Skip to main content

Katibu wa CCM Mufindi:Vijana tuepuke kutumika katika kuvuruga amani na utulivu iliopo nchini




 
Katibu wa CCM Wilaya ya Mufindi Jimson Mhagama

MUFINDI: KATIBU wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mufindi Gimson Mhagama ametoa rai kwa vijana kuepuka kutumika katika kuvuruga amani na utulivu uliopo nchini Tanzania kwa kutumika na baadhi ya vyama vya siasa na kuhatarisha amani ya Taifa. 

Alisema kuwa amani ambayo tunajivunia ipo siku itatoweka na iwapo vyama vya siasa vitaacha kufanya kazi yake ya kisiasa kwa kunadi sera za vyama vyao na kueneza chuki dhidi ya serikali kama ilivyo hivi sasa kwa baadhi ya vyama kuendesha siasa za chuki na kuwatumia vijana kuvuruga amani yetu.

Katibu hiyo ambayo alikuwa katibu msaidizi wa CCM Mkoa wa Iringa na kuteuliwa kushiki nafasi ya ukatibu Wilaya ya Mufindi alitoa rai hiyo wakati akikongea na vijana wa stendi ya mafinga pamoja na madereva taxi na bodaboda jana ikiwa ni kazi yake ya kwanza tangu kuteuliwa. 

Alisema kuwa Tanzania ni nchi pekee yenye ustawi wa amani barani Afrika na kutoa mfano kwa nchi jirani zinazoonesha madhara ya kuichezea amani na kuongeza kuwa ni rahisi sana kupoteza amani na umoja lakini ni vigumu sana kuirejesha.

“Nawaomba vijana wenzangu kuacha kuandamana kwa kuiga tu kwa kuwa umeambiwa fanya jambo hilo, mbali mwe vijana bora katika kudumisha amani iliyopo na kamwe msije iga siasa vya vyama vya upinzani siasa ya kufanya vurugu,” alisema katibu.

Alisema kuwa moja ya changamoto kubwa inayowakabili vijana na ambayo kwa kushirikiana nao atahakikisha inafanyiwa kazi ni kwa kutumia fursa mbalimbali zinazowazunguka katika sekta ya biashara, kilimo kwa kupitia vikundi vya maendeleo. 

Alisema Tanzania ina jumla ya vyama vya siasa 22 na lengo ya kila chama ni kushika dola na kuongeza kuwa vyama vya upinzani bado sana kushika dola na itachukuwa miaka 75 ijao.

Alisema kuwa vyama vya upinzani havina demokrasia ndani ya vyama vyao kwa sababu wenyeviti wa vyama hivyo ni wale wale tofauti na CCM ambapo tumeshuhudia upana wa demokrasia kwa watia nia kuvitokeza kwa wingi zaidi ya 35.

Pia aliwaomba vijana wajitokeze kupiga kura katika uchaguzi mkuu hapo tarehe 25.10.2015 na wasisahau kuipigia kura CCM kwa sababu ni chama pekee chenye uwezo wa kudumisha amani, upendo na mshakamano. 

Wakati huohuo, Katibu CCM Wilaya Mufindi ametoa vifaa vya michezo kwa vijana stendi kama vile jezi na mipira kwa ajili ya kuwasaidia kuimarisha afya zao kupitia michezo.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...