Skip to main content

Membe azoa wadhamini Iringa


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amezoa wadhamini 380 mjini Iringa.

Wadhamini hao kutoka wilaya zote tatu za mkoa wa Iringa walianza kukusanyika katika ukumbi wa chama hicho mjini Iringa majira ya saa 7 mchana hadi saa 4 usiku, kumsubiri Membe akitokea mkoani Njombe.

Akiwashukuru wadhamini hao, Membe alisema; “miongoni mwa ngome zangu kubwa sana za kisiasa nchini ni mkoa wa Iringa. Katika Uchaguzi wa Halmashauri Kuu ya Taifa, wajumbe wa mkoa wa Iringa walinipa kura zao zote.”

Alisema CCM ina utaratibu mzuri wa kuchuja na kupitisha viongozi wa kitaifa na kwa ukubwa wake ndio sababu kuna wagombea wengi wa urais wanaojitokeza kuwania nafasi hiyo.

“Watanzania msikiache chama hichi, tuna marafiki duniani kote, ni chama ambacho kimesaidia kupatikana kwa Uhuru kwa nchi zaidi ya nane barani Afrika.

Akizungumzia nafasi anayoiwania, Membe alisema; “urais haujaribiwi wala sio kazi ya kukurupuka, ni lazima uwe umejipanga na wenzako waamini kwamba wewe unaweza kugombea na lazima uwe na hekima na busara.”

Huku hotuba yake ikikatizwa mara kwa mara na shangwe na vifijo toka kwa wadhamini hao, Membe alisema uzoefu wa uongozi alionao ndani na nje ya nchi umemsukuma kuomba nafasi hiyo.

“Nikijaaliwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, angalieni timu nitakayojenga, baraza la mawaziri nitakalochonga, litakuwa na vijana, wanawake na wazee kwasababu wazee ni dawa,” alisema.

Alisema anataka kuiondoa nchi hapa ilipo na kuipeleka kwenye uchumi wa viwanda vitakavyotegemea kilimo na akawaponda wagombea wasiojua nini wanatakiwa kufanya endapo watachaguliwa kwa kisingizio kwamba wanategemea vipaumbele vyao vipo kwenye Ilani.

Aidha, alisema akichaguliwa kuwa rais atahakikisha atajenga uchumi wa viwanda ili mazao ya kilimo yaweze kusindikwa nchini.

Alisema kuwa kwa muda mrefu nchini inasifika kuwa namba moja kwa kuzalisha malighafi ambayo inanufaisha nchi zingine ambazo zinapata faida kubwa kuliko sisi.

Alisema akiwa rais atahakikisha anafufua viwanda vikiwemo vya Iringa ili viweze kuajiri watu wengi na hatimaye kupunguza umaskini.

Alisema kuwa mgombea yeyote anayetumia nguvu ya fedha kuwanunua wananchi ataona haya kuwakemea wenzake wanaopatikana na hatia ya rushwa.

Mgombea mwingine aliyefika mkoani hapa ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli (CCM) aliyepokelewa na wanachama na mashabiki wengi na kujizolea wadhamini 680 waliotia saini kwenye fomu yake na hatimaye kuelekea mikoa ya Njombe na Mbeya.


Aliwaomba wananchi wa Iringa wampe ridhaa ya kuteuliwa na chama chake ili aweze kupeperusha bendera ya Jumhuri ya Muungano wa Tanzania. 
CHANZO: NIPASHE

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...