Skip to main content

Hepautwa:nafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuichagua Chadema uchaguzi wa mwaka 2010


Nuru Hepautwa



Na Friday Simbaya, Iringa

KADA maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wa mjini Iringa, Nuru Hepautwa amesema anafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuachia jimbo hilo mikononi mwa Chadema katika uchaguzi wa mwaka 2010 lakini akaahidi kuyamaliza endapo atapewa ridhaa hiyo.

Hepautwa ambaye pia ni mfadhili wa mashindano ya soka yaliyojizolea umaarufu mjini Iringa ya Hepautwa Cup alitoa mchango huo jana wakati akijinadi kwa wanachama katika Kata ya Kitwiru Jimbo la Iringa mjini.

MFANYABIASHARA huyo alitangaza nia ya kuwania ubunge wa jimbo la Iringa Mjini hivi karibuni katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu kwa kupitia tiketi ya chama chake, Chama cha Mapinduzi (CCM).

Hepautwa ambaye pia ni Naibu Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Iringa Mjini alisema anafahamu maumivu yaliyotokea kwa wana CCM baada ya kuachia jimbo hilo mikononi mwa Chadema katika uchaguzi lakini akaahidi kuyamaliza endapo atapewa ridhaa hiyo.

Kwa mwaka wa tano sasa, jimbo la Iringa Mjini limeendelea kuongozwa na Mchungaji Peter Msigwa aliyechaguliwa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika Uchaguzi Mkuu wa 2010.

Akizungumzia vipaumbele vyake endapo atapewa ridhaa hiyo, Hepautwa alivitaja kuwa ni pamoja na kubuni vyanzo vipya vya ajira kwa vijana na kuboresha huduma katika sekta mbalimbali zikiwemo za afya, maji, elimu, miundombinu ya barabara na biashara.

Kwa upande wa sekta ya biashara alisema mpango wake ni kuwashawishi wafanyabiashara wenye uwezo mkubwa kujenga viwanda vya mazao ya kilimo, kutenga maeneo ya wafanyabiashara wadogo na kuufanya mji wa Iringa kuwa mji wa kibiashara.

“Nataka kuona Iringa unakuwa mji wa biashara za aina zote, magari, vipuri, mitambo, nguo, vyakula na nyinginezo ili waliojirani na CCM wasiende tena Dar es Salaam ili sehemu ya kununua mali wanazohitaji kwa jumla iwe Iringa,” alisema.

Alitaja biashara nyingine zinazoweza kufanywa na wakazi wa Iringa Mjini kuwa ni pamoja na ya kuongoza na kusafirisha watalii ili kuiongezea msukumo wa kutosha.

“Kule kaskazini, vijana wengi kama sisi wamenufaika na mapato yatokanayo na utalii kwasababu wamethubutu kuwekeza katika sekta hiyo. Nataka kuona na sisi wa Iringa tunatumia ujirani wetu na hifadhi ya Taifa ya Ruaha kuchangamkia fursa hiyo,” alisema.

Katika afya alizungumzia namna atakavyosaidia kuboresha huduma hasa za mama na mtoto, mapambano ya virusi vya Ukimwi na upatikanaji wa vifaa tiba na dawa katika vituo vyote vya kutolea huduma.

Katika Jimbo la Iringa mjini, mkoani Iringa chama hicho kimeandaa mikutano kwa wagombea ubunge wote ya kuwatambulisha kwa wanachama ikiwa sehemu ya pili ya mchakato ya kumpata mgombea pekee atakaye peperusha bendera ya chama hicho kwa kushindana na vyama vya upinzani katika Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka huu.

Jumla ya wagombea ubunge 13 Iringa mjini waliochua na kurudisha fomu na wameanza safari ya kuwatambulisha kwa wanachama katika matawi 81 ya CCM Jimbo la Iringa Mjini.

Wana CCM hao wanaoomba nafasi ya ubunge ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu, Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Frederick Mwakalebala na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mahamudu Madenge.

Katika orodha hiyo yupo pia Dk Yahaya Msigwa, Nuru Hepautwa, Addo November Mwasongwe, Adestino Mwilinge, Frank Kibiki, Aidani Kiponda, Peter Mwanilwa, Fales Kibasa, Michael Mlowe na Balozi mstaafu Dk. Augustine Mahiga.



Addo November Mwasongwe,

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa Jesca Msambatavangu

Fales Kibasa

Frank Kibiki

Balozi mstaafu Dk. Augustine Mahiga

Michael Mlowe

Dk Yahaya Msigwa

Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe Frederick Mwakalebala

Peter Mwanilwa

Aidani Kiponda (Weekend)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...