Skip to main content

SERIKALI YASEMA UJENZI WA KITUO CHA MAFUTA NDIUKA NI SALAMA



Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza (mbele kulia) akitoa taarifa ya mkoa wa iringa ya mafanikio ya utekelezaji wa matokeo makubwa sasa (BRN) Julai, 2013 hadi kufikia Februari, 2015 wakati mkutano na waandishi wa habari jana. 


Serikali ya Mkoa wa Iringa imewatoa hofu wananchi kuhusu ujenzi wa kituo cha mafuta kinachojengwa eneo oevu (wetland) ya Mto Ruaha eneo la Ndiuka Ipogolo, Manispaa ya Iringa. 


Akitoa taarifa ya Mkoa wa Iringa ya mafanikio ya utekelezaji wa matokeo makubwa sasa (BRN) Julai, 2013 hadi kufikia Februari, 2015, kwa waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho hautakuwa na adhari zozote za kimazingira.


Alisema kuwa uongozi wa mkoa ulipata taarifa kuwa ujenzi wa kituo cha mafuta (petrol station) ulikuwa unatarajiwa kuanza katika Kiwanja Namba 30/1 Kitalu “A” kilichopo eneo la Ndiuka Ipogolo katika Manispaa ya Iringa. 


Aidha, alisema kuwa ujenzi huo ulikwisha pata kibali cha ujenzi kutoka manispaa baada ya kampuni ya Puma Energy Tanzania Limited, inayojenga kituo hicho, kuwasilisha cheti cha tathmini ya mazingira.


Alisema kuwa baada ya kupata taarifa hizi, uongozi wa mkoa uliona ni muhimu kujiridhisha juu ya usalama wa wananchi, kutokana na kituo hiki kujengwa katika eneo oevu la mto ruaha, ambao maji yake yanatumiwa na wananchi wengi. 


Aidha, wadau walisema ujenzi wa kituo hicho kinaweza kuwa chanzo cha ajali za magari kwa kuwa kinajengwa jirani na barabara kuu ya TANZAM na ile inayopandisha mjini Iringa.


Hatua zilizochukuliwa na mkoa, tarehe 29/12/2014, mkuu wa mkoa alimwandikia barua Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, Dkt. Binillith Mahenge (MB), kufika ili kusaidia kutoa ufafanuzi kuhusu ujenzi wa kituo hicho ikizingatiwa kuwa eneo hilo ni oevu.


“Waziri mara moja alimtuma Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Mazingira la Taifa (NEMC), Eng. B. T. Baya kufika mkoani na kukutana na uongozi wa mkoa na manispaa. Mkurugenzi mkuu wa NEMC akiambatana na wataalam wake alifika na kufanya kikao na uongozi wa mkoa na manispaa, ambapo maelezo ya kina yalitolewa juu ya mchakato wa kutoa cheti cha kuruhusu ujenzi wa kituo cha mafuta ulivyofanyika,” alisema mkuu wa mkoa.

Alisema kuwa baada ya maelezo ya mkurugenzi mkuu wa NEMC juu ya masharti aliyopewa mwekezaji (Puma Energy Tanzania Ltd) ili kuhakikisha ujenzi na uendeshaji wa kituo hauathiri mazingira, uongozi wa mkoa uliamua kiitishwe kikao cha wadau katika mradi huo ili NEMC pamoja na mwekezaji watoe ufafanuzi kwa hoja mbalimbali walizonazo wadau kuhusiana na ujenzi huo wa kituo.


Kikao cha wadau, tarehe 13/03/2015 wataalam wa NEMC pamoja na wamiliki wa kampuni ya Puma Energy Tanzania Limited walifika mkoani na kukutana na wadau, ambapo wadau walipata maelezo ya kina juu ya mchakato wa utoaji wa cheti cha tathmini ya athari kwa mazingira ulivyofanyika, na masharti yaliyowekwa ili kuhakikisha kuwa usalama wa maji na mazingira ya mto Ruaha, unazingatiwa. 


Alisema, uongozi wa mkoa, ukishirikisha wataalam na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, uongozi wa manispaa pamoja na wataalam, meneja na wataalam wa Tanroads, Iringa, wataalamu kutoka Bonde la Mto Rufiji, Mamlaka ya Maji mjini Iringa (IRUWASA), Mkurugenzi mkuu na wataalam wa NEMC na mwekezaji (Kampuni ya Puma Energy Tanzania Limited).


Katika kikao hicho wadau walipata nafasi ya kuhoji mambo mbalimbali waliyokuwa na wasiwasi nayo, hususan uchafuzi wa maji ya Mto Ruaha na hofu ya uwezekano wa kutokea ajali za magari katika barabara kuu ya Tanzam jirani na kituo hicho.


Kuhusu uchafuzi wa maji ya Mto Ruaha wadau walielezwa kuwa kwa kuzingatia eneo la kituo kuwa kwenye eneo oevu la mto ruaha, nemc waliagiza utafiti ufanywe ili kujua mwenendo wa maji katika eneo kinapojengwa kituo. 

Utafiti wa ki-haidrojia uliofanywa na Dr. Ibrahim Mjema wa Chuo cha Sua, ulithibitisha kuwa hakutakuwa na uchafuzi wa maji ya Mto Ruaha kutokana na mwenendo wa maji ya ardhini. 


Aidha, maji ya mvua yatakayotiririka yatadhibitiwa kwa kuongozwa kwenye mfereji unaoenda mtoni kabla ya kufika eneo la kituo. 


Alisema kuwa kituo kitajengwa nje ya eneo la Hifadhi ya barabara Kuu ya Tanzam na ile inayoingia mjini Iringa. 


Aidha, magari yanayoingia kituoni yataingia na kutokea katika barabara ya tanzam tu. Sharti hili litawezesha madereva wanaoingia au kutoka kituoni kuona kwa uwazi magari katika barabara kuu, kabla ya kuchepuka kuingia au kutoka kituoni.


“Baada ya wadau kuuliza na kufafanuliwa kwa kina hoja zote, wadau walielewa na kuridhika juu ya tahadhari zilizochukuliwa na masharti yaliyowekwa na NEMC kwa mwekezaji wakati wa ujenzi na uendeshaji wa kituo hicho,”Alielezea mkuu huyonwa mkoa. 


Maoni ya mkoa, kwa kuzingatia uchunguzi uliofanywa na mkoa pia ufafanuzi wa kina wa NEMC kwa wadau kuhusu ripoti ya tathmini ya athari kwa mazingira uliotolewa tarehe 11/03/2015, uongozi wa mkoa umeridhika na mradi huo kutokana na tahadhari zote zilizochukuliwa na zitakazoendelea kuchukuliwa na mwekezaji pia mamlaka zinazoshughulika na kudhibiti uharibifu wa mazingira.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...