Skip to main content

MWENYEKITI WA BAVICHA AMVAA MCHUNGAJI MSIGWA UBUNGE IRINGA MJINI



Na Fredy Mgunda, Iringa

MWENYEKITI wa Baraza la Vijana la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Bavicha), Leonce Marto amechukua fomu ya kuwania ubunge katika jimbo la Iringa kupitia chama chake hicho.

Amechukua fomu hiyo siku moja tu baada ya Rais Jakaya Kikwete kulihutubia na hatimaye kulivunja bunge la 10 la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambalo uhai wake utakoma Agosti 20, mwaka huu.

Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, jimbo la Iringa Mjini limekuwa likiongozwa na Mchungaji Peter Msigwa ambaye pia alichaguliwa kupitia Chadema katika uchaguzi wa 2010.

Kwa kupitia taarifa yake aliyoisambaza kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii jana, Marto alisema; “nawasalimu nyote wenye mapenzi mema na Taifa letu la Tanzania na wapenda mabadiliko na demokrasia za ushindani ndani ya vyama vya siasa kwa minajili ya katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 .”

“Nianze kwa kuwashukuru watu wote ambao kwa muda wa uhai wangu wameshiriki kwa namna moja ama nyingine kuniwezesha kufika hapa nilipo . Pili nawashukuru viongozi , wanachama , wafuasi wa Chadema, ndugu, jamaa na marafiki ambao kwa wingi wenu sitaweza kuwataja wote,” alisema.

Marto alisema ameamua kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo iliyokuwa ikiongozwa na Mchungaji Msigwa baada ya kupata msukumo wa ndani na nje ya chama.

Alisema kwa haraka katika fahamu zake aliona jambo hilo ni zito na la hatari kulinganisha na watu wanavyosema kwasababu kazi ya umma ni kazi inayohitaji dhamira safi, uadilifu, umahiri, weledi, kujali ya maisha ya watu na maendeleo yao na zaidi sana kupenda na kutathmini Taifa na watu wake.

Marto alisema ilimchukua muda kujiridhisha pasipo shaka na jambo hilo kama anaweza kubeba wito huo wa kuwatumikia wananchi wa Iringa Mjini.

“Baada ya kutafakari kwa kina nilijipa mtihani wa kwanza wa kuzunguka nchi yetu na kukutana na jamii za watanzania. Kwa mantiki hiyo ninayafahamu kwa undani na kwa uhalisia wake maswala na matatizo muhimu yanayowakabili watanzania na wana Iringa Mjini,”alisema.

Marto alisema kwa kuwa anakidhi vigezo vya kikatiba, na kwa kuwa anaamini Mungu amempa karama ya uongozi ambayo watu wameiona na kumuomba agombee ubunge na kwa kuwa anayajua matatizo yanayowakabili watanzania na wana Iringa anayajua na yamemchosha kama yalivyowachosha watanzania wengine:


Na kwa kuwa Chadema kimejengwa kwenye mhimili na msingi mkuu wa Demokrasia pamoja na itikadi na falsafa yake ya Nguvu ya Umma na kwa kuwa anaamini viongozi bora wanapatikana kwa ushindani, kwa ujasiri wote aliopewa na Mwenyezi Mungu anatangaza rasmi kuomba ridhaa ya chama chake kugombea ubunge katika jimbo hilo.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...