Skip to main content

CHADEMA YAGARAGAZWA NA CCM KESI ZA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA...!



Mahakama ya Wilaya ya Iringa imetoa hukumu ya kutengua matokeo ya mitaa 13 kutoka Manispaa ya Iringa ili kufanya uchaguzi wa marudio wa Serikali za Mitaa kutokana na kasoro kadhaa zilizojitokeza katika uchaguzi uliofanyika Desemba 14 mwaka 2014.

Hukumu hiyo ilitolewa jana mbele ya mahakamu wakazi wanne ambao ni Andrew Scout, John Mpitanjia, E. Nassoro na Isaya, waliokuwa wanaendesha kesi hizo katika Mahakama ya Wazi ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Iringa.

Chama cha Mapindizi (CCM) kulifungua kesi 35 za madai za uchaguzi wa serikali za mitaa tarehe 13.01.2015 na kuwakilishwa na wakili msomi, Gaster Likatage Mdegela dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na chama wananchi CUF, ambapo kesi 34 zilikuwa za Chadema na kesi moja tu ndio ilikuwa ya CUF.

Aidha, katika kesi hizo mlalamikiwa namba moja alikuwa ni Chadema walioshinda uchaguzi wa serikali za mitaa na mlalamikiwa wa pili alikuwa ni msimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Katika upande utetezi mawakili nane walisimamia kesi hizo ambao ni Barnabas Nyulusi, Mariam Mbano, Leah Francis, Queen Mtove, Catherine Chalwa, Charles Lawisso, Collins Malekela na Jane Massey.

Moja ya kasoro hizo zilizolalamikwa ni kuchanganywa kwa majina ya wagombea wa uenyekiti. 

Hata hivyo, mitaa iliyotenguliwa matokeo yake ya uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Desemba 14, 2014 kutokana kasoro mbalimbali ni pamoja na SabaSaba Kata ya Gangilonga, Darajani na Kondoa Kata ya Mivinjeni, Ndiuka ‘D’ Kata ya Igumbulo, Kaduma Kata ya Mkimbizi na Semtema ‘A’ Kata ya Kihesa, 

Mitaa mingine ni Nyamhanga ‘B’ Kata ya Kitwiru, Muungano ‘A’na ‘B’ Kata ya Kwakilosa, Kajificheni Kata ya Ilala, Kihodombi ‘B’ Kata Isakalilo, Dodoma Road na Mkimbizi ‘B’ Kata ya Mkimbizi.

Aidha, mahakimu wakazi hao watengua matokeo ya mitaa 13 ili uchaguzi kurudiwa ndani ya siku 30 bila kulipa gharama zozote za uendeshaji wa kesi kwa pande zote mbili za mlalamikaji na mlalamikiwa na rufaa iko wazi.

Awali, Chadema walipeleka mapingazi ya awali 35 mahakamani ili kesi zifutwe kwa gharama lakini kesi nane madai zilitupiwa mbali kwa gharama katika hukumu ndogo (ruling).

Mahakama hiyo ilitupilia mbali kesi nane hizo kwa kukosa ushahidi kwa upande wa mlalalmikaji (CCM).

Kwa mantiki hiyo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimegaragazwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kesi ya msingi ya madai ambapo mahakama ilitenguliwa matokeo ya uchaguzi wa serikali za mitaa ili uchaguzi urudiwe katika nafasi ya wenyeviti.

Katika hukumu hiyo ambayo ilitolewa na Mahakama ya Wilaya ya Iringa Juni 30, mwaka huu imekubaliana na hoja za walalamikaji ambao ni wagombea wa CCM washinda mitaa 13 na Chadema wao walishinda mitaa sita katika ya jumla kesi 19 zilizosikilizwa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...