Skip to main content

JWTZ wavamia mitaani Songea, wazua taharuki

Songea/Dar. Wananchi wa Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma jana walikumbwa na taharuki baada ya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuvamia mitaa, ofisi za Serikali na binafsi, benki, nyumba za ibada na katika maeneo ya biashara wakiwa na silaha huku magari yao yakiranda kila kona na kuanza kuwapekea watu wote waliyekutana naye huku wakidai kuonyeshwa vitambulisho.


Hata hivyo, hiyo ni mara ya kwanza kwa wanajeshi hao kuchukua hatua hiyo ambayo ilielezwa kuwa ni sehemu ya mazoezi na mafunzo kwa vitendo.


Wananchi waliohojiwa na gazeti hili kwa nyakati tofuti kufuatia kizaazaa hicho akiwamo Anastazia Mhale alisema alikutana na wanajeshi hao alipokuwa akielekea benki, walimsimamisha na kumuuliza maswali kisha wakamfanyia upekuzi.


“Nilishangaa kusimamishwa na wanajeshi na kutuhoji maswali huku wakitutaka tuwaonyeshe vitambulisho, hali hii iliwakuta hata watu waliokwenda wanakwenda sokoni,” alisema Mhale.


Alisema mbali ya kuwakagua raia, pia walisimamisha kila gari barabarani na kulifanyia upekuzi sambamba na abiria waliokuwa ndani ya magari hayo.


Erasto Haule alisema: “Hata kama hakuna madhara yoyote wangetutangazia kama wanafanya mazoezi, wametutia hofu kubwa,” alisema.


Alisema baadhi ya watu jana walishindwa kutoka kwenda kuendelea na shughuli zao wakihofi kukamatwa na wanajeshi hao.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Mihayo Msikhela alipoulizwa alisema zoezi hilo ni la kawaida na aliwataka wakazi mjini humo kuwa na amani na waendelee kufanya shughuli zao kama kawaida.


Gazeti hili pia liliwashuhudia askari hao wa jeshi wakiwa wametanda eneo lote la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, lilipotaka kwenda kuonana na mkuu wa mkoa ili atolee maelezo zoezi hilo.


Alipoulizwa Brigedia Jenerali wa Kamandi ya Kusini, John Chacha alisema hiyo ni sehemu ya mafunzo kwa wanajeshi hao.


Alisema JWTZ hufanya mafunzo mbalimbali ya kujiimarisha ikiwamo ya kulinda miji, maporini na mengineyo.


“Mazoezi haya yameanza leo (jana) na tutamaliza usiku. Mafunzo hayo ni muhimu kwetu, yanatoa mbinu za kujihami na uvamizi wa adui yeyote anayeweza kuingia ndani ya mipaka yetu na kuteka viwanja vya ndege, ofisi nyeti za Serikali, benki au hospitali kubwa, ndiyo maana tunayafanya mahali popote,” alisema.


Hata hivyo, Brigedia Chacha alisema kabla ya kuanza kwa zoezi hilo, walitoa taarifa katika ofisi zote kuanzia ngazi ya kata hadi wilaya kwa lengo la kuondoa hofu ambayo ingeweza kutoa kwa wananchi. (CHANZO: MWANANCHI)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...