Skip to main content

ELIMU ZAIDI YATAKIWA KUBADILI JAMII KUTHAMINI MAALBINO



Meneja wa Kituo cha Habari na Mawasiliano cha Redio Sengerema mkoani Mwanza Bw. Felician Ncheye akiwakaribisha mameneja wa Redio za jamii nchini (hawapo pichani) walioshiriki kwenye mafunzo ya siku moja ya kutoa elimu kwa Redio za jamii nchini juu ya kuandaa vipindi vyenye ujumbe sahihi wa masuala yanayohusu watu wenye Albinism iliofanyika katika kituo cha Redio Jamii Sengerema hivi karibuni. Katikati ni Afisa mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye Albinism la Under The Same Sun (UTSS), Kondo Seif na kulia ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.

Na modewjiblog team, Sengerema

Ofisa mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye Albinism la Under The Same Sun (UTSS) Kondo Seif, ameitaka jamii kuungana kupiga vita imani potofu zinazosababisha mauaji kwa watu wenye albinism.

Alisema jamii ikiamka na kuamua kumaliza tatizo hilo, mauaji hayo yatakoma.

Kauli hiyo aliitoa katika semina ya siku moja ya elimu kwa Redio za jamii nchini juu ya kuandaa vipindi vyenye ujumbe sahihi ya masuala yanayohusu watu wenye Albinism iliofanyika katika kituo cha Redio Jamii Sengerema mkoani Mwanza hivi karibuni.

Kondo alisema katika jamii kumekuwa na imani potofu ambapo Albinism wamekuwa wakiitwa majina yanayolenga kunyanyapaliwa na kusababisha kushamiri kwa vitendo vya ukatili na mauaji dhidi yao.

Aliitaka jamii kutambua kuwa albinism ni hali ya ukosefu wa rangi asilia mwilini inayoathiri ngozi, macho na nywele na ni nadra hali hiyo kupatikana na haiambukizi kama watu wengine wanavyodhani.

Aidha ametaja jina sahihi la Kiswahili lililokubaliwa na baraza la Kiswahili Tanzania kuitwa watu wenye albinism kuwa ni watu wenye ualbino.

Alisema watu wenye ualbino wamekuwa wakikabiliwa na changamoto za kukosekana kwa taarifa sahihi zinawagusa wao kama ngozi kushindwa kuhimili jua, uoni hafifu na kupungua kwa usalama.

Kwa mujibu wa Takwimu za shirika hilo watu wenye Albinism zaidi ya albino 70 nchini Tanzania wameuawa, zaidi ya 30 wamekatwa viungo vyao na makaburi ya watu wenye Albinism 20 yamefukuliwa.

Ameviomba vyombo vya habari kushiriki kikamilifu kutoa elimu sahihi kwa jamii ili kustawisha maisha ya watu wenye Albinisms kuwa kufanya hivyo maendeleo yao, jamii na taifa kwa ujumla yataimarika.

Awali akizungumza na washiriki wa semina hiyo Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliwataka waandishi wa habari kuzingatia matumizi sahihi ya lugha wanapoandika habari na kuandaa vipindi vinavyozungumzia masuala ya Albinism.

Pia amesisitiza kuandaa vipindi vinavyobeba ujumbe sahihi wa kuelimisha jamii juu ya masuala yanayohusu Albinism ili kubadilisha mitazamo ya jamii ili kuwathamini, kuwalinda, kuwaheshimu na kuwashirikisha katika maendeleo.

Sambamba na hilo amevitaka pia kubeba jukumu kubwa la kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la mpiga kura na kutoishia kujiandikisha tu bali wajitokeze kupiga kura kuwachagua viongozi ambao ni Madiwani, Wabunge na Raisi October 2015 pamoja na kuipigia kura katiba inayopendekezwa wakati ukifika.

Ameongeza katika matukio hayo muhimu ya kitaifa watu wenye Albinism wahamasishwe kushiriki kikamilifu vile vile na makundi mengine kama wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, wazee na makundi mengine maalum.


Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph akielezea dhima ya UNESCO kuwashirikisha shirika la Under The Same Sun (UTSS) kutoa elimu kwa Redio jamii ili kupaza sauti kwa jamii dhidi ya mauaji ya watu wenye Albinisim pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili walemavu wa ngozi.


Mshauri na Mkufunzi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Rose Haji Mwalimu akitoa mwongozo kwa washiriki wa semina hiyo.


Afisa mtetezi na ushawishi kutoka shirika linaloshughulika na watu wenye Albinism la Under The Same Sun (UTSS), Kondo Seif akiendesha mafunzo kwa mameneja wa Redio jamii nchini (hawapo pichani) kwenye semina ya siku moja iliyofanyika wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza. Katikati ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph.



Meneja wa Redio jamii Mpanda FM iliyopo mkoani Katavi, Prosper Kwigize akichangia maoni yake kwenye semina hiyo namna ya kudhibiti mauaji ya watu wenye Albinism iliyofanyika hivi karibuni wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza.


Meneja wa kituo cha Redio Jamii FADECO ya wilayani Karagwe, Adelina Lweramula akielezea jitahada za kituo chake cha Redio kinavyoshiriki katika kukemea mauaji ya watu wenye Albinism kwa kuendesha midahalo mbalimbali pamoja na makala maalum kuhusiana na walemavu wa ngozi.


Baadhi ya mameneja wa vituo vya Redio jamii nchini walioshiriki semina hiyo ya siku moja wakifuatilia kwa umakini mafunzo yaliyokuwa yakitolewa na Bwana Kondo Seif (hayupo pichani) wa Shirika la Under The Same Sun (UTSS).




Mkufunzi wa semina ya siku moja kwa Mameneja wa Redio jamii nchini Kondo Seif akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa semina hiyo.




KAWAIDA

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...