Skip to main content

BRIGHTERMONDAY TANZANIA YATOA FURSA KWA WANAOTAFUTA AJIRA KUWATEMBELEA KWENYE MAONYESHO YA SABASABA



Meneja Masoko wa kampuni ya Brightermonday Tanzania, Lugendo Khalfan ndani ya hema la banda la Jakaya Kikwete akiwa tayari kukuhudumia wewe mtanzania utakayetembelea banda lao katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’, yanayoendelea kurindima kwenye viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.( Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Na Modewjiblog team

Watafuta ajira kote nchini Tanzania wamehamasishwa kujisajili na tovuti ya Brighter monday ili wapate fursa ya kuunganishwa na watoa ajira.

Akifanya mahojiano na mtandao wa habari wa modewjiblog.com, Meneja Masoko wa Brighter monday Tanzania Khalfan Lugendo, amesema usajili huo mbao ni bure, utamwezesha mhusika kupata taarifa mbalimbali na kuweza kuomba nafasi tofauti za kazi ambazo zimewekwa katika tovuti hiyo.

Amesema Brightermonday inajivunia kuwa ndio tovuti namba moja ya ajira nchini Tanzania kwa kuwa idadi ya kazi wanazoziweka katika mtandao huo ni nyingi kuliko chanzo chochote kile cha ajira nchini Tanzania.

Bw. Lugendo ameongeza kuwa kwa mwaka jana 2014 waliweza kuweka nafa za ajira 30,000 na hivyo kuwarahisishia waajiri mchakato mzima wa kuajiri na kupata watu wenye viwango bora zaidi.

Aidha ametoa wito kwa watu wote wanaotembelea maonyesho ya mwaka huu ya kimataifa ya biashara Sabasaba, kutembelea banda lao lililopo katika hema la Jakaya Kikwete ambapo watapata maelekezo kuhusu namna ya kuweza kupata ajira kwa urahisi.

Ametaja namna ya kuwapata ni kupitia anuani ya tovuti ambayo ni www.brightermonday.co.tz au e-mail : info@brightermonday.co.tz,

Simu: +255688 333 334,

Katika mitandao ya kijamii wanapatikana kwa anuani zifuatazo


facebook: brightermondaytz,

Instagram: brightermondaytz pia katika Googleplus na Twitter.


Key Account Manager wa Brightermonday Tanzania, Gloria Nyiti kwenye sehemu maalum ya kupokea wageni katika banda lao lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.



Wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakitoa huduma kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao lilipo ndani ya hema la Jakaya Kikwete kwenye maonyesho sabasaba.


Gloria Nyiti akiwahudumia watafuta ajira katika banda la Brightermonday lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.


Gloria Nyiti akitoa maelekezo ya namna ya kujisajili kwenye mtandao wa Brightermonday kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao kwenye maonyesho ya sabasaba yanayoendelea kupamba moto jijini Dar.


Timu ya wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakiwa nadhifu katika banda lao tayari kuwahudumia wateja kwenye maonyesho ya Sabasaba.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...