Skip to main content

NCAA, UNESCO WAANGALIA UTALII ENDELEVU NGORONGORO



Mkufunzi ambaye pia ni mtaalamu mshauri wa Unesco, katika masuala ya utalii endelevu, James Banks akiendesha mafunzo kwenye warsha ya siku nne ya kutengeneza mkakati wa utalii endelevu hifadhi ya Ngorongoro iliyomalizika mwishoni mwa wiki mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha na kuandaliwa na Shirika la UNESCO kwa kushirikiana na Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA). Pichani chini kulia ni Mmoja wa wakufunzi wa warsha hiyo, Tamim Amijee.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)

Karatu

SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) likishirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) wameandaa kongamano la siku nne lililofanyika mjini hapa kuangalia mkakati mpya wa kuendeleza utalii kama kitovu cha mapato katika hifadhi ya Ngorongoro.

Kongamano hilo ni moja ya makongamano kadhaa ambayo yameandaliwa kwa pamoja kwa lengo la kutoa mwelekeo mpya katika hifadhi hiyo ambayo binadamu na wanyama huishi pamoja.

Akizungumza na mtandao huu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues, alisema kwamba kongamano hilo limeandaliwa kwa lengo la kujenga uwezo kwa wadau mbalimbali wa sekta ya utalii kutambua haja ya utalii endelevu ambao pia utazingatia maslahi ya wananchi wanaoishi katika eneo hilo.

Alisema wakati NCAA inaangalia upya mkakati wake wa maendeleo katika hifadhi hiyo ambayo pia ni urithi wa dunia, UNESCO kama washirika wa karibu wamekubaliana kuendesha kongamano ambapo wadau wote kuanzia wananchi wanaoishi katika hifadhi hiyo na waendesha utalii zikiwemo hoteli na watawala kuangalia namna bora ya kuendesha hifadhi na kuneemesha wananchi.


Zulmira alisema kwamba hifadhi hiyo inaingiza fedha nyingi ambazo zingeweza pia kuwafikia wananchi moja kwa moja kwa kuanzisha mikakati ambayo inahusisha wananchi wenyewe na wadua mbalimbali wa sekta hiyo.

Alisema kwamba idadi ya watalii wanaoingia hapo wanaingiza fedha nyingi serikali kuu lakini kiasi hicho hakionekani wazi wazi kwa wananchi na hivyo ipo haja ya kuangalia mwelekeo mpya ambao utaendelea kuhifadhi urithi huo huku wananchi wake wakifaidika na uwapo wa urithi huo.

Wakati wa kongamano hilo washiriki walifanya ziara katika maeneo mbalimbali ya kitalii kabla ya kufanya majadiliano na kuweka mwelekeo wa namna bora ya kutengeneza mkakati utakaoshirikisha wadau wote wa utalii katika eneo hilo.

Alisema kwa muda mrefu tangu hifadhi hiyo iwe urithi UNESCO na NCAA walikuwa wakiangalia zaidi suala la hifadhi kiasi cha wananchi kuona kama wameachwa nyuma hivyo mkakati wa sasa ni kuwawezesha wananchi kufaidi matunda ya urithi huo kwa kila kada kupewa wajibu wake na kuona namna ya kuutekeleza ili ndoto iwe kweli.


Mkufunzi ambaye pia ni mtaalamu mshauri wa Unesco, katika masuala ya utalii endelevu, James Banks akiwaelekeza jambo washiriki wa warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa wiki mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha.

“Tumedhamiria kujenga uwezo… kusaidia wananchi kuongeza kipato chao kutoka kwa watalii … ukiangalia katika kreta unaweza kuona magari mengi yakiwa na watalii… tunataka watu wanaoishi katika eneo hili pia wafaidike …” alisema.

Hifadhi hii inatambulika duniani kwa kreta yake kubwa, mbuga yenye wanyama wengi na eneo ambalo inasadikiwa binadamu wa kwanza aliishi kabla ya kutawanyika duniani

Ikiwa na ukubwa wa kilomita za mraba 8,300 Hifadhi ya Ngorongoro ndio hifadhi pekee duniani ambapo wanadamu wanaishi pamoja na wanyama kwa usalama.

NCA ilianzishwa mwaka 1971na kutangazwa kuwa urithi wa dunia na UNESCO mwaka 1979 lakini kwa muda sasa kumekuwepo na mawazo kwamba dhima kubwa imekuwa kulinda wanyama na mazingira na kusahaua kwamba pale pana binadamu ambao wanamahitaji na wanataka kufaidika pia na mazingira ambayo wanayalinda.


Pichani juu na chini ni washiriki na wadau wa sekta ya utalii kwenye warsha ya siku nne ya kutengeneza mkakati wa utalii endelevu hifadhi ya Ngorongoro iliyomalizika mwishoni mwa wiki mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha na kuandaliwa na Shirika la UNESCO kwa kushirikiana na Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA).

Kwa mwaka zaidi ya watalii 450,000 huzuru Ngorongoro ikiwa ni asilimia 60 ya watalii wanaofika nchini.

Mtaalamu mshauri wa Unesco, James Banks, ameelezea kufurahishwa kwake na kongamano hilo na kusema kwamba linatoa mwanya wa wadau mbali mbali muhimu Ngorongoro kuona mwelekeo mpya unaostahili kuchukuliwa ili kuwa na utalii endelevu.

Alisema matokeo ya mkakati huo sio tu utaongeza mapato serikalini bali pia utaimarisha utalii kutokana na ushiriki wa moja kwa moja wa jamii zinazoishi ndani ya hifadhi hiyo.

Mshiriki mwingine wa kongamano hilo Flora Assey, Afisa Utalii kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha alielezea kufurahishwa na kongamano hilo hasa kwa kuchukua mlengo wa masomo kwa vitendo hali ambayo anaamini itabadili kabisa utekelezaji wa mkakati unaobuniwa kwa sasa.


Naye Meneja mkuu wa Ngorongoro Serena Safari Lodge, Dismas Simba alielezea kuridhishwa kwake na kongamano hilo na kusema litawezesha wadau wote kufanyakazi kwa pamoja kuhakikisha kwamba utalii unakuwa endelevu katika eneo hilo hasa kwa kuzingatia kwamba eneo hilo ndilo pekee duniani ambako wanyama na wanadamu wanaishi pamoja.

Naye Ofisa Mwandamizi wa Miradi na Mratibu wa UNESCO katika masuala ya urithi wa dunia na utalii endelevu, Peter DeBrine amepongeza hatua iliyofikiwa na wadau katika kongamano hilo na kusema raundi ya pili Juni mwaka huu itatoa mwangaza zaidi kwani utarejesha majibu ya maswali ambayo kila mtu amepewa kuyafanyia kazi.

Alisema amefurahishwa na kiwango cha kujituma cha wajumbe waliofika katika kongamano hilo na kusema kwa jinsi ilivyo mabadiliko yanayofikiriwa na NCAA yatafanikiwa ili wananchi nao wawe wanafaidika moja kwa moja na uwapo wa urithi huo wa dunia katika maisha yao.



Flora Assey, Afisa Utalii kutoka ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha akinakili mambo muhimu wakati wa kuhitimisha warsha hiyo ya siku nne iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano Kudu Lodge and Campsite iliyopo mji mdogo wa Karatu mkoani Arusha.


Mwenyekiti wa Baraza la wakina Mama kata ya Oloirobi, Kijiji cha Mokilal mkoani Arusha, SEKETO OLDUMU akishiriki kwenye kikundi kazi wakati wa warsha ya siku nne ya kutengeneza mkakati wa utalii endelevu hifadhi ya Ngorongoro iliyomalizika mwishoni mwa wiki mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha na kuandaliwa na Shirika la UNESCO kwa kushirikiana na Ngorongoro Conservation Area Authority (NCAA).


Meneja Mkuu wa Ngorongoro Crater Lodge | &BEYOND, Markus Schroeder (kulia) akishiriki kuchangia maoni wakati wa warsha ya siku nne ya kutengeneza mkakati wa utalii endelevu hifadhi ya Ngorongoro iliyomalizika mwishoni mwa wiki mji mdogo wa Karatu, mkoani Arusha. Kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la elimu sayansi na utamaduni (UNESCO) Zulmira Rodrigues.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...