Skip to main content

IPC WAPATA VIONGOZI WAPYA KWA MIAKA MITATU IJAYO


Msimamizi wa uchaguzi  Hakimu Mwafongo (kushoto) akitangaza matokeo katika mkutano mkuu wa tatu wa mwaka uliyofanyika Ukumbi wa Lutheran Center mjini Iringa. Kulia ni msimamizi msaidizi wa uchaguzi, Sofia Mpunga.

Mgombea Tukuswiga Mwaisumbe katika nafasi ya katibu akiomba kura

Mtia nia Conrad Mpila katika nafasi ya makamu mwenyekiti akiomba kura.

Mtia nia Frederick Siwale katika nafasi ya makamu mwenyekiti akiomba kura.




Mtia nia Jackson Manga katika nafasi ya makamu mwenyekiti akiomba kura.


Mtia nia Francis Godwin katika nafasi ya katibu na makamu mwenyekiti akiomba kura.



Na Friday Simbaya, Iringa

KLABU ya Waandishi wa Habari mkoani Iringa (IPC) imepata viongozi wapya watakaokuwa madarakani kwa miaka mitatu ijayo katika uchaguzi wa mkutano mkuu wa mwaka uliofanyika jana mjini Iringa.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi hayo msimamizi wa uchuguzi, Hakimu Mwafongo, akisaidiana na msaidizi wake, Sofia Mpunga alimtangaza Frank Leonard kuwa mwenyekiti mpya wa chama hicho kwa mara ya pili tangu aliyekuwa mwenyekiti, Daudi Mwangosi kuuawa Septemba 2, 2012 baada ya kupigwa bomu kwenye mkutano wa Chadema huko Nyololo, wilayani Mufindi mkoani Iringa.

Alisema chama hicho kilifanya uchaguzi katika nafasi za makamu mwenyekiti na katibu mtendaji wakati nafasi za ujumbe na mwenyekiti walipita bila kupingwa.

Mchuano mkubwa ulikuwa katika nafasi ya makamu mwenyekiti ambapo wagombea walijitokeza wanne akiwemo Conrad Mpila, Frederick Siwale, Jackson Manga na Francis Godwin.

Hata hivyo, Fredrick Siwale aliibuka mshindi katika nafasi ya makamu mwenyekiti baada ya kuwashinda wagombea wengine watatu walioomba nafasi hiyo kwa kupata kura 16.

waliogombea wengine katika nafasi hiyo na matokeo yao katika mabano ni Conrad Mpira (1), Jackson Manga (1) na Francis Godwin (5), ambapo jumla ya wajumbe waliopiga kura ni 23.

Katika nafasi ya katibu, Tukuswiga Mwaisumbe alichaguliwa kuwa katibu mtendaji kwa kupata kura 14 baada ya kumshinda mpinzani wake Francis Godwin aliyekuwa akitetea nafasi yake kwa kupata kura (10).

Katika uchaguzi huo pia wajumbe saba waliochaguliwa ambao ni Selina Ilunga, Gertrude Madembwe, Happy Matanji, Jackson Manga, Francis Godwin, Shaban Lupimo na Frola Kamage.

Viongozi wengine waliochaguliwa bila kupingwa ni pamoja na Janeth Matondo mweka hazina na Selemani Boki mweka hazina msaidizi.

Klabu hiyo ya waandishi wa habari ina jumla ya wanachama 41, kati yao ni wanachama 31 waliohai ambao wamelipa ada na ndio walioalikwa katika mkutano mkuu huo.

Chama hicho katika kipindi cha mwaka 2013 hadi 2015 kilikusanya michango na misaada ya zaidi ya shilingi milioni 10.



Fedha hizo ni makusanyo ya akiba yanayotokana na fedha kutoka umoja wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania (UTPC), ada za wanachama na wadau wengine.





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...