Skip to main content

TTCL YATOA MSAADA WA KOMPYUTA KUMI KWA GLOBAL OUTREACH





KUMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imekabidhi kompyuta kumi (10) pamoja na kifurushi cha intaneti ya bure yenye kasi ya 2Mbps kwa muda wa miezi sita vyote vikiwa na thamani ya 20,197,600/- kwa ajili ya Iringa Secondary School Internet Library (ISSIL).

Kampuni ya simu hiyo ya kizalendo ambayo inatoa huduma mbalimbali  za mawasiliano nchi imetoa misaada hiyo Global Outreach Tanzania ili kuunga mkono mradi wa maktaba mtandao (intaneti) katika kuboresha mfumo wa elimu nchini.


Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dr. Kamugisha Kazaura, Meneja wa Kanda Nyanda za Juu Kusini, Juvenal Utafu alisema kuwa TTCL in moja ya wadau muhimu katika kuboresha sekta ya elimu nchini kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHEMA/ELIMU MTANDAO).

Alisema jana kuwa kampuni imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia juhudi zinazofanywa na serikali na wadau wengine katika kuboresha mfumo wa elimu kwa ajili ya maendeleo ya nchi yetu.

“Ili kuungana na Global Outreach Tanzania katika mradi huu mkubwa TTCL imetoa kompyuta kumi (10) pamoja na kifurushi cha intaneti ya bure kwa miezi sita,” alisema.

Alisema kuwa kituo hicho kitasaidia kuleta manufaa kwa wanafunzi wote pamoja na walimu wao na kuwaasihi wanafunzi na walimu kutumia kituo hicho ipasavyo ili kujiendeleza kielimu na kutanua wigo wa maarifa kupitia intaneti (elimu mtandao).

Hata hivyo, meneja wa kanda hiyo aliwaasa vijana wote waitumie huduma hiyo ya intaneti kwa malengo yaliyo kusudiwa na kuachana na matumizi mengine yasiyo na tija, ambayo yanapatikana kwenye intaneti kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza ambaye aliwakilishwa na Afisa Elimu Mkoa Eusedius Mtavangu alipokea msaada huo kwa niaba ya Global Outreach Tanzania katika hafla fupi iliyofanyika katika Kituo cha Kichangani Student Center mjini Iringa.

Mkuu wa mkoa huyo alitoa shukrani za dhati kwa uongozi na wafanayakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) kwa juhudi za kuinua sekta ya elimu pamoja na sekta zingine.

“Jambo hili ni mfano wa kuigwa kwa makampuni mengine, sisi kama serikali tunatambua mabadiliko na ukuwaji wa tecknolojia kwa kasi ambao si budi kwa Tanzania-tukiwemo wanairinga, tujiandaa vyema ili kukabiliana na maendeleo hayo ili tusibaki nyuma,” alisema.

Pia alilipongeza shirika lisilo la kiserikali la global outreach Tanzania kwa kuanzisha mradi wa kuinua elimu kupitia teknolojia ya habri na mawasiliano.

Aidha, aliwaasa wanafunzi, walimu na wadau wengine wanaotumia kituo hicho kama chachu au njia ya kujiongezea maarifa, kutumia intaneti kutafuta vitabu au taarifa ambazo zitawasaidia katika masomo.

Pia kuelewa dunia sasa inakwendaje kiuchumi, kisiasa, na kisayansi pamoja na kutumia intaneti katika lengo la kutafuta fursa mbalimbali za masomo, kubalishana mawazo na wataalam kwa nia njema na sio kinyume chake.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Global Outreach Tanzania, Francis Mwachombe alisema shirika hilo lilianzishwa na Stan Muessle mwaka 1998 chini ya Global Outreach U.S.A na kusajiliwa mwaka 2007 kama Global Outreach Tanzania.

Lengo kuu la shirika hilo ni kuingiza elimu ya teknolojia ya kompyuta katika mihtasari ya shule za sekondari ili kuongeza ufaulu.

Shirika hilo limefanya na linafanya kazi na shule za sekondari za Pomerini, Image, Bomalang’ombe, Nyerere, Lugalo, Shule ya Sekondari ya Wasichana Iringa, Mafinga Seminary, Ifunda Shule ya Ufundi, St.     Micheal, Mawelewele, St. Joseph Ipogolo, Mtera na Cagliero.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...