Skip to main content

CHADEMA YAZINDUA KAMPENI JIMBO LA KALENGA






Na Mathias Canal, Iringa 
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia Umoja wa katiba ya Wananchi {UKAWA} kimezindua kampeni zake katika Jimbo la Kalenga lililopo mkoani Iringa kwa muktadha wa kuanza vyema mikikimikiki ya kumnadi mgombea wake ambaye mara kadhaa amesikika akisema jimbo hilo limekosa muwakilishi wa wananchi bungeni. 

Chadema/ukawa inataraji kuanza kampeni zake za kumnadi mgombea wa Urais, wagombea ubunge, na udiwani mara baada ya uzinduzi wa kampeni zinazotaraji kufanyika mwishoni mwa wiki hii.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hizo zilizofanyika katika eneo la Ifunda, mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema/Ukawa, Mdede Mussa Leonard amesema kuwa ameamua kugombea jimbo hilo kwa kuwa ni mkazi wa Kalenga hivyo hakusoma kwenye kitabu changamoto za jimbo na wala hana haja ya kusimuliwa.


Amesema kuwa lengo mahususi la kugombea jimbo hilo ni kuhakikisha anaibana serikali na kushirikiana na wanakalenga wa ndani na nje ya jimbo na wadau mbalimbali wamaendeleo kuhakikisha Jimbo hilo linakwamuliwa kutoka kwenye mkwamo wa maendeleo na huduma duni za kijamii.


Ameeleza kusikitishwa sana na ukosekanaji wa maji jimboni hapo, ukosefu wa barabara nzuri ambazo zitawasaidia wananchi kusafirisha mazao yao, gharama kubwa za elimu ambapo ameeleza kuwa serikali imefuta ada kwa shule za serikali lakini imesahau kufuta michango ambayo ndiyo imekuwa mikubwa zaidi.


Mdede ambaye ni mzaliwa wa kijiji cha Kipera, Kata ya Nzihi, ana umri wa miaka 27, shahada ya udaktari ya chuo kikuu cha Afya ya tiba Bugando amewahi kuwa Rais wa chuo hicho kwa kipindi cha mwaka mmoja sawia na kuwa Rais wa vyuo vikuu vyote Tanzania bara na visiwani TAHLISO. 

Mdede amekuwa kiongozi wa ngazi mbalimbali za chama ikiwa ni pamoja na mwaka 2012-2013 alikuwa muasisi na mwenyekiti wa Chadema chuo kikuu cha Bugando, 2013 alipokuwa mwenyekiti wa chadema kwa vyuo vyote vya mkoa wa Mwanza.

Aidha Mdede ameshiriki mafunzo ya uongozi kwa marais wa vyuo vikuu vya Afrika Mashariki yaliyofanyika Arusha mwaka 2013 sambamba na kuhudhuria ziara ya mafunzo kiuongozi nchini China.

Wakati wa uzinduzi wa kampeni jimboni humo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chadema ngazi ya Jimbo, Wilaya na mkoa, Mdede alisema kuwa jimbo hilo lina jumla ya Kilomita 4038.1, Wakazi 15079,Tarafa 3,Kata 15,Vitongoji 434, na Vijiji 75, hivyo anaamini endapo watampa ridhaa atafika kila mahali na kuhakikisha changamoto za wakazi wa jimbo hilo zinatatuliwa kwa kiasi kikubwa. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa BAVICHA mkoa wa Iringa, Leonce Marto amesema kuwa serikali ya chama cha mapinduzi ambayo inamaliza muda wake imeshindwa kuwawezesha wananchi kupata hata pembejeo za kilimo, pamoja na nchi ya Tanzania kuwa na rasilimali nyingi ikiwa ni pamoja na madini, gesi, maziwa, bahari na vivutio mbalimbali ikiwa ni pamoja na mbuga za wananyama.


Alisema Tanzania imekosa mafanikio na kuendelea kubaki nyuma kimaendeleo kwa sababu ya udhalimu na ubovu wa uongozi wa CCM ambao asilimia kubwa wanatuhumiwa katika kesi mbalimbali ikiwa ni pamoja na ufisadi. 

Sawia na kufanyika kwa uzinduzi huo ambao unataraji kufanyika kwa ngazi ya Tarafa ambapo hiyo itakuwa awamu ya kwanza lakini utaendelea kwa awamu ya pili ngazi za vijiji mara baada ya kufanyika uzinduzi wa kampeni za chama hicho kitaifa.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...