Skip to main content

MAKUSANYO YA MAPATO WILAYA YA MUFINDI YAONGEZEKA

Na Friday Simbaya, Mufindi

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mufindi, Saada Malunde amesema makusanyo ya mapato yameongezeka kutoka zaidi ya shilingi bilioni 2,192,830,130/- mwaka 2010/2011 na kufikia zaidi ya shilingi bilioni 4,146,583,199/- mwaka 2014/2015.

Mkurugenzi Mtendaji huyo alitoa taarifa hiyo hivi karibuni baada ya kuvunjwa rasmi Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi lililodumu kwa muda wa miaka mitano na kuoanisha mafanikio kadhaa yaliyofikiwa tangu kuundwa kwake mnamo mwaka 2010.

Akisoma taarifa ya mafanikio ya halmashauri hiyo, kwenye kikao maaluum cha kuvunjwa kwa baraza, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mufindi, Saada Malunde alitaja baadhi ya mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Halmashauri ya Mji wa Mafinga, kuongezeka kwa makusanyo ya mapato kutoka zaidi ya shilingi bilioni 2,192, 830,130/- mwaka 2010/2011 na kufikia zaidi ya shilingi bilioni 4,146,583,199/- mwaka 2014/2015.

Malunde alisema kuwa lengo la halmashauri ya wilaya katika shule za sekondari ni kuhakikisha wanafunzi wote wanaojiunga na kidato cha kwanza wanahitimu na kufaulu kidato cha nne.

“Tumepata mafanikio katika mwaka wa 2014/2015 kwani idadi ya shule za sekondari imeongezeka toka shule 18 hadi kufikia shule 57 mwaka 2015, idadi ya wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza imeongezeka kutoka wanafunzi 2,880 mwaka 2010 hadi kufikia 4,926 mwaka 2015. Pia idadi ya walimu wa shule za sekondari imeongezeka kutoka walimu 81 mwaka 2010 hadi kufikia walimu 887 wakiwemo wanaume 586 na wanawake 301 mwaka 2015, ” alisema Malunde.

Alisema kuwa halmashauri ya wilaya imeunganishwa na grid ya Taifa na kuwa na uhakika wa umeme unaotokana na nguvu ya maji na mwaka wa fedha 2014/2015. 

Na kuongeza kuwa vijiji 13 na kitongoji kimoja kimepata huduma ya umeme unaozalishwa na kampuni ya Mwenga “Hydro Power” katika Kata ya Ihanu. 

Aidha, mradi huo una mpango wa kuongeza huduma ya umeme katika vijiji 18 vya Tarafa ya Kibengu.

“Tunao mradi unaosimamiwa na wakala wa umeme vijijini (REA) ameanza kusambaza na kusimika nguzo kuanzia hapa Mafinga hadi kata ya Sadani, Isalavanu na Igombavanu na kuanzia Makambako hadi Malangali, Ihowanza kupitia Kata ya Mbaramaziwa kwa hiyo vijiji vitakavyopata umeme vitaongezeka kwenye Tarafa ya Sadani na Malangali mara mradi utapokamilika,” Malunde aliongeza.

Mkurugenzi huyo mtendaji aliyataja mafanikio mengine kuwa ni uwepo wa mtandao mzuri wa barabara unaofikia kilometa 1,558.3 sanjari na kufanikiwa kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami kwa umbali wa kilometa kumi (10) katika Mji wa Mafinga na kuboresha upatikanaji wa maji. 

Alisema kuwa hivi sasa idadi ya watu wanaopata maji safi na salama imeongezeka kutoka asilimia 40 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 64 mwaka 2014/2015 kwa wa kazi wa mjini, wakati vijijini ongezeko imepanda kutoka asilimia 56 hadi kufikia asilimia 62.3.

Awali akitoa salamu za Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa (RAS), Wamoja Ayubu, amewataka watumishi chini ya mkurugenzi wa halmshauri hiyo, kuzingatia maelekezo ya TAMISEMI wakati wa kufanya maamuzi hususan yanayohusiana na fedha kwa kipindi chote ambacho halmashauri itakuwa chini ya uongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo.

Mwisho





Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...