Skip to main content

BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO (TADB) YAFANYA BONANZA LA NANENANE MKOANI LINDI



Kaimu Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Bi. Miriam Mtima akizungumza wakati wa kufungua bonanza la Nanenane lilioandaliwa na benki ya Maendeleo ya Wakulima (TADB), jana mkoani Lindi.


Mkurugenzi wa Mikopo wa benki ya Maendeleo ya Wakulima, Bwana Robert Paschal akitoa hotuba ya ufunguzi wakati wa uzinduzi wa bonanza la Nanenane katika viwanja vya Ilulu mkoani Lindi jana.


Kaimu Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Bi Miriam Mtima akipiga mpira kuashiria ufunguzi wa bonanza la Nanenane lilioandaliwa na benki ya Maendeleo ya Wakulima (TADB), jana mkoani Lindi.


Vijana wakishiriki shindano la kuvuta kamba.


Vijana wakishiriki mashindano ya riadha.


Mashindano ya kukimbia na magunia.


Kikundi cha Ngoma na sarakasi cha Akoa Mpiluka kikitoa burudani.

Benki mpya ya Maendeleo ya Kilimo, leo imefanya bonanza maalumu la kuhamasisha wananchi kushiriki katika uzinduzi wa benki hiyo utakaofanyika katika kilele cha maonyesho ya Nanenane yanayoendelea hapa mkoani Lindi.

Katika bonanza hilo lililojumuisha michezo mbalimbali kama vile ngoma za jadi, muziki, mpira wa miguu na mpira wa pete kwa wanawake lilianza majira ya saa nane mchana na kukamilika saa kumi na mbili jioni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamasha hilo, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Bi Miriam Mtima amewataka wakazi wa Lindi hasa vijana kujipanga kutumia fursa zitakazotolewa kupitia benki hiyo na kwamba ofisi yake iko tayari kushirikiana nao watakapoanzisha vikundi kwa ajili ya kujishughulisha na kilimo.

"Niwahamasishe tujitokeze kwa wingi tarehe nane, Rais atakuja kuizindua benki hii maalumu kabisa kwa wakulima ambayo itatoa fursa za mikopo kwa vijana watakaoungana kwa ajili ya shughuli za kilimo’ alisema Bi Mtima.

Awali katika hotuba ya kumkaribisha Mgeni Rasmi katika bonanza hilo, Mkurugenzi wa Mikopo wa benki, Bwana Robert Paschal amesema kuwa bonanza hilo ni mwanzo wa shughuli mbalimbali zitakazoendelea mkoani humo kama utangulizi wa shughuli kubwa ya uzinduzi.

"Bonanza hili la leo na matembezi ya hisani yatakayofanyika siku ya ijumaa ni mwendelezo wa shughuli mbalimbali zinazofanywa na Benki ya wakulima ili kuwaandaa wananchi na hasa wakulima na wafugaji kushiriki kikamilifu katika uzinduzi wa benki yao siku ya jumamosi kwa malengo makuu mawili, kwanza waielewe nini hasa adhima ya serikali kuanzisha benki ya kilimo, baada ya kuilewa wajiandaye kutumia fursa zitakazoletwa na benki hii" alisema Robert Paschal.

Benki hiyo itakayofunguliwa rasimi kesho tarehe 7 jijini Dar es Salaam na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr Jakaya Mrisho Kikwete na baadae kuzinduliwa rasmi katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa mjini Lindi yakiwa na lengo la kuchochea maendeleo ya kilimo kwa kutoa mikopo kwa wakulima wadogo na wakati.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...