Skip to main content

POLISI MKOANI IRINGA WAKAMATA MAGUNIA MATATU YA BANGI



Polisi mkoani Iringa wamefanya msako kali kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na uaslama na kufanyikwa kukamata magunia matatu ya bangi, CD za mafunzo ya jihadi za kialshaababu pamoja na nguzo 35 za umeme mali ya shirika la umeme Tanesco.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, ACP Ramadhani Mungi alisema polisi walifanya opresheni kusaka mambo yanayohusu makosa ya jinai na kufanyikwa kukamata maguni ya bangi pamoja na kukamatwa watuhumiwa sugu katika eneo ya njiapanda ya Tosamaganga.

Alisema magunia hayo ya bangi yakiwa yamefungashwa katika mifuko mdogo na misokoto yalikamatwa pamoja na watuhumiwa sugu wawili.

“Watu hawa wamekamatwa wakati wa kiendelea kufunga bangi hizo katika vifungashio mbalimbali pamoja na misokoto,” alielezea kamanda.

Kamanda huyo aliwataja watuhumiwa kuwa ni Steven Sanga na Nicolaus Tweve, ambao alisema ni maarufu sana kwa kuingiza na kusambaza bangi mkoani hapa.

Alisema kuwa Tweve ni maarufu sana kwa kuingiza na kusambaza madawa ya kulevya mkoani hapa na hivi juzi juzi ametoka magereza kwa kosa hilo hilo la kujihusisha na usambaji na uigizaji wa bangi.

“Watu kama hawa wanatuharibia vijana wetu, wanatuharibia pia nguvu kazi,” alisisitiza kamanda.

Kama vile haitoshi, Jeshi la Polisi lilifanyikiwa kukamata nguzo za umeme 35, nyaya za umeme na vifaa vingine vya kufungia umeme katika maeneo mbalimbali vinazodaiwa kuwa mali ya shirika la umeme nchini Tanesco.

Alisema kuwa vifaa hivyo vimekatwa kwa watu binafsi wawili, lakini kutokana na upelelezi kuendelea kamanda huyo hakutaka kuwataji watuhumiwa hao.

Aliongeza kuwa nguzo hizo zilitakiwa kuwepo maeneo ya vijijini ambapo kuna zoezi la kusambaza umeme vijijini, lakini zimekutwa kwa watu binfasi kinyume na sheria.

“Huku ni kurudisha nyuma jitihada za serikali za kusambaza umeme katika mkoa wetu hasa maeneo ya vijijini,” alisema kamanda.

Wakati huouhuo, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na mbalimbali limewakata watoto wanne wakiwa na CD zinazoonesha mafunzo ya ukatili, kuchinja na kuua ya kialshaababu.

Alisema kuwa watoto hao wanakadriwa kuwa na umri kuanzia 12 hadi 16 na wanaonesha CD hizo katika maeneo mbalimbali.

Alisema CD hizo zimekatwa kutoka kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu na polisi inaendelea na uchunguzi kujua watoto hao wamezipata wapi na ni kwa lengo gani na kutakujua baada ya mafunzo hayo watayafania kazi gani.

“CD hizo tumeziangali zinaonesha mafunzo ya kialshaababu yakiwemo kuua, kuchinja pamoja na mambo mengine. CD hizi tumebaini zinaonesha kwa kutumia kompyuta ambayo imefungwa kwa pasiwedi (password). Kama jeshi la polisi hatutaishia hapo tutaendelea na uchunguzi watoto hao CD hizo wanazipata wapi na kwa madhumini gani,” alisema.

Alisema kuwa kumekuwepo na tabia ya watu kujihusisha na mambo ya kiuharifu kama vile kusamabza madawa ya kulevya pamoja na uharibifu wa miundo mbinu ya umeme.

Hata hivyo, kamanda huyo ametoa wito kwa umma kushirikiana na jeshi la polisi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kutoa taarifa pindi wanapoona kuna watu au vitu ambavyo si vya kawaida.

“CD hizi nyingi, bangi ni nyingi lakini vile vile uharibifu wa miuondombinu wa umeme ni mkubwa,” alimalizia kamanda.

Mwisho









Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...