Skip to main content

CCM WAZOA WANACHAMA WAPYA 200 MKWAWA



KATIBU wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Sixtus Mapunda amewataka vijana wa chama hicho kuwa wa kwanza kulinda amani hata pale chama chao kinapotukanwa bila sababu na wapinzani wao katika mikutano yao ya kisiasa.

Mapunda aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wake wa hadhara alioufanya nje ya Chuo Kikuu cha Mkwawa, mjini Iringa katika ziara yake ya siku tano aliyofanya mkoani Iringa kukiimarisha chama hicho.

Kabla ya mkutano huo, Mapunda alifanya mikutano na uzinduaji wa matawi mapya ya UVCCM katika wilaya za Kilolo, Iringa Vijijini na Manispaa ya Iringa.

“Mkisikia wapinzani wanafanya mkutano wao, na mkahamasika kwenda kuwasikiliza, nendeni na kawasikilizeni kwa adabu, wakiwakwaza kwa maneno yao rudini nyumbani mkapumzike,” alisema.

Mapunda alisema watanzania wanapaswa kuendelea kuiamini CCM kwasababu ina dereva anayejua kazi yake tofauti na wale wanaotaka kujifunza kazi hiyo wakiwa Ikulu.

Aliwataka wananchi wa manispaa ya Iringa na vitongoji vyake kujiandikisha kwa wingi katika daftari la kudumu la wapiga kura ili watumie haki yao kutimiza wajibu wao wa kuirudisha tena CCM madarakani.

“Msema kweli ni mpenzi wa Mungu, mwaka 2010 mlitupa dhamana ya kuendelea kuongoza nchi hii kwa miaka mitano mingine, kuna maeneo mlitupa mamlaka kamili, na kuna maeneo kwa makusudi mlitupatia wapinzani,” alisema.

Alisema jimbo la Iringa Mjini ni moja ya eneo ambalo wananchi wa manispaa ya Iringa waliamua kumchagua mbunge toka upinzani huku kura za Rais na madiwani zikitolewa kwa wingi kwa CCM.

“Katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, tusaidieni kututolea gunzi kwenye tochi ya CCM, gunzi hilo ni shiiida, linapinga bajeti, linapinga ujenzi wa maabara, linapinga katiba mpya, barabara na mengi yanayohusu maendeleo ya watu wa Iringa na Taifa,” alisema.

Alisema jambo kubwa linalosikitisha katika siasa za nchi ni kwamba wanaoamua kuwa wa kwanza kujipofusha ndio wale waliopata bahati ya kuona jua.

“Wanaokubali kujipofusha ni wale waliomaliza kidato cha nne, cha sita na vyuo vikuu. Siko tayari kuamini mwanafunzi wa chuo kikuu anawezaje kukubali kudanganywa, naloliona ni kama wanajidanganya wenyewe,” alisema.

Alisema baadhi ya wanafunzi hao wamekuwa vinara wa kushangilia na kupiga makofi wanapowasikia wapinzani wakiisema serikali ya CCM kwamba haijafanya kitu.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...