Skip to main content

UN YAISIFU TANZANIA KUWA MSTARI WA MBELE KUTETEA ALBINO



Baadhi ya watu wenye ulemavu wakipita na mabango yenye ujumbe katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kwa maandamano kwenye maadhimisho ya Siku yao ambayo inalenga kutoa elimu ya kupinga matendo maovu wanayofanyiwa na watu wenye nia mbaya.(Picha na modewjiblog)

Na Mwandishi wetu, Arusha

MRATIBU Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi wa Shirika la Mpango wa maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodgriguez amepongeza Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele kushawishi dunia siku ya kukumbuka watu wenye ulemavu wa ngozi duniani.

Alisema dhana ya Juni 13 ilianzia Tanzania kwa mshikamano kati ya serikali ya Tanzania na mashirika yasiyo ya kiserikali kama Shirika la Under the same sun (TAS).

Alisema kutokana na bidii walizoonesha Novemba 18,2014, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha siku hiyo kuadhimishwa duniani kote kila ifikapo Juni 13

Akihutubia kabla ya rais Jakaya Kikwete ambaye alikuwa mgeni rasmi kuzungumza, Rodgriguez alisema dunia inapaswa kuangalia kwa makini maisha ya walemavu wa ngozi na kuzuia ukatili dhidi yao.

Alisema pamoja na haja ya kuongeza ufahamu wa watu juu ya masuala ya ualibino na maalbino ni vyema jumuiya ya kimataifa kuhakikisha kwamba kila mwanamke, mwanamume na mtoto wanatendewa kwa usawa na kwa heshima.

Alisema kutokana na haja hiyo Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanyakazi na serikali ya Tanzania kuboresha maisha ya watu wake kwa kusaidia kuimarisha mfumo wa mahakama, masuala ya wakimbizi na masuala ya utoaji haki.

Alisisitiza kuwa kuwapo kwa haki, usawa na utu kutahakikisha kuwapo kwa amani na usalama kwa jamii zenye ulemavu wa ngozi.

Alisema kwa sasa kuna woga mkubwa kwa jamii ya ulemavu wa ngozi kutokana na chuki, unyanyapaa, mashambulizi ya kutisha, mauaji na kugeuzwa kuwa bidhaa huku wakiuuawa kwa sababu za matambiko ya kutafuta utajiri.

Mratibu huyo alisema kwamba taifa na jamii ya binadamu wote wanatakiwa kushirikiana katika kuzuia ukatili kwa wenye ulemavu na pia kuwasaidia kukabilina na mazingira yao magumu hasa upatikanaji wa vifaa vya kuwakinga na madhara ya jua.

Alitaka pia jamii kuelimishwa kuhusu mtiririko wa vinasaba vinavyosababisha ulemavu wa ngozi na kupambana na ubaguzi na tishio la maisha kwa kutoa mafunzo mbalimbali.

Aidha alisema Umoja wa Mataifa utaendelea kufanya kazi na wanachama wa taasisi mbalimbali zisizo za kiserikali na Serikali kuimarisha haki za binadamu .


Baadhi ya watu wenye ulemavu wakipita na mabango yenye ujumbe katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kwa maandamano kwenye maadhimisho ya Siku yao ambayo inalenga kutoa elimu ya kupinga matendo maovu wanayofanyiwa na watu wenye nia mbaya.


Baadhi ya watu wenye ulemavu wakipita na mabango yenye ujumbe katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Arusha kwa maandamano kwenye maadhimisho ya Siku yao ambayo inalenga kutoa elimu ya kupinga matendo maovu wanayofanyiwa na watu wenye nia mbaya.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete akihutubia wananchi waliohudhiria maadhimisho hayo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa(UN) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hapa nchini, Alvaro Rodriguez akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.


Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa(UN) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hapa nchini, Alvaro Rodriguez akipongezwa na Rais Jakaya Kikwete baada ya kutoa hotuba yake katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.


Balozi wa Canada hapa nchini, Alexandre Leveque akihutubia katika Maadhimisho ya Siku ya wenye Ualbino yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.


Mwenyekiti wa wenye ulemavu wa ngozi nchini(TAS), Ernest Kimaya akitoa nasaha zake.


Naibu Waziri wa Afya, Dk.Kebwe Steven Kebwe akitoa nasaha zake.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk Jakaya Kikwete akiwapongeza watoto wenye Ualbino wanaofadhiliwa na USAID chini ya mpango wa Tuwalee.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete akiagana na Balozi wa Canada hapa nchini, Alexandre Leveque baada ya maadhimisho hayo, kulia ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa(UN) na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) hapa nchini, Alvaro Rodriguez na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...