Skip to main content

JIMBO LA SHINYANGA LAPATA ASKOFU MPYA..!




Mwanzoni mwa Mwezi Februari Baba Mtakatifu Francisko alimteua Monsinyori Liberatus Sangu kutoka Jimbo Katoliki la Sumbawanga, kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Shinyanga, Tanzania ambapo baadaye Jumapili iliyopita (tarehe 12/04/2015) aliwekwa wakfu na kusimikwa jimboni humo.

HISTORIA FUPI YA SKOFU MTEULE, LIBERATUS SANGU


Alizaliwa Februari 19, 1963 katika kijiji cha Mwanzye Jimbo Katoliki la Sumbawanga.
Baada ya kumaliza masomo ya Falsafa katika Seminari Kuu Kibosho Jimbo Katoliki Moshi na Teolojia katika Seminari Kuu ya Segerea Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, alipewa Daraja la Upadri Julai 9, 1994.

Katika maisha yake kama Padri, Askofu Mteule Sangu amewahi kuwa Mlezi wa Seminari ndogo ya Kaengesa Jimbo Katoliki la Sumbawanga kuanzia mwaka 1994 hadi mwaka 1995. Akateuliwa kuwa Paroko wa Parokia ya Matai kuanzia mwaka 1995 hadi mwaka 1996.

Mwaka 1996 hadi mwaka 1999 alikuwa Roma kwa masomo ya elimu ya juu na shahada ya Uzamili katika (Teolojia) taalimungu ya Sakramenti za Kanisa, katika Chuo Kikuu cha Kipapa cha Mtakatifu Anselmi kilichoko mjini Roma.
Kuanzia mwaka 1999 hadi mwaka 2000, aliteuliwa kuwa Msimamizi wa Parokia ya Mwanzye.

Kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2007 akateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Miito Jimbo Katoliki la Sumbawanga, mlezi katika mwaka wa malezi na Mkurugenzi wa Utume wa Vijana Jimbo Katoliki Sumbawanga.

Kunako mwaka 2007 hadi mwaka 2008 aliteuliwa kuwa Paroko wa muda Parokiani Sopa. Kuanzia mwaka 2008 hadi uteuzi wake, amekuwa akitekeleza utume wake kama Afisa Mwandamizi Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu mjini Vatikani.
Itakumbukwa kwamba, Jimbo Katoliki la Shinyanga, kuanzia mwaka 2012 limekuwa wazi kufuatia kifo cha Askofu Aloysius Balina.

Historia fupi ya Jimbo Katoliki Shinyanga
Juni 24 mwaka 1950 Jimbo hilo lilikuwa Vikarieti Apostoliki ya Maswa, ilipofika Machi 25 mwaka 1953 likawa Jimbo Katoliki Maswa. Ilipofika Agosti 9 mwaka 1956 jina la jimbo hilo likabadilika likawa Jimbo Katoliki Shinyanga hadi leo.

MAASKOFU WALIOWAHI KUONGOZI JIMBO HILO

Askofu Edward Aloysius MC Gurkin, M.M. kuanzia Julai 4 mwaka 1956 hadi Januari 30 mwaka 1975 alipostaafu.
Askofu Castor Sekwa aliyeteuliwa Januari 30, mwaka 1975 hadi Juni 4, mwaka 1996 alipofariki.
Askofu Aloysius Balina aliyeteuliwa Agosti 8 mwaka 1997 hadi Novemba 6 mwaka 2012 alipofariki.
Askofu Mteule Liberatus Sangu aliyeteuliwa Februari 2 mwaka 2015.

(CHANZO: Radio Vatican)


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...