Skip to main content

SAMAKI WAADIMIKA MTERA


Soko Kuu la Manispaa ya Iringa, mkoani Iringa linakabiliwa na uhaba wa samaki kutokana na uvuvi haramu unaoendelea katika Bwawa la Mtera.

Baadhi ya wafanyabiasha wa samaki walioongea na gazeti la Nipashe leo walisema uhaba wa samaki katika soko hilo unatokana na sababu nyingi na kubwa zaidi ni uvuvi haramu uliyokidhiri katika Bwawa la Mtera.


Walisema kuwa kuna uvuvi haramu unaondelea katika bwawa hilo unaofanywa na wafanyabiashara wakubwa kwa kushirikiana na viongozi na wanasiasa wanaofanya biashara ya kuvua samaki wadogo wanaofahamika kwa jina maarufu kama dungu.

Walisema kuna wafanyabiashara wakubwa, viongozi wa serikali na wanasiasa wanachochea kukuwa kwa biashara ya uvuvi haramu kwa kutumia nyavu zenye nchi moja kuvua samaki katika bwawa pamoja na kufungua maduka mengi ya nyavu zenye macho madogo (small mesh fish nets) kila kona.

Walisema kuwa siasa imekuwa ikitumika kuchochea biashara haramu ya uvuvi na kuingilia kazi za wataalamu ambapo wafanyabiashara hao walishauri kuwa kazi ya wataalamu iaachwe ifanywe na wataalumu wenyewe na masuala ya siasa yawekwe pembeni ili kunusuru kizazi cha samaki bwawa la Mtera kisipotee.

Francis Haule, ni wafanyabiashara ya samaki maarufu ambaye alianza biashara ya samaki tangu mwaka 1984, alisema kuwa kuna sababu nyingi zinazopelekea kupungua kwa samaki sokoni hapa.

Alisema kuwa sababu ya kwanza kabisa vyanzo vya samaki vimekuwa ni vilevile havioongezeki wakati walaji wa samaki  wanaongezeka kila siku lakini vyanzo vya samaki vinabakia vile vile.

Alisema kuwa kimekuwa na chanzo kimoja cha samaki cha Bwawa la Mtera ambapo samaki wanaotoka katika bwawa hilo wanapelekwa katika mikoa mbalimbali kama vile Mbeya, Ruvuma, Njombe, Dodoma, Morogoro, Dar es Salaam, Lindi na Mtwara.

Aidha, alisema samaki wanaopatikana katika bwawa la Mtera ni pamoja na Perege, Kambale, Galala, Sulusulu, Mchema na Katoga.

Alisema kuwa sababu nyingine inayosababisha kuwa na uhaba wa samaki ni bwawa hilo kukauka maji kutokana na kilimo cha umwagiliaji cha mpunga katika Mto Ruaha.

“Kumekuwa na matumizi mabaya ya maji yasiotumika kulingana na mahitaji, maji mengi yanaenda porini bure. Watu wanatakiwa kiwa na kilimo cha umwagiliaji endelevu kwa kutumia maji kulingana na mahitaji na baada yakutumika maji yarudishwe kwenye mkondo wake wa mto yakatumike kuzalisha umeme katika bwawa la Mtera,” alisema Haule.

Alisema kuwa kuwepo na matumizi ya maji yasiotumika kulingana na mahitaji kunapelekea kupungua kwa maji bwawa la Mtera na kusababisha tatizo la umeme la mara kwa mara.

Alisema pia kwamba kumekuwepo na mahitaji makubwa ya samaki katika jamii na baada ya watu wengi kuacha kula nyama nyekundu (red meat) na kukimbilia kwenye nyama nyeupe (white meat) baada yakushauriwa na madaktari kuwa nyama nyekundu ina madhara kiafya.

Alisema kuwa watu wengi wamekuwa wakikimbila kula nyama nyeupe kama vile samaki, kuku na kitimoto, ambayo wanadai kwamba haina madhara ukilinganisha na nyama nyekundu ambayo ina kemikali kwenye nyama kutokana na madawa yanayotumika kufugia.

Naye, Henry Shabani ambaye pia ni mfanyabiashara wa samaki katika Soko Kuu la Manispaa alisema kuwa uhaba ya samaki sokoni ni kutokana na uvuvi haramu unaendelea katika bwawa la mtera bila kudhibitiwa.

Alisema kuwa uvuvi haramu unaofanywa aidha na wafanyabiashara wakubwa kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali wa serikali na wanasiasa kwa maslahi binafsi ndio chanzo cha uhaba wa samaki.

Alisema kuwa wafanyabiashara hao wakubwa kwa kushirikiana ama na viongozi wa serikali na wanasiasa wamekuwa wakifanya uvuvi haramu kwa kutumia nyavu zenye nchi moja badala yakutumia nyavu za nchi tatu ( 3 ply fish nets) zinazoruhusiwa.
Alisema kuwa nyavu zenye nchi moja kimsingi ni makokolo kwa sababu zinakusanya kila aina ya samaki wakubwa kwa wadogo pamoja na samaki wenye mayai.

Alisema kuwa na kuwepo kwa kuzembea kwa waatalamu hasa mabwana samaki ambao muda wote wapo maofisini na kuruhusu watu wafanye uvuvi haramu tatizo lingine linalosababisha kukosekana kwa samaki sokoni.

“Na kumbuka enzi za Magufuli wakati akiwa Waziri wa Uvuvi kulikuwa na udhibiti mkubwa wa uvuvi haramu tulishuhudia makokolo yakikamatwa na kuchomwa moto lakini leo hii uvuvi haramu ni jambo la kawaida…!,” alisema Shabani.

Alisema wafanyabiashara wakubwa wana maduka ya kuuza nyavu kila kona lakini cha kushangaza hakuna bwana samaki au kiongozi yeyote wa serikali anayekagua maduka hayo kuhakikisha yanauza nyavu zilizoruhusiwa kuvua samaki.

Aliongeza kuwa wamekuwa wakishuhudia pia magari makubwa kutoka nchini Congo ya kibeba samaki wadogo  (dungu)pale Mtera kwa kuwa kuna soko kubwa la samaki wadogo wanaovuliwa kinyume cha kisheria.

“Ndugu mwandishi wa habari hebu jaribu kutembelea kila meza ya samaki hapa sokoni utaona samaki wadogo kwa jina maarufu (dungu), zamani ukikutwa unauza samaki kama hawa unakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria pamoja na mtu aliyekuuzia samaki hao kutoka bwawani. 

Laiti mabwana samaki wangekuwa wakifanyakazi ipasavyo na kufuatilia kwa makini kuhakikisha nyavu zenye macho madogo na samaki  wadogo kudhibitiwa wasingefika hapa sokoni,” alisema Shabani.

Alisema kuwa samaki hao wadogo kwa mfano, wanauzwa shilingi 30/- mmoja wakati samaki mkubwa mmoja anauzwa kati ya 2,000/- na 5,000/-, kwa maana hiyo utalazimika kuuza samaki wadogo kwa wingi ili upate shilingi elfu mbili au elfu tano.

Aliongeza kwa mtazamo wake yeye kuwa baada ya miaka mitano ijayo bwawa la Mtera litakauka na samaki watapotea kutokana na baadhi ya watu kulima karibu na bwawa kunako sababisha bwawa kujaa udongo kutokana na shughuli za kilimo kandokando la bwawa.

Alisema biashara ya samaki imemfanya ajenge nyumba na kupeleka watoto shule lakini anapoona uvuvi haramu unaendelea kunamfanya akate tamaa.


“Nimekuwa katika biashara ya kuuza samaki tangu 2002 na takribani miaka 13 sasa nipo bado kwenye biashara hii nimejenga nyumba yangu na kupeleka shule watoto kwa biashara hii, lakini ninapoona uvuvi haramu huu… isee,” alimalizia shabani. 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...