Skip to main content

Pato la Mkoa wa Iringa limeongezeka



Pato la Mkoa wa Iringa limeongezeka kutoka Shilingi milioni 867,482 mwaka 2005 hadi kufikia Shilingi milioni 2,755,924 Mwaka 2013 ambapo Mkoa ulishika nafasi ya tano.

Hayo alibainika wakati wa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza akitao taarifa ya mafanikio ya utekelezaji wa matokeo makubwa sasa (BRN) Julai, 2013 hadi kufikia Februari, 2015 kwa waandishi wa habari jana. 

Alisema kuwa katika kuchangia pato la Taifa, Pato la Mkazi mwaka 2005 lilikuwa Shilingi 558,444 ambalo limeongezeka hadi kufikia Shilingi 1,660,532 mwaka 2013 na kuufanya Mkoa kushika nafasi ya pili kwa kuwa na pato kubwa la Mkazi.

“Pato la Mkoa huchangiwa kwa kiasi kikubwa na mashamba makubwa ya tumbaku, chai, viwanda vya chai, misitu na viwanda vya mbao,” alisema. 

Katika sekta ya maji, alisema kuwa malengo makuu ni kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika Halmashauri zote nne kwa kujenga miradi ya maji 31 katika vijiji 42. 

Aidha vituo 381 vya kutekea maji vimejengwa na 175 kati ya hivyo vinatoa huduma kwa watu 38,015. 

Kwa ujumla watu wanao pata huduma ya maji safi kufikia Desemba, 2014 ni 652,278 sawa na asilimia 69.3 ya wananchi wote wa Mkoa wa Iringa. 

Katika utekelezaji wa Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Miradi ya Maji ni kama ifuatavyo; 

Miradi iliyokamilika ni Mradi wa pamoja wa Mawelewele, Mkoga na kitasengwa, mradi wa pamoja wa Nduli, Mgongo na Kigonzile Manispaa ya Iringa; Igangidung’u H/Wilaya ya Iringa; Kipaduka, Vitono na Ikuka H/Wilaya ya Kilolo na Igomaa, Mapanda na Kiponda H/Wilaya ya Mufindi. 




Miradi iliyo zaidi ya 80% ni 10 ambayo ni: Irindi, Ihimbo, Ilamba, Ng’uruhe na Ipalamwa H/Wilaya ya Kilolo, Ikimilinzowo H/Wilaya ya Mufindi na Malinzanga, Kikombwe, Weru na Mfyome H/Wilya ya Iringa. 


Miradi iliyo 60% - 80% ni 3 ambayo ni: Mwatasi na Lulanzi H/Wilaya ya Kilolo na Ukami H/Wilaya ya Mufindi. 

Miradi iliyo chini ya 60% ni 3 ambayo ni: mradi wa pamoja wa Itengulinyi, Isupilo na lumuli, na miradi ya Izazi na Migoli H/Wilaya ya Iringa. 

Miradi ambayo haijaanza ni 5 ambayo ni: Mosi, Ugele na Ulonge-Kigungawe, Manispaa ya Iringa, Izazi na Migoli H/Wilaya ya Iringa, Sawala-Kibao na Mkonge-Igoda H/Wilaya ya Mufindi. 

Utekelezaji wa miradi kwa Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa katika sekta ya afya imejikita katika huduma za mama na mtoto. 

Malengo makuu ni kupunguza vifo vya mama wajawazito kutoka kiwango cha sasa cha vifo 156/100,000 (vizazi hai) hadi kufikia 150/100,000; Kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5 kutoka kiwango cha sasa cha 9.1/1000 hadi kufikia vifo 7/1000; Kupunguza vifo vya watoto chini ya mwaka 1 kutoka kiwango cha sasa cha vifo 8.5/1000 hadi kufikia vifo 5/1000; na kupunguza vifo vya Watoto Wachanga wenye umri wa siku 28 baada ya kuzaliwa kutoka kiwango cha sasa cha vifo 8.1/1000 hadi kufikia vifo 4/1000. 

Utekelezaji wa Mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa 

Utekelezaji wa Mfumo wa Matokeo Makubwa katika shughuli za afya hadi Desemba, 2014 uko kama inavyoonyesha katika viashiria vifuatavyo: 

Mama wajawazito wanaozalia vituoni (wanaohudumiwa na wakunga wenye ujuzi ni asilimia 100. 

Mama wajawazito wanaohudhuria kliniki katika wiki 12 ni asilimia 50. Wanawake wenye umri wa kuza (umri wa miaka 15 – 49) ni asilimia 49. 

Watoto waliopatiwa chanjo ya “Pental 3” ni asilimia 94 

Watoto wanaopatiwa dawa (ARV) za kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI ni asilimia 92 

Napenda kutumia nafasi hii kutoa shukrani kwa wadau wote tunaoshirikiana katika kuboresha huduma za afya mkoani. 

Aidha ninawashukuru umoja wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya hapa mkoani Iringa kwa kujitokeza kutoa damu kwa wagonjwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Iringa tarehe 11/4/2015 ambapo “units” 23 za damu zilipatikana. 

Pia ninatumia nafasi hii kutoa taarifa kwa wananchi wa mkoa wa Iringa kuwa kutakuwa na wiki ya chanjo Kitaifa ambayo itaanza tarehe 24-30/4/2015. 

Ninawaomba wananchi wote wa mkoa wa Iringa kuwapeleka watoto wenye umri chini ya miaka 5 kupata chanjo za kuzuia magonjwa ambazo ni muhimu sana. 

Lengo la wiki hiyo ni kuhamasisha jamii umuhimu wa kupata chanjo ili kuzuia magonjwa yanayoweza kuzuilika kwa chanjo ambayo ni polio, donda koo, pepo punda, kichomi, kuharisha, surua na uti wa mgongo. 

“Ujumbe wa wiki ya chanjo mwaka huu, 2015 ni: “Jamii iliyochanjwa ni Jamii yenye Afya” na Kauli mbiu ni “Chanjo ni Zawadi ya Maisha. 


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...