Skip to main content

ALBINO 43 WAMEUAWA NCHINI KATIKA KIPINDI CHA MIAKA KUMI ILIYOPITA




Kamishna Msaidizi wa Polisi toka ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai, Hussein Kashindye amesema kati ya mwaka 2006 na 2015 kulikuwa na matukio 56 yanayohusisha walemavu wa ngozi kuuawa au kujeruhiwa.

“Katika matukio hayo, 43 yalihusisha watu kuuawa na 13 kujeruhiwa. Katika kipindi hicho watu 12 walihukumiwa kunyongwa kwa makosa hayo na kesi nyingine 12 zipo kwenye hatua ya upelelezo huku nyingine zikitupiliwa mbali baada ya kukosekana kwa ushahidi” alisema.

Akiwasihi watanzania wote kushiriki katika mkakati wa kuwanusuru walemavu hao, Kashindye alisema suala la kuwalinda albino linatakiwa kuzingatia polisi jamii kwa kuanzia ngazi ya familia, kata, tarafa wilaya na mkoa.

Hivi karibuni Chama cha Wataalamu wa Ustawi wa Jamii (TASWO) kimefanya kongamano kubwa mjini Iringa lililowajengea uwezo wataalamu wa ustawi wa jamii nchini katika utetezi, ulinzi wa haki na ustawi wa watu wenye ulemavu hususani walemavu wenye ualbino.

Kauli Mbiu ya kongamano hilo lililofunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu ni “utetezi, ulinzi wa haki na ustawi wa watu wenye ulemavu hasa katika kuthibiti mauaji ya watu wenye ualbino na maambukizi ya virusi vya Ukimwi na Ukimwi.”

Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii, Radikira Mushi alisema; “ni fikra potofu kuamini viungo vya watu wenye ualbino vinawawezesha kubadili maisha kwa kuwaondoa katika wimbo la umasikini.”

Naye, Katibu Mtendaji wa TASWO, Nicolaus Mshana alisema mbali na mauaji, walemavu hao wana changamoto za umasikini na maambukizi ya VVU na Ukimwi hali inayosababishwa na mazingira wanayoishi, aina yao ya uelemavu, uelewa mdogo wa VVU na Ukimwi na uwezo wa wataalamu katika kutoa huduma kwa kundi hilo hasa kwa wasioona vizuri.

Kwa upande wake mmoja wa viongozi wa chama cha walemavu wa ngozi mkoani Iringa, Hellen Machibya aliitaka serikali kuwapa kipaumbele walemavu wanapohitaji kupata huduma mbalimbali zinazowahusu.

Akizungumzia jinsi wanavyopata kwa shida huduma za afya, Machibya alisema wamekuwa wakitibiwa kama wagonjwa wengine pamoja na kueleweka kwa tatizo lao la ngozi.



Mbali na wawakilishi wa TASWO, kongamano hilo lililofanyika mjini hapa, lilishirikisha maafisa ustawi wa jamii, polisi, mashirika ya haki za binadamu, walemavu, Tacaids, ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali, shirika la JSI/CHSS na shirika la kitaalamu la NASW la Marekani.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...