Skip to main content

BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA IRINGA LAVUNJWA RASMI...!

Meya wa Manispaa ya Iringa Mstahiki Amani Mwamwindi akufafanua jambo wakati wa kikao cha mwisho cha baraza hilo jana. Kulia kwake walioketi ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, Mkuu wa Wilaya ya Iringa Andelina Mabula akifuatia na Naibu Meya Gervas Ndaki.

Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kupitia Idara ya Fedha na Biashara imekusanya jumla ya 5,357,849,597/- kati ya hizo 1,010,046,997/- in mapato ya ndani katika kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Julai 2014/2015.

Akisoma taarifa ya kazi zilizotekelezwa na kamati ya fedha na uongozi kwa baraza la madiwani lililovunjwa jana, Naibu Meya Gerevas Ndaki kwa niaba ya mwenyekiti wa kamati hiyo, alisema kuwa 4,347,802,600/- ni ruzuku toka serikali kuu kwa ajili ya mishahara, matumizi mengineyo na miradi ya maendeleo.

Alisema kuwa kamati ya fedha na uongozi hiyo iliongozwa na mwenyekiti wake Amani Mwamwindi ambaye pia kulikuwa ni Meya wa Manispaa ya Iringa katika kipindi cha robo ya nne.

Alisema kuwa lengo la mwaka la kukusanya mapato ya ndani ya halmashauri ili kuwa ni kukusanya jumla ya 3,344,443,084/- kati ya 3,873,388,024/= sawa na asilimia 86.

Kwa upande wa ruzuku toka serikali kuu halmashauri ilipokea jumla ya shilingi 24,290,898,004.70 kati ya lengo la shilingi 26,607,093,100/- sawa na asilimia 91.

Aidha, alisema kuwa katika kipindi cha robo ya nne halmashauri ilitumia pia jumla shilingi 5,487,339,738.70 kati ya hizo Tshs. 4,825,568,215/- ni mishahara ya watumishi na Tshs. 661,771,523.70 ni matumizi mwengineyo na miradi ya maendeleo.

“Kwa lengo la mwaka 2014/2015 halmashauri imetumia jumla ya Tshs. 25,005,282,271.80 kati ya shilingi 31,258,652,999.93 sawa na asilimia 80. Kati ya matumizi hayo zaidi ya shilingi bilioni 19 ni matumizi ya mishahara, Tshs. 1,337,837,004.3 ni matumizi menegineyo na Tshs. 4,334,302,931.5 ni miradi ya maendeleo,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Kwa upande wa uwekezaji, kamati hiyo ilishughulikia masuala ya uwekezaji kwa kufanya uthamini wa eneo la mradi wa upimaji viwanja Igumbilo kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo na Uwekezaji (TIB).

Alisema jumla ya wananchi 232 walithaminiwa ardhi yao ambapo fidia ya mali ni Tshs. 1,579,681,809/-.

Mwisho









Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...