Skip to main content

TANZANIA, JAPAN WATILIANA SAINI UJENZI WA KITUO CHA UFUNDI STADI ILEJE


Signing the grant contract, witnessed by Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, and Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner. Front line from the left: Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Simon Mwango'nda, Executire Director of the recipient organisation, Integrated Rural Development Organisation, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.

Na Mwandishi wetu

MKATABA wa Ujenzi wa kituo cha mafunzo ya ufundi stadi katika Wilayani Ileje, Mkoani Mbeya umetiwa saini.

Mradi huo uliobuniwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Janet Mbene na Simon Kamiyoge umelenga kuwawezesha wakazi wa Ileje kuwa na taaluma ya ufundi na baadae kutumika kuendelea wilaya hiyo.

Mkataba huo ulitiwa saini kati ya Kazuyoshi Matsunaga wa ubalozi wa Japan nchini na na Mwakilishi wa Integrated Rural Development Organisation (IRDO) Simon Kamiyoge wakishuhudiwa na Naibu waziri wa Viwanda na Biashara, Mh. Janet Mbene , Mbunge wa Ileje Rosemary Staki na Mkuu wa wilaya ya hiyo Mohamed Maliyao Mwala, na Mwenyekiti wa halmashauri ya Ileje Musa J. Otieno na maofisa wengine wa wilaya hiyo.

Kaimu Balozi wa Japan Kaziyoshi alisema amefurahishwa sana kutiwa saini kwa mkataba huo kwa kuwa unamkumbusha miaka 70 iliyopita katikati ya vita kuu ya pili ya dunia ambapo Japan ilijikuta katika uharibifu mkubwa pamoja na kubomolewa kwa majengo ya shule.

Alisema katika vita hiyo Japan ilijikuta si tu hawana shule bali hakukuwa na nyumba, maji, umeme hamna chochote kile lakini sasa hivi Japan ni ya tatu kiuchumi.


Discussion between Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan, and Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade. From left: Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner, Hon. Mohamed Maliyao Mwala, Chairperson of Ileje District Council, Mr. Mussa Otieno, District Executive Director, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan.

Amesema pamoja na kuwa na uchumi mkubwa Japan haina gesi, haina dhahabu wala almasi kama ilivyo Tanzania.

Alisema siri ya maendeleo makubwa ya Japan ni elimu na wafanyakazi wenye ujuzi unaotakiwa.

Alisema kuonesha ukuaji wa ujuzi alisema kwamba kampuyni maarufu ya magari ya Toyota, kabla ya vita ilikuwa ni kampuni ya nguo . Lakini baada ya vita ilijibadilisha kuwa kampuni ya magari, na sasa ni namba moja duniani.

Alisema siri ya Toyota ni kuwa na wataalamu wenye ujuzi na kuwa na malengo ya wazi yanayoambatana na tamaa ya kufanikiwa katika malengo hayo.

Lengo la Toyota lilikuwa kushindana na viwanda vya Marekani na hivyo walinunua gari kutoka Marekani na kulivunja katika vipande 4000 na baadae mafundi wa Toyota wakaigiza vipande hivyo na kuunga gari kwa mikono yao wenyewe.


Speech by Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires. From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Mr. Joseph Safe Mchome, District Land, Natural Resources and Environmental Officer, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade.

Katika hatua za mwanzo magari yaliyotengenezwa yalikuwa mabaya sana lakini siku zilivyokwenda walitoa gari nzuri zaidi na sasa ni namba moja duniani.

Kwa sasa Toyota si tu kampuni yenye wataalamu tu lakini pia wataalamu hao hupewa motisha ya kuweza kutekeleza malengo yote.

Kaimu alisema kwamba kwa kuangalia uzoefu wa zamani wa kiutendaji , Japan inaamini ili kuendeleza ni lazima kutengeneza namna ya mradi unaohamasisha vijana na pia kuwapa utaalamu wa kuutumia na katika dhana hiyo wanatoa msaada kuijenga Ileje ijayo.


Shaking hands after the speech. From left: From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Mr. Joseph Safe Mchome, District Land, Natural Resources and Environmental Officer, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade.

Kituo hicho kinatarajiwa kuwanoa vijana kitaalamu katika masuala ya ufundi stadi ili vijana hao waweze kutekeleza ndoto zao na za eneo lao wanalotoka na taifa.

Mradi huo uliotiwa saini ni wa shilingi milioni 160.

Balozi huyo alitoa shukurani kwa timu ya watu waliofanikisha kupatikana kwa mradi huo na kusema wanaandaa vyema wakazi wa Ileje kwa maendeleo yao wenyewe.

Alisema serikali ya Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kuhakikisha kwamba Tanzania inasonga mbele katika kufunzi za wataalamu.


Discussion between Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires of the Embassy of Japan, and Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, at the planned construction site of vocational training centre. From left: Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires.


Gift from Ileje District. From left: Mr. Kazuyoshi Matsunaga, Chargé d'affaires, Hon. Janet Mbene, Deputy Minister of Industry and Trade, Hon. Rosemary Senyamule, Ileje District Commissioner.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...