Skip to main content

KONGAMANO LA UPATIKANAJI WA FEDHA ZA NDANI ZA MAENDELEO LAFANYIKA JIJINI ARUSHA




Mratibu Mkazi Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UN) na Mwakilishili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez ambaye alikua mgeni rasmi katika Kongamano la upatikanaji wa fedha za ndani za maendeleo akitoa hotuba yake kwa washiriki kutoka Halmashauri za wilaya nchini lililofanyika jijini Arusha.




Mkuu wa Mfuko wa Umoja wa mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF) nchini na Meneja wa LFI duniani, Peter Malika akizungumza wakati Kongamano hilo.


Mkurugenzi wa Huduma(Tamisemi), Denis Bandisa akizungumza wakati Kongamano ambalo pamoja na mambo mengine alizitaka halmashauri nchini kubuni vyanzo vya ndani vya mapato badala ya kutegemea wafadhili.


Washiriki kutoka maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi wakifatilia kwa makini mada katika Kongamano hilo.


Washiriki kutoka maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi wakiwa katika picha ya pamoja, Kongamano hilo limefanyika katika hoteli ya Mount Meru jijini Arusha.

Na Mwandishi wetu, Arusha

MFUKO wa Umoja wa Mataifa wa Ukuzaji Mitaji (UNCDF) kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), umeitisha kongamano la siku mbili la upatikanaji wa fedha za ndani kwa maendeleo.

Kongamano hilo linahusisha wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa nchini Tanzania na linashirikisha watu 110.

Pamoja na wakurugenzi hao, wapo na wawakilishi kutoka Serikali Kuu na wawakilishi walioteuliwa kutoka serikali za mitaa za Uganda, Senegal na Benin.

Kwa mujibu wa taarifa ya UNCDF, nia ya kongamano hilo ni kuonesha mafanikio ya mfumo wa ukusanyaji wa fedha za ndani kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi ya kibiashara katika nchi za Tanzania na Uganda.

Taarifa hiyo imesema kwamba baada ya kujifunza mafanikio hayo washiriki watajadiliana na kujipanga kwa ajili ya utekelezaji wa mfumo huo katika nchi zao wanaokotoka ili kupiga hatua mbele katika uendelezaji wa miradi bila kutegemea fedha za nje.

Akizungumza wakati wa ufunguzi Katibu Mkuu Tamisemi, Jumanne Sagini alisifu kazi inayofanywa na programu ya uwezeshaji wa fedha za ndani kwa maendeleo ( Local Finance Initiative- LFI) chini ya sekretarieti ya UNCDF kwa ubunifu wake unaowezesha kupatikana kwa mitaji ya kuwekeza katika miradi ya maendeleo inayofadhiliwa na serikali za mitaa.

Aidha alielezea dhamira ya serikali ya kutumia mfumo huo ulioasisiwa na UNCDF kwa kuufanya uwe wa kitaasisi zaidi ili kuweza kusaidia kutekeleza mipango ya maendeleo na uwekezaji ya serikali za mitaa.

Akizungumzia umuhimu wa kongamano hilo, Mgeni rasmi, Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Alvaro Rodriguez, aliipongeza serikali ya Tanzania kwa kufuata mfumo wa utafutaji wa fedha za ndani kwa ajili ya kukuza uwekezaji katika miundombinu ya kibiashara inayoleta mabadiliko kwa umma.

Rodriguez alisema katika hotuba yake kwamba kwa kuwezesha mfumo wa UNCDF LFI kwenye serikali za mitaa ndio jibu la uhakika la uwekezaji wenye mafanikio endelevu kwa taifa zima.

Aidha alisema mpango huo wa LFI ambao umekuwepo nchini kwa miaka mitatu na kuwezesha kuleta mabadiliko katika jamii, unafaa kumilikiwa na jamii ili kuwezesha mafanikio ya juu katika uwekezaji.

Mratibu huyo alisema kwamba Umoja wa Mataifa kupitia UNCDF utaendelea kufanyakazi na serikali ya Tanzania,kwa kuwa wanaamini kwamba vita dhidi ya umaskini itafanikiwa kwa kuhamisha mitaji na kuipeleka katika ngazi za chini kwa maendeleo ya wananchi.

Kongamano hilo ambalo ni mwendelezo wa uwezeshaji na kubadilishana uzoefu na elimu kwa lengo la kuwezesha miradi ya umma na binafsi inayochagiza maendeleo kujengwa; katika siku ya kwanza ya kongamano hilo washiriki wataoneshwa miradi iliyotekelezwa manispaa ya Busia Uganda na Kibaha nchini Tanzania.

Manispaa ya Busia imejenga kituo cha malori, ushuru wa forodha na maeneo ya kufanyia biashara, wakati Kibaha wamejenga kituo cha kisasa cha mabasi na soko.

Timu ya wataalamu wa UNCDF watawafundisha washiriki kwa siku 2 kuhusu miradi ya maendeleo, awamu za malipo ya fedha na mikakati ya kupata fedha na malipo na mbinu za kupunguza hatari za kibiashara.

Akisisitiza umuhimu wa kongamano hilo Mkuu wa UNCDF nchini na Meneja wa LFI duniani Peter Malika alisema kwamba kongamano hilo linatoa nafasi kwa watumishi wa serikali za mitaa na wengine kujifunza namna mpya ya kupata mitaji kwa kutumia vyanzo vya nyumbani ili kufadhili miradi ya miundombinu ya kiuchumi inayohitajika kwa ajili ya kutoa fursa za ujasiriamali , biashara, uwezeshaji, ajira, kuboresha maisha ya watu, ukusanyaji kodi na utoaji huduma.

Kongamano hilo la siku 2 ni miongoni mwa juhudi kadha za UNCDF za kuwezesha serikali za mitaa kufikia maendeleo endelevu na kuleta athari chanya kwa jamii ili kuondoa umaskini.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...