Skip to main content

CCM WILAYA YA IRINGA MJINI YAANZA KUWATAMBULISHA WAGOMBEA UBUNGE KWA WANACHAMA


Katibu wa Wilaya ya Iringa mjini, Elisha Mwampashi (kulia) akiongea na waandishi wa habari jioni leo na kushoto ni Mwenyekiti wa Wilaya ya Iringa mjini Abeid Kiponza.



Zoezi la awali la utoaji na urejeshaji wa fomu kwa wagombea nafasi za ubunge na madiwani kupitia Chama cha Mapidunzi (CCM) nchi nzima umekamilika jana.

Katika Jimbo la Iringa mjini, mkoani Iringa chama hicho kimeandaa mikutano kwa wagombea ubunge wote ya kuwatambulisha kwa wanachama ikiwa sehemu ya pili ya mchakato ya kumpata mgombea pekee atakaye peperusha bendera ya chama hicho kwa kushindana na vyama vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari jana usiku, Katibu wa Wilaya ya Iringa mjini, Elisha Mwampashi alisema awamu ya kwanza ya kutoa na kurudisha fomu za ubunge limealianza tarehe 15.07.2015 na kumalizika hadi 19.07.2015.

Aliongeza kuwa awamu ya pili ya mchakato itaanza tarehe 20.07.2015 hadi 31.07.2015 lengo ni kuwatambulisha watia nia kwa wanachama katika matawi ambapo utaratibu ni kwamba watapanda gari moja wagombea wote 13 na kila mmoja atapewa nafasi ya kujieleza wakati wa mikutano katika kata zote 18 za Jimbo la Iringa mjini.

Alisema kuwa jumla ya wagombea ubunge 13 Iringa mjini waliochua na kurudisha fomu na wataanza safari hiyo ya kuwatambulisha kwa wanachama katika matawi 81 ya CCM.

Wana CCM hao wanaoomba nafasi ya ubunge ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu, Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Frederick Mwakalebala na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mahamudu Madenge.

Katika orodha hiyo yupo pia Dk Yahaya Msigwa, Nuru Hepautwa, Addo November Mwasongwe, Adestino Mwilinge, Frank Kibiki, Aidani Kiponda, Peter Mwanilwa, Fales Kibasa, Michael Mlowe na Balozi mstaafu Dk. Augustine Mahiga.

Kwa mwaka wa tano sasa, jimbo hilo linaongozwa na Mch. Peter Msigwa (Chadema) aliyeshinda kwa tofauti ya kura 828 katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 baada ya kujipatia kura 17,744 dhidi ya kura 16,916 alizopata mgombea wa CCM, Monica Mbega.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...