Skip to main content

LUKUVI: MAOFISA ARDHI NDIO CHANZO CHA MIGOGORO YA ARDHI MIJINI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa wilaya ya iringa na manispaa ya iringa, kuhusiana na migogoro ya Ardhi inaokabili wananchi hao pamoja na kutowalipwa fidia ya maeneo yao. (Picha Friday Simbaya)

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (kulia) akizungumza na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Iringa kuhusiana na migogoro ya ardhi inaokabili wananchi pamoja na kutowalipwa fidia baada ya maeneo kupolwa. Waziri huyo alikuwa mkoani hapa ziara ya siku moja ya kikazi ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea masijala ya ardhi za Manispaa ya Iringa na wilaya ya Iringa. (Picha Friday Simbaya)


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (kushoto) akioneshwa ramani ya mpango kabambe ya matumizi bora ya ardhi ya miaka 20 ijayo (2015-2036) na Afisa Ardhi wa Manispaa Willclif Benda (katikati) anayeshuhudia ni Mkrugenzi wa Mtendaji wa Manispaa ya Iringa Ahmed Sawa (kulia). Waziri huyo alifanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani hapa ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea masijala za ardhi za Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Iringa jana. (Picha Friday Simbaya)


Sehemu ya wananchi wa Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Iringa Vijijini waliofika kumsikiliza Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi (hayupo pichani) kuhusiana na migogoro ya ardhi inaokabili wananchi hao jana. Waziri huyo alifanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani hapa ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea masijala za ardhi za Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Iringa jana. (Picha Friday Simbaya)


IRINGA: Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema asilimia kubwa ya migogoro ya ardhi mijini inasababishwa na maofisa ardhi.

Lukuvi alisema hayo alipofanya ziara ya siku moja ya kikazi mkoani Iringa, ambapo pamoja na mambo mengine alitembelea masijala ya ardhi za Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Iringa jana.

Waziri huyo aliongea na viongozi mbalimbali wa mkoa na wananchi wa Manispaa ya Iringa na Wilaya ya Iringa Vijijini kuhusiana na masuala yanayohusu sekta ya ardhi mkoani humo katika ukumbni wa mikutano wa Siasa ni Kilimo. 

Alisema kuwa migogoro mingine ya ardhi inasababishwa kwa sehemu kubwa na maofisa ardhi na baadhi ya wananchi wakorofi kwa kushirikiana maofisa ardhi. 

Akizungumza na viongozi na wananchi wa mkoa wa Iringa, Waziri wa Ardhi Nyumba na Mendeleo ya Makazi Mh William Lukuvi alisema Wizara imepunguza kwa zaidi ya nusu gharama za upimaji ardhi kutoka 800,000/- hadi 300,000/- ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati suala ambalo litapunguza kwa kiasi kikubwa migogoro ya ardhi ambayo imekuwa inatokea.

“Wizara imepunguza kwa zaidi ya nusu gharama za upimaji ardhi kutoka 800,000/- hadi 300,000/- ili kila mwananchi aweze kupima eneo lake na kupata hati na kwa upande wa hati mliki za kimila, wizara imepunguza kodi ya ardhi kutoka 1,000/- hadi 400/- kwa ekari moja kwa mwaka kwa maeneo ya vijijini,” alisisitiza Lukuvi.


Aidha Lukuvi aliongeza kuwa sambamba na kupunguza migogoro ya ardhi, serikali pia itaweza kukusanya kwa wingi kodi ya pango la ardhi na hivyo kuongeza mapato amabayo yataisiaidia serikali katika kufanikisha shughuli za maendeleo. 


Hata hivyo pamoja na kupunguza gharama hizo Wazrizi Lukuvi aliwaonya Maofisa ardhi, kuacha tabia ya kuendesha shughuli za serikali kwa kukiuka taratibu, akitolea mfano wa maafisa hao kupima viwanja juu ya viwanja suala ambalo limekuwa linaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi.


“Maafisa ardhi lazima wafanye kazi kwa kuzingatia taratibu ili kuepusha migogoro ambayo inatokea miongoni mwa wananchi na kuwasababisha kuichukia serikali yao” alisema Lukuvi.


Waziri Lukuvi alikuwa na ziara ya siku moja kwa shughuli za kikazi mkoani Iringa, ambapo pamoja na mambo mengine aliwaasa viongozi wa mkoahuo kutafuta suluhu ya migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali ya mkoa.

“Msitumie nguvu kubwa kutatua migogoro ya ardhi kwa sababu kwa kufanya hivyo mtaleta madhara makubwa kwa wananchi, lakini mtumie njia ya mazungumzo kutatua migogoro hiyo. Uzoefu unaonesha kwamba mahali palipotumika nguvu kubwa ya kutatua migogoro pameshindwa kuleta suluhu ya migogoro hiyo,” aliwaasa viongozi wa mkoa.



Awali, Katibu tawala wa mkoa wa Tabora Wamoja alimweleza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa kwa sasa Mkoa wa Iringa una migogoro mitatu mikubwa ya ardhi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...