Skip to main content

UJUMBE WA IRINA BOKOVA, MKURUGENZI MKUU WA UNESCO SIKU YA BAHARI DUNIANI



Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Bi Irina Bokova.

DUNIA endelevu haiwezi kuwapo kama hakutakuwepo na bahari yenye kuendeleza uhai.

Miezi michache kabla ya kufanyika kwa kongamano la kihistoria la COP21 (21st Conference of the Parties to the United Nations Framework Convention on Climate Change) la kutengeneza ajenda mpya ya maendeleo endelevu, ujumbe huu ulikuwa hauna tija.

Lakini sasa ujumbe huu una tija sana na muhimu sana.

Iwe nchi iko mbali na bahari au karibu, kila nchi na kila aina ya uhai hutegemea zaidi namna bahari inavyokuwa salama na yenye kutekeleza wajibu wake wa kulea uhai.

Kiukweli bahari ni kitu muhimu katika mfumo wa hali ya hewa duniani, ikiratibu kwa namna ya kipekee mabadiliko ya muda mrefu ya hali ya hewa na mfupi na pia uwepo wa hewa mbalimbali katika anga ikiwemo oksijeni tunayovuta.

Aidha inawezesha kuwapo kwa lishe na kuwa chanzo cha chakula.

Wakati wanasayansi wanaweka teknolojia mpya kuweza kuangalia tabia za bahari , tunatambua kwamba zipo athari za shughuli za kibinadamu katika afya ya bahari hasa hewa ya ukaa inayozalishwa kwa sababu za shughuli za kiviwanda.

Alisema hewa hiyo ya ukaa imevuruga mfumo wa ikolojia wa baharini na kuweka kazi ya uratibu ya bahari katika hatari.

Kupanda kwa kina cha bahari, kuyeyuka kwa mabonge ya mabarafu, kuzidi kwa kiwango cha tindikali, kuwepo na maeneo yaliyokufa, kuzaliwa kwa mimea bahari hatari, kufumuliwa kwa matumbawe,kupungua kwa samaki na mfumo wa ikolojia… kunaonesha uwapo wa matatizo katika kiwango cha kitaifa na kimataifa.

Ili kuangalia athari za shughuli za kibinadamu Unesco inaangalia elimu, utamaduni, sayansi na mawasiliano katika kubadilisha elimu na teknolojia kwa jamii katika maendeeo endelevu na mabadiliko ya tabia nchi.

Kupitia kamisheni ya bahari dunia, Unesco inaangalia mfumo wa aina yake wa bahari kwa ajili ya utafiti wa hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi.

Pia inawawezesha wataalamu mbalimbali kuchambua matokeo ya tafiti za sasa na hasa kuzidi kwa joto katika bahari na tindikali kwa kutambua thamani bahari katika mabadiliko ya tabia nchi.

Katika Siku ya Bahari , UNESCO kwa kusaidiwa na Monaco, Sweden na Ufaransa, inawezesha tukio kubwa katika makao yake makuu mjini Paris, Ufaransa kuangalia umuhimu wa bahari kabla ya mkutano wa majadiliano wa mabadiliko ya tabia nchi.

Mabadiliko ya tabia na hali ya hewa yana mahusiano makubwa na mabadiliko baharini na hakuna nchi yoyote duniani hata iwe na nguvu kiasi gani cha uchumi inaweza kukabili mabadiliko yanayotokea baharini.

Katika siku hii ya kuadhimisha Siku ya Bahari, ninatoa wito kwa nchi zote wanachama,taasisi zisizo za kiserikali na sekta binafsi kushirikiana katika kuhakikisha kwamba dunia inachukua hatua kuona umuhimu wa bahari katika mfumo wa wa hali ya hewa duniani.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...