Skip to main content

SAFARI YA MATUMAINI YA LOWASSA YAIBUKIA CHADEMA...!





WAZIRI Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) huku akiahidi kuendeleza safari yake ya matumaini iliyopigwa STOP na alivyoviita vikao vya Chama cha Mapinduzi (CCM) vilivyokiuka katiba yake.


Katika hafla rasmi ya kukabidhiwa kadi yake, iliyofanyika hii leo jijini Dar es Salaam, Lowassa alisema mchakato mzima wa kumpata mgombea urais kupitia CCM uligubikwa na hila, chuki, majungu na uzushi dhidi yake.


Lowassa alisema maamuzi yaliyofanywa na vikao vilivyochuja jina lake na ya wengine, hayajawahi kufanywa katika historia ya chama hicho..

Alisema Kamati ya Maadili na Usalama ya chama hicho ilipokonya madaraka ya Kamati Kuu na akakifananisha kitendo hicho na lugha ya mtaani ya kubaka demokrasia.

Alisema CCM ile aliyoiona Dodoma sio ile iliyomlea na kumkuza na akaomba watanzania wajiunge na kuing'oa madarakani


Alisema kama ilivyowahi kusemwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, kwamba CCM sio baba yangu wala mama yangu; “na mimi hii leo natangaza rasmi kujiondoa CCM na kujiunga na Chadema. CCM sio mama yangu wala baba yangu. Naondoka CCM najiunga Chadema.”


Akizungumzia kashafa ya Richmond, Lowassa alisema ameitolea majibu mara kwa mara lakini watu wanataka kuziba masikio.


Lowasa alisema hausiki na kashfa hiyo na madai yanayotolewa dhidi yake kama yana ushahidi, mwenye ushahidi huo aende mahakamani.


MBOWE
SIASA ni mchezo ambao wakati mwingine gia ni lazima ibadilishiwe angani na kwamba chama ambacho hakiamini mabadiliko hicho sio chama.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...