Skip to main content

Mashine 1,600 zaidi za BVR zawasili nchini


Dar es salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema uandikishaji wa wananchi kwenye Daftari la Wapigakura nchini utamalizika mwishoni wa mwezi ujao baada ya mashine 1,600 zaidi za kielektroniki kwa ajili ya kazi hiyo kuwasili juzi.


Ofisa ugavi mwandamizi wa NEC, Datus Matuma alisema mashine hizo zinazotumia teknolojia ya utambuzi wa alama za mpigakura (Biometric Voter’s Registration), zitaanza kupelekwa mikoa ya Mara, Arusha, Manyara na Kilimanjaro.


“Ule uvumi ambao ulikuwa ukienea nchini kwamba Tume ya Taifa haiwezi kumaliza uandikishaji, sasa umefikia mwisho kwani hizi mashine ni za kisasa na zitaanza kazi moja kwa moja kwenye mikoa hiyo niliyoitaja na mwishoni mwa mwezi Juni au mwanzoni mwa mwezi wa Julai watu wote watakuwa wameshaandikishwa,” alisema Matuma.


Alisema wananchi wajitokeze kwa wingi kujiandikisha ili wasikose haki yao ya msingi ya kupiga kura kwani kila aliyefikisha umri wa kupiga kura anatakiwa kujiorodhesha kwenye daftari hilo.


Alisema Serikali ni sikivu ndio maana imekata kiu ya Watanzania kwa kuleta mashine hizo ambazo sasa zimefikia 8,000 na zinakidhi kabisa mahitaji ya Watanzania wote kwani zinafika kila mkoa na zitagawiwa kwenye halmashauri kwa ajili ya kuzisambaza kwenye vituo vya uandikishaji .


BVR 250 ndizo za kwanza kuwasili na kutumika kwa majaribio katika majimbo ya Kawe, Kilombero na Mlele na baadaye kutumika kwenye uandikishaji mkoani Njombe.


Baadhi ya changamoto zilizojitokeza katika uandikishaji huo ni mashine kushindwa kutambua vidole sugu na kuchukua muda mrefu kuandikisha mtu mmoja. Hata hivyo changamoto hizo zilipatiwa ufumbuzi


Wadau wa uchaguzi walipokutana na NEC Februari 12, mwaka huu waliilalamikia tume hiyo kushindwa kuweka wazi ratiba, makadirio ya wapiga kura watakaoandikishwa, mzabuni wa vifaa hivyo, nchi vinakotoka, kiasi cha fedha kilichotolewa na serikali na kampuni inayohusika kuweka mfumo wa ndani wa mashine hizo.


Aprili 2, NEC ilitangaza rasmi kushindikana kwa kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa iliyokuwa imepangwa kufanyika Aprili 30 baada ya kushindwa kumaliza kuandikisha wapigakura kama inavyopanga.


NEC ilisema uandikishaji utaendelea na kwamba hadi kufikia Julai, mwaka huu watakuwa wamemaliza nchi nzima na kwa kushauriana na Tume ya Uchaguzi Zanzibar watatangaza tarehe ya Kura ya Maoni.


Uhaba wa BVR uliwapa wasiwasi wadau wengi hususani vyama vya siasa kwamba uandikishaji hautakamilika kufikia Julai na kwamba hali hiyo inaweza kusababisha kuahirishwa kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.


Hata hivyo, mwezi uliopita NEC ilitangaza kwamba hakuna mpango wowote wa kuahirisha Uchaguzi Mkuu na kusisitiza kuwa utafanyika kama ilivyopangwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...