Skip to main content

Mbunge Lembeli aondoka CCM



HUYU ameondoka Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anasema, chama hicho kinanuka rushwa na kwamba yeye hawezi kugombea kwenye chama ambacho kimebeba wala rushwa. Ni James Lembeli, mbunge wa Kahama mkoani Shinyanga.

Akizungumza na wanachama wa CCM, wilayani Kahama, Lembeli amesema, “…nimekuja kuwaeleza, kwamba sitagombea ubunge katika jimbo hili kupitia CCM.”

Hii ilikuwa majira ya saa nne asubuhi. Mara baada ya kauli yake hiyo, kuliibuka tahahuri miongoni mwa wanachama wa chama hicho, waliokuwa wamejazana ofisini kumsubiri Lembeli achukue fomu ya kuwania nafasi hiyo.

Mbunge huyo machachari nchini alikuwa ni miongoni mwa wabunge waliojipambanua kupinga ufisadi, ndani na nje ya Bunge.

Kabla ya uamuzi huo, Lembeli amekuwa akilalamikia chama chake kubeba baadhi ya wagombea; kujenga makundi ya wanamtandao na kuanza kampeni kabla ya muda.

“Sitaki kuwa sehemu ya uchafu huu. Hivyo, nimeamua kutogombea ubunge kupitia CCM, ingawa nitagombea kupitia chama kingine,” ameeleza.

Amesema katika ziara zake jimboni amekuwa akipokea kadi nyingi ambazo zimetolewa na wagombea kinyume cha taratibu na taarifa hizo alizifikisha katika ofisi ya wilaya lakini hakuna hatua zilizochukuliwa.

Mara baada ya kutoa shutuma hizo, Lembeli aliondoka katika ofisi hizo bila kusalimiana na katibu wa chama hicho wilayani Kahama ambaye alikuja kumsubiri ili amkabidhi fomu za kuwania ubunge kupitia CCM.

MwanaHALISI Online, lilipoulizwa katibu wa CCM wilaya ya Kahama, Alexandulina Katabi, kuhusu madai ya Lembeli, haraka alisema, “madai hayo yanapaswa kupelekwa ofisini siyo kwenye magazeti.”

Alisema, kamati ya maadili ya chama hicho iliwahi kumuita mbunge huyo ili kuja kutoa ushahidi, lakini amegoma kufanya hivyo.

Alisema, “kadi feki zinajulikana kupitia kwangu kwa kuwa ndiye ninayezitoa.”

Taarifa ambazo zimepatikana baadaye zinasema, Lembeli anatarajiwa kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), muda wowote kutoka sasa.
Aidha, wabunge wengine wa CCM majina tunayo, wanatarajiwa kujiunga na chama hicho na kugombea ubunge katika majimbo mbalimbali nchini.


Mwanahalisi Online

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...