Skip to main content

DKT. MAHIGA: SIJAKUBALI WALA KUKATAA USHAWISHI WAKUGOMBEA URAIS



Balozi Dkt. Augustine Mahiga ni mmoja wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuwa nyuma ya kauli ya Rais Jakaya Kikwete kwamba kuna watu wanauwezo wa kurithi nafasi yake, lakini hawajajitokeza.

Balozi wa kudumu katika umoja wa mataifa huyo amesema kuwa bado hajakataa wala kukubali ushawishi unaofanywa na makundi ya watu juu ya kuwania nafasi ya urais kupitia CCM katika uchaguzi utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Akizungumza na waandishi mara baada ya kumalizika kwa mahafali kuongea na wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Tosamaganga iliyopo wilaya ya Iringa, Balozi Mahiga alisema tangu Rais Kikwete atamke tamko la kimapinduzi kule Songea na gazeti la Raia Mwema kuandika watu wamekuwa wakijitokeza kumshawishi kuwania nafasi hiyo kupitia CCM.

Pamoja na balozi Dk. Mahiga wengine wanaotajwatajwa nyuma ya kauli ile ni pamoja na aliyekuwa Jaji mkuu Augustine Ramadhani.
Alisema kushawishiwa kuchukua fomu kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo nyeti kwa taifa ni jambo moja, jingine ni mchakato mzima wa kukamilisha masharti ya chama ikiwemo kuzunguka mikoa 10 kupata wadhamini na tatu ni kazi ya chama.

“Nimepata makundi ya watu na mtu mmoja mmoja wakinishauri  nichukue fomu ya kuwania urais baada ya Rais Kikwete kutoa kauli kule Songea mkoani Ruvuma, lakini bado sijakubali wala kukataa ushawishi huo”, alisema Balozi Dk. Mahiga.

Aidha alisema kumekuwepo na hali ya wanaowania nafasi ya urais kutumia fedha jambo ambalo litalifikisha taifa mahali pabaya kwa kumpata mtu asiyestahili.

Alisema endapo ikitokea akachaguliwa Dk. Mahiga alisema ni vema rais ajaye akawa na sifa zinazoenea na kuelezeka ili kuweza kupokea kijiti kutoka kwa Rais wa sasa na kulipeleka mbele taifa katika kipindi cha miaka mingine.

Alizitaja sifa za rais ajaye kuwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kuzitatua changamoto ambazo hazijaweza kutatuliwa kwa sasa ikiwemo ya ugaidi, usafirishaji wa binadamu (human trafficking) na mashabulizi dhidi ya wageni (xenophobia).

Nyingine ni kuwaunganisha watanzania kuwa kitu kimoja, muadilifu na mwenye mtazamo wa mbali kwa watanzania na taifa.

Dkt. Mahiga alisema pia kutambua matatizo ya msingi ya watanzania, uwajibikaji na kuonesha mfano kwa watumishi wa umma.

Dkt. Mahiga amepata kuwa Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Ban ki Moon, nchini Somalia na pia nchini Liberia wakati wa Vita ya wenyewe kwa wenyewe wakati huo yeye akifanya kazi ya kuongoza shughuli za Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la (UNHCR).

Mahiga amepata pia kuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika kipindi cha kati ya mwaka 2003 hadi 2010, ambapo alirejesha heshima ya Taifa hili kiasi cha kufikia kuwa mojawapo ya zilizounda Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Katika kipindi cha kati ya mwaka 1980 hadi mwaka 1983, Mahiga alikuwa Kaimu Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, nafasi ambayo ilimpa fursa ya kuifahamu Tanzania nje na ndani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...