Skip to main content

DK. MAHENGE AHIMIZA USAFI, UTUNZAJI MAZINGIRA NCHINI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mzingira) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Makete, Dkt. Eng. Binilith Mahenge akisoma hotuba.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mzingira) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Makete, Dkt. Eng. Binilith Mahenge (mwenye tai ya bluu) akifurahia igizo wakati wa uzinduzi wa mradi wa mazingira wilayani Makete. Kulia kwake ni Diwani wa Iniho Jison John Mbalizi, Mkuu wa Chuo VETA-Makete Ramadhan Sebbo na Mwenyekiti wa Bodi wa CCDO Majaliwa Mayova.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mzingira) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Makete, Dkt. Eng. Binilith Mahenge (mwenye tai ya bluu) akikabidhi vifaa vya michezo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Makete (MDFA), Bosco Godigodi Mazangalila (kulia) kwa timu za mazingira (Environmental Clubs) wanaoshuhudia ni Meneja Mradi Agnes Mahenge na Mwenyekiti wa Bodi CCDO Majaliwa Mayova


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mzingira)  Dkt. Eng. Binilith Mahenge akionesha kitabu cha mazingira cha mwalimu cha kufundishia katika shule za msingi baada yakukizindua.




WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dkt. Eng. Binilith Mahenge (MB) ametoa wito kwa wananchi kuwa suala la usafi na utunzaji wa mazingira linaanza na mtu mmoja na hatimaye jamii nzima.

Dkt.  Mahenge alisema haya wakati wakuzindua miradi miwili ya hifadhi ya mazingira inayofadhiliwa na UNDP na Tanzania Forest Fund (TFF) kupitia Asasi ya Children Care Development Organization (CCDO) wilayani Makete, mkoani Njombe jana.

Mradi wa kwanza unaofadhiliwa na UNDP unalenga kuiwezesha jamii katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi na mwengine unaofadhiliwa na TFF unalenga katika upandaji miti ili kuboresha hifadhi ya misitu na chanzo cha maji eneo la Unyangogo katika Kata ya Iniho.

Miradi hiyo inatekelezwa na asasi ya CCDO, inayojishughulisha na kazi ya utoaji elimu ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi, utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji katika wilaya za Iringa na Makete.

Alisema kuwa ili kulinda afya zao wananchi hawanabudi kuyatunza mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo.

“Sote tumeshuhudia athari za mabadiliko ya tabianchi kama vile ukame uliokidhiri, mvua zisizotabirika, mafuriko, kuongezeka kwa joto, kuibuka kwa magonjwa kama malaria katika maeneo ambayo huko nyuma hayakuwa na historia ya magonjwa hayo; mfano katika baadhi ya maeneo ya Makete,” alisema.

Alisema kuwa malaria kwa sasa imeripotiwa katika mikoa mingi ikiwemo mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya na Kilimanjaro.

“Haya yote ni ushahidi wa uwepo wa mabadiliko ya tabianchi na yanatukumbusha kwamba sote tunao wajibu wa kuhifadhi na kulinda mazingira yetu ili kuilinda nchi yetu na dunia kwa ujumla kutokana na majanga yatokanayo na uharibifu wa mazingira,” aliongeza waziri huyo.

Alisema kuwa serikali inaendelea na juhudi za kulinda na kuhifadhi rasilimali za mazingira nchini kupitia utekelezaji na usimamizi wa sera, sheria, kanuni na miongozo.

“ Nitumie fursa hii kuzielekeza mamlaka za serikali na mitaa na taasisi za serikali kutekeleza kikamilifu matakwa ya sheria ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2004 kwa kuhuisha masuala ya hifadhi ya mazingira katika mipango yao ya maendeleo na bajeti zao za kila mwaka,” alisema.

Pia alitoa wito kwa asasi zisizo za serikali, taasisi za dini, na wadau wengine kushiriki kikamilifu katika juhudi za kuhifadhi mazingira na  kila mdau kwa nafasi yake.

Juma lililopita tarehe 22 Aprili, 2015, serikali ilizindua ripoti ya pili ya hali ya mazingira nchini. Ripoti hii inabainisha ongozeko la watu likiambana na kuongezeka kwa kasi kubwa ya uharibifu wa mazingira hususan misitu na vyanzo maji.

Ripoti pia imeanisha athari za mabadiliko ya tabianchi katika sekta za kiuchumu kama vile, kilimo, mifugo, uvuvi, miundombinu, wanayapori, uchukuzi, viwanda na afya.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi, Meneja wa Mradi, Agnes Mahenge alisema kuwa asasi ya children care development organization imekuwa ikijishugulisha na kazi ya kutoa elimu ya kupambana na athari za tabianchi, utunzaji wa mazingira na vyanzo maji kwa watoto na wanawake kwa lengo la kufanya watoto kuyapenda mazingira wakiwa bado wadogo na kuwa askari wema kwa nchi yao.

Pia alisema kuwa watoto kuwafanya wawe walimu wazuri kwa vizazi vijavyo hususan katika kutekelezaji wa sheria namba 20 ya mazingira ya mwaka 2004 katika kuwajengea uwezo wa uelewa, kupanua ajira na namna ya kupambana na umaskini wa kifikra na kipato.

Alisema kuwa shirika hilo limefanyikiwa kuunda timu 16  za mpira wa miguu kwa  wanaume, wanawake na watoto.

Timu hizi za mazingira ni za kudumu na lengo lake ni kuona timu hizi zinakuwa zikiendeshwa kwa mfumo wa ligi na kuwa na timu moja mama ambayo itapiganiwa kupanda daraja kwa kushiriki kwenye ligi kuu ya Vodacom huku ikifanya kazi ya kuhamasisha jamii kuhusiana na elimu ya mabadiliko tabianchi.

Wakati huohuo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mzingira) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Makete, Dkt. Eng. Binilith Mahenge alitoa vifaa vya michezo zikewemo jezi seti nne na mipra 20 kwa timu za mazingira (Environmental Clubs) kutoka halmashauri za Iringa na Makete.

Alisema kuwa lengo la kutoa vifaa hivyo ni kuona vijana wengi wa maeneo ya vijijini wanashirika kikamilifu katika kukuza vipaji vyao  pamoja na kutoa elimu ya uhifadhi wa mazingira.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...