Skip to main content

BENKI YA MAENDELEO YA KILIMO YASHIRIKI NANENANE KITAIFA MKOANI LINDI



Mmoja wa wafanyakazi wa benki ya Maendeleo ya Wakulima, Geofrey Mtawa akizungumza na moja ya wadau waliotembelea banda lao katika maonyesho ya Nanenane.

Na Mwandishi wetu

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania inashiriki maonesho ya kilimo ya Nanenane kitaifa kwa mara ya kwanza mkoani Lindi mwaka huu kwa lengo la kutambulisha huduma zake kwa wadau wake wakuu, wakulima.

Katika maonesho hayo yaliyofunguliwa rasmi jana jumanne na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda, benki hiyo inatoa elimu na kujitambulisha kwa wakulima kwa kuwaelezea huduma zake zenye lengo la kuanzisha mtizamo mpya wa kukiendeleza kilimo kupitia kushirikisha wadau mbali mbali, kuangalia kila mnyororo wa thamani kwa ukamilifu wake, pamoja na kuwa na ubunifu katika kuchangia kifedha kwenye miradi ya muda mrefu, ya kati na muda mfupi kwenye sekta ya kilimo.


Akifungua maonesho hayo Waziri Mkuu Mh. Pinda, alisema kuwa Nanenane ni shamba darasa kwa wakulima kwa kuwa kupitia maonesho hayo wakulima watajifunza mbinu mbalimbali zenye kuongeza tija katika kilimo chao, na pia kujifunza wapi wanaweza kupata msaada kwa ajili ya kuinua kilimo chao sambamba na kujua namna wanavyoweza kutumia zana za kisasa ili kuongeza tija katika kilimo.

Benki ya Maendeleo ya Wakulima imeanzishwa maalum kwa ajili ya kuinua kilimo na itakuwa ikitoa huduma za uwezeshaji kwa wakulima na wafugaji kupitia wadau mbalimbali wa katika sekta ya kilimo ili kuhakikisha kuwa pamoja na mambo mengine wakulima wa kitanzania wanafikiwa na zana za kilimo kama vile mbegu za kisasa, pembejeo, uwezeshaji wa vifaa vya usindikaji mazao ili kuongeza tija katika shughuli za kilimo.

Kwa wadau wanaotembelea banda lake hapa Nanenane, warapata fursa ya kuona vibanda vidogovidogo baadhi vikisheheni wakulima, wasindikaji na wauzaji wa bidhaa walizochakata wenyewe kutoka mashambani kwa upande mmoja lakini pia wako wadau wanaowezesha wakulima kama vile taasisi za utafiti wa mbegu za kilimo, wauzaji wa zana za kilimo kama SUMA JKT ili kuisaidia benki hiyo kufafanua namna itavyowezesha mfumo wa killimo na kuhakikisha kuwa mkulima anapata huduma hiyo kwa urahisi zaidi.

Benki ya Maendeleo ya kilimo Tanzania inatarajiwa kuzinduliwa rasmi tarehe nane katika kilele cha maonesho haya ya Nanenane na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimwa Jakaya Mrisho Kikwete.


Muonekano wa nje wa banda la benki ya wakulima la Nanenane.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...