Skip to main content

GRL YAGAWA MICHE YA MITI MILIONI TANO KWA WANANCHI KUANZISHA MASHAMBA BINAFSI

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mufindi (DED), Saada Malunde (mwenye hijabu) akipata maelezo kutoka kwa mtaalum wa uzalishaji miche, Prosper Wilbright (pili kulia) ya jinsi Kampuni ya Green Resources Ltd hiyo inavyozalisha miche ya miti kitaalamu alipotembelea bustani hiyo ya kuzalisha miche mbalimbali iliyopo katika Kijiji cha Mabaoni wilayani Mufindi, Mkoa wa Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mabaoni, Sailas Ndenga (kushoto) akipekea akipokea funguo ya jengo kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Green Resources Ltd, Anthony Kisondella wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika Kijiji cha Mabaoni, wilayani Mufindi, mkoani Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)



Green Resources Ltd (GRL) imegawa zaidi ya miche milioni tano (5,000,000) kwa wananchi wa vijiji pamoja na kupatiwa mafunzo ya namna ya utunzaji na upandaji wa misitu.

Kaimu Mkurugenzi wa GRL, Anthony Kisondella kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji, Roselyne Mariki, alisema kuwa hekta zinazokadiriwa kufikia 20,000 zimepandwa miti katika mashamba binafsi ya wanavijiji.

Alitoa rai wakati wa kukabidhi jengo la ukumbi na ofisi kwa Kijiji cha Mabaoni, Kata ya Makungu katika Wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa jana.

Green Resources Ltd (GRL) ni kampuni tanzu ya Green Resources AS ya Norway, na imewekeza katika sekta ya misitu ikiwa na mashamba makubwa ambapo hekta 17,000 tayari zimepandwa miti katika wilaya za Mufindi na Kilombero.

“Kampuni ya GRL itaendelea kushirikiana kwa dhati na halmashauri za wilaya ya Mufindi na Kilombero na jamii za vijiji ilipowekeza katika kutekeleza miradi inayolenga kuboresha maisha wa wananchi,” alisema.

Kaimu mkurugenzi huyo aliwataka wananchi kutoa ushirikiano unaostahili na michango iliyo ndani ya uwezo wao kama nguvukazi na vifaa kama mawe, matofali na mchanga.

Alisema kuwa mradi wa ujenzi wa jengo la ukumbi na ofisi kwa ajili ya serikali ya Kijiji cha Mabaoni ulianza rasmi Oktoba mwaka jana, ambapo ujenzi wake uligharimu jumla ya shilingi 66,439,456/-.

Aidha, alisema jamii ilishiriki kwa kiasi kikubwa kutoa nguvukazi wakati wa utekelezaji wa mradi huu.

“Jengo hili lina ukumbi wenye uwezo wa kuchukua watu 200 kwa ajili ya kufanyia mikutano, sherehe na semina na vilevile jengo hilo lina vyumba vinne vya ofisi na vyumba viwili vya kuifadhia wahalifu, ” alisema.

Alisema kuwa ujenzi wa jengo hilo ulisimamiwa kwa niaba ya GRL na shirika linaloitwa ‘Southern Highlands Participatory Organization (SHIPO)’ lenye makao yake makuu mkoani Njombe.

Kampuni ya GRL imekabidhi rasmi Serikali ya Kijiji cha Mabaoni jengo la ukumbi na ofisi mbele ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi, ili kama wamiliki waweze kulitumia kulingana na malengo yaliokusudiwa.

“Moja ya mikakati ambayo Kampuni ya GRL imejiwekea ni kushirikiana na jamii kwenye maeneo iliyowekeza kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya jamii katika sekta ya afya, elimu na kadhalika inaotokana na mahitaji na vipaumbele vya jamii husika,” alisema kaimu mkurugenzi mtendaji.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mufindi (DED), Saada Malunde ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika makabidhiano ya jengo la ukumbi na ofisi kwa Kijiji cha Mabaoni, aliishukuru kampuni ya GRL kwa msaada huo.

Aidha, DED huyo aliwaasa wananchi wa Kijiji cha Mabaoni kwa kuhakikisha wanatunza vizuri jengo na endapo kutatokea uharibifu wowote, basi watafanya matengenezo yanayotakiwa.

Alisema kuwa serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji nchini.

“Na faida ya uwekezaji ni kama haya matunda tunayoyaona leo kwa kijiji cha Mabaoni,” aliongezea.

Naye, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Mabaoni, Sailas Ndenga aliishukuru Kampuni ya GRL kwa msaada huo kwa niaba ya wananchi wake na kuahidi kushirikiana na kampuni hiyo kwa lengo la koboresha maisha ya wananchi.

Alisema kuwa wakati anatoa ardhi hiyo kwa kampuni ya GRL, wapo wananchi waliothubutu kumnyoshea vidole kwamba ameuza ardhi ya kijiji kwa mwekezaji, lakini leo wanaona matunda yake.

Aidha, kampuni hiyo ya Green Resources Ltd ina bustani kubwa ya kuzalisha miche iliyopo Kijiji cha Mabaoni.

Mashamba mengine ya miti yapo kwenye vijiji vya Mapanda, Chogo, Ukami, Incomet na Idete kwa Wilaya ya Mufindi na vijiji vya Uchindile, Masagati na Kitete kwa Wilaya ya Kilombero.




Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...