Skip to main content

VIGOGO WANNE WANAODAIWA KUFUKUZWA KAZI WA TALGWU KILOLO YAWATETEA

Mwenyekiti wa TALGWU Kilolo, Andrea Mwandimbile

CHAMA cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU), wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa kimepinga uamuzi wa halmashauri ya wilaya hiyo, wa kuwafuta kazi vigogo wake wanne.

Taarifa iliyotolewa juzi na Mwenyekiti wa TALGWU wa wilaya hiyo, Andrea Mwandimbile kwenye mkutano mkuu wa chama hicho, inaonesha vigogo hao wamefukuzwa kazi hivikaribuni baada ya kusimamishwa kazi Oktoba mwaka jana.

Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya hiyo, Rukia Muwango hakuweza kupatikana kuzungumzia sababu za watumishi hao “vigogo” kufutwa kazi kama ilivyodaiwa na chama hicho.

Vigogo hao wametajwa katika kikao hicho kuwa ni pamoja na mweka hazina wa halmashauri hiyo Eriekel Mbise, mwanasheria wa halmashauri Alto Lixolelo, afisa misitu wa halmashauri Godfrey Mwita na afisa ununuzi wa halmashauri Alex Mkuba.

Novemba mwaka jana, mkurugenzi wa halmashauri hiyo, alitoa kwa wanahabari taarifa iliyohusu kusimamishwa kazi kwa vigogo hao kwa kile alichosema ni kwa ajili ya kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizoelekezwa dhidi yao.

Wakati akitoa taarifa hiyo, Muwango alisema watumishi hao wanahusishwa katika mikataba tata iliyoisababishia halmashauri hiyo hasara na akakataa kutoa ufafanuzi wa hasara hiyo akidai kwamba ingekuwa ni “sawa na kuingilia suala linaloendelea kufanyiwa kazi.”

Aliitaja mikataba hiyo kuwa ni ile inayohusiana na uvunaji wa miti katika msitu wa halmashauri hiyo na wa kampuni ya New Forest inayozalisha nguzo katika eneo la Viwengi wilayani humo.

“Siwezi kufafanua nini kipo katika mikataba hiyo na hawa watumishi wanatuhumiwaje katika mikataba hiyo. Kwa kuwa wanatakiwa kujieleza au kujitetea, tunasubiri wafanye hivyo ili haki iweze kutendeka” alisema.

Katika mkutano huo, mwenyekiti wa Talgwu alisema; “kuna kila dalili kwamba watumishi wenzetu hao wamefukuzwa kazi katika mazingira yanayoashiria kutofuatwa kwa kanuni, taratibu na maadili ya utumishi wa umma.” alisema.

Aliwauliza wajumbe zaidi ya 80 waliohudhuria mkutano huo kama wanakubaliana na maamuzi ya halmashauri hiyo ya kuwafukuza kazi watumishi hao na kwa pamoja walijibu “hatukubaliani” huku wakipiga meza.

Mkanda mzima wa kilichojiri katika mkutano huo kukujia kupitia mtandao huu hivi punde... 

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...