Skip to main content

TDBP KUJENGA MITAMBO YA BIOGESI 4000 NCHI NZIMA

Mratibu wa Program ya Biogesi Tanzania (TDBP), Cyprian Shila (kulia) akibadilishana na mawazo na mmoja ya watendaji wa Mkoa wa Njombe baada yakumalizika kwa semina ya wakulima wa kilimo hifadhi pamoja na biogesi.

Dr. Rehema Nchimbi(katikati), ambaye pia ni Mkuu wa Njombe akiongea na wakulima wakati wiki ya wakulima watatifi katika kilimo hifadhi na biogesi jana. Waliyeketi toka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Waging'ombe, Frederick Mwakalebela na Mkuu wa Mradi Kilimo Hifadhi, Profesa Ndelilio Urio kutoka SUA.
    

Wakulima wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Dkt. Rehema Nchimbi wakati wa wiki ya wakulima mkoani Njombe.



Njombe: Mratibu wa Program ya Biogesi Tanzania (TDBP), Cyprian Shila amesema watasimika mitambo ya biogesi 4,000 kwa nchi nzima ukiwemo mkoa wa Njombe mwaka huu katika mpango wa utekelezaji kwa kushirikiana wadau mbalimbali katika sekta ya hiyo. 

Shila alisema kuwa lengo la kusimika mitambo ya biogesi nchi nzima sio tu kwa kuleta maendeleo kwa wananchi tu, lakini pia kutasaidia kusafisha hewa ya ukaa ya methane (CH4) inayotokana na kuwepo wingi wa mifugo.

Hayo yalibainika wakati wa wiki ya wakulima watatifi katika mradi wa kilimo hifadhi (conservation agriculture) iliyoandaliwa na Chuo cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kwa kushirikiana na Programu ya Biogesi Tanzania (TDBP) iliyofanyika mkoani Njombe Ijumaa wiki iliyopita.

Alisema kuwa katika harakati za kupunguza hewa ukaa ya methane inayotokana na vinyesi vya mifugo kunakopelekea mabadiliko ya tabianchi (climate change), programu ya biogesi Tanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali watasimika mitambo hiyo ya biogesi kwa kulima.

“ Miradi ya biogesi unatumia kinyesi cha binadamu na wanyama wanaozalisha hewa ya ukaa ya methane ambayo inachangia kuchafuzi wa hali ya hewa inayosababisha mabadiliko ya tabianchi kutaokoa pia mazingira yanayoharibika kutokana na kukata miti kwa matumizi ya nishati ya kuni na mkaa,” alisema.

Alisema ili kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana ukataji miti ovyo na kulima kilimo kisichozingatia huhifadhi, program hiyo itajenga mitambo ya biogesi pamoja kuhamasisha wananchi kutumia biogesi ilikujiletea maendeleo yao wenyewe na hatimaye kuboresha maisha kwa kupunguza umasikini.

Mratibu huyo alitoa wito kwa Watanzania kuanza kutumia nishati mbadala ya biogesi kwa kupitia kilimo hifadhi ambacho alisema ni mkombozi kwa wakulima.

Alisema matumizi ya biogesi vijijini kutasaidia kupunguza muda kwa kinamama na watoto wakike kutumia muda mwingi wa kutafuta kuni kwa ajili ya kupikia.

Mkuu wa Mradi Kilimo Hifadhi, Profesa Ndelilio Urio, Makamu Mkuu wa Mradi, Dr. Peter Mtakwa na Afisa Kilimo, Alpha Mtakwa toka SUA walisema kuwa killimo hifadhi ni kilimo ambacho hupunguza matumizi ya nguvu kazi huku kikiongeza tija.

Walisema kuwa kilimo hifadhi hakihitaji mkulima kulima kwa kugatua udongo mashambani lakini kuchimba mifereji kwa ajili ya kupanda mbegu kwa kutumia mbolea ya samadi inayotokana na tope chujio (bioslurry) pamoja na mbolea za madukani.

Walisema kuwa kilimo hifadhi hupunguza muda wa kuhudumia mashamba kwa vile hutumia dawa ya kuuliwa magugu mashambani na kupunguza muda wakupalilia kwa kutumia jembe la mkono.

Walisema kuwa kwa vile udongo mwingi una upungufu wa rutuba kwa hiyo wakulima wameshauriwa kutumia mbolea mchanganyiko ili kuweza kupanda mavuno mengi.

Kwa upande wake mgeni rasmi katika maadhimisho ya wiki ya wakulima, Dr. Rehema Nchimbi, ambaye pia ni Mkuu wa Njombe alisema kuwa kilimo hifadhi ni mkombozi wa uharibifu wa mazingira nchini pamoja na matumizi ya biogesi, kutokana na mkoa huo kuwa na hali ya hewa inayofaa kwa kilimo.

Alisema kuwa kilimo hifadhi na tope chujio inayotokana na matumizi ya biogesi kutasaidia kurudisha rutuba katika ardhi.

Alisema mkoa wa njombe unatakiwa kuwa shamba darasa la nchi kwa kulimo hifadhi na matumizi ya biogesi kwa sababu mkoa huo hauna tatizo la migogoro ya ardhi.

Alisema kuwa migogoro mingi nchini inatokana na wafugaji wanaotangatanga na mifugo kumbe wafugaji hao wangetumia kulimo hifadhi na kuwekeza katika teknolojia ya biogesi kunawaza kupunguza migogoro mingi ya ardhi.

Awali, watafiti toka SUA, TDBP, maofisa ugani, wakulima watafiti na wadau mbalimbali walitembea shamba la utafiti Nyumbanitu Cosmas Mfugale ni mkulima wa mfano aliyepata maendeleo makubwa kwa kutumia nishati mbadala ya biogesi lililopo katika Wilaya ya Wanging’ombe, mkoani Njombe.

Kijiji hicho cha Nyumbanitu kina jumla ya wakulima watafiti nane wanaonufaika na mradi wa kilimo hifadhi ambaye pia wamejenga mitambo ya nishati mbadala ya biogesi.

Wakati huohuo, mratibu wa program ya biogesi Tanzania, Cyprian Shila atangaza kuwa maadhimisho ya siku ya biogesi kitaifa mwaka huu itafanyika tarehe 10 mwezi wa tisa mwaka huu katika mkoa wa Njombe.

Mkoa wa njombe ina jumla ya wakulima therathini ambao wanatumia kilimo hifadhi na wanatumia mitambo ya biogesi ambao walielezea faida za kilimo hifadhi na mitambo ya biogesi.




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...