba na maelekezo ya Chama katika utekelezaji wao wa Kazi zao za Kamati ili kutoviyumbisha vikao vya maauzi vya Chama. Pia ili kuondoa mgongano unaweza ukajitokeza kati ya viongozi, wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi kwa ujumla wake. Kwa mujibu wa Kanuni za uongozi na maadili toleo la 2012; fungu la nne 7(1)…”Katika kusimamia maadili ya viongozi wa CCM wakati wo wote wa utekelezaji wa kanuni hizi, ..Kamati ya Usalama na maadili katika ngazi inayohusika (mkoa) itazingatia Katiba ya CCM na Kanuni zingine za CCM zitakazo kuwepo wakati huo, pamoja na maelekezo mengine ya msingi yatakayokuwa yametolewa na Halmashauri Kuu ya Taifa”. 



Ninawasisitiza kuzingatia zaidi; Kanuni za Uongozi na Maadili fungu la Nne 7(4)ii-kinachohusu Tuhuma: Kinasema

”Uchambuzi wa tuhuma hizo utafanywa kwa kutumia njia mbali mbali pamoja na mashahidi watakaoweza kupatikana.

Na endapo itadhihirika kwamba tuhuma zina uzito, mtuhumiwa atatitwa mbele ya kikao cah Kamati ya Usalama na Maadili ya ngazi inayohusika, kama ni lazima, ili apate kuhojiwa ana kwa na.



Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa



Madam Jesca Msambatavangu







Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...