Skip to main content

TANAPA KUKUSANYA ZAIDI YA 2.5BN/- KAMPENI YA KUHAMASISHA UTALII YA NDANI


Kushoto kwenda kulia ni Afisa Utalii Nyanda za Juu Kusini Gervas Mwashimaha,  Ofisa Utalii wa Tanapa wa ofisi ya Utalii Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Risala Kabongo, Kaimu Meneja Masoko TANAPA Victor Ketansi na Afisa Mawasiliano Mwandamizi TANAPA Catherine Mbena wakiongea na wanahabari mkoani Iringa jana. (Picha na Friday Simbaya)

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia hifadhi zake 16 linakusudia kukusanya zaidi ya 2.5bn/- katika kampeni ya kuhamasisha watu kutembelea hifadhi za taifa ili kuhamasisha utalii wa ndani, yeney kauli mbiu yake, “Tembelea Hifadhi Uzawadike.”

Kaimu Meneja Masoko TANAPA, Victor Ketansi akiongea na waandishi mkoani Iringa jana iliweka msisitizo katika kutangaza na kuhamasisha utalii wa ndani ili kupunguza utegemezi kwa watalii wa kigeni. 

Alisema kuwa TANAPA kwa kushirikiana na makala wa utalii (tour operators)katika kampeni hiyo ya miezi sita (6) iliyoanza Julai 1 hadi Desemba 31, 2015 watanzania watumia fursa hii kutembelea Hifadhi za Taifa na kujipatie zawadi kemkem katika kipindi hiki cha kampeni.

Alisema kwa pamoja na kwamba utaburudika, kushangaa na kufurahia kuona vivutio mbalimbali, pia utapata zawadi mbalimbali zitakazotolewa kwa kila atakayetembelea hifadhi wakati huu wa uhamasishaji.

“Washirika/wadau wetu wapo katika mikoa ya Mwanza, Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Iringa, Morogoro na Mbeya mjini,” alisema kaimu meneja masoko wa TANAPA.

Zawadi zitakazotolewa ni DVD za wanyama,Vitabu vya wanyama, Tshirts, Kofia, Tai za TANAPA, zawadi nono ya kwenda kutalii katika Hifadhi ya Taifa Serengeti au Gombe kwa muda wa siku TATU na kulala katika hotel yenye hadhi ya Nyota tano. 

Hata hivyo, Kaimu Meneja Masoko TANAPA, Victor Ketansi alisema kuwa tangu kuanzisha kwa kampeni za kuhamasisha jamii tembelea hifadhi za taifa utalii wa ndani umeomgezeka ambapo kwa mwaka watalii 427,208 alitembea hifadhi za taifa.

Kwa Hifadhi ya Saanane na Kilimanjaro zawadi itatolewa kwa taasisi itakayopeleka idadi kubwa ya watalii.

Kampeni hii na zawadi husika haziwahusu wafanyakazi katika kampuni za kitalii na mahoteli yaliyoko ndani na hifadhi.

Mchanganuo wa Zawadi zitakazotolewa.
Katika kipindi hiki cha kampeni kwa yeyote atakayetembelea hifadhi zaidi ya mara moja atapata zawadi isipokuwa kwa hifadhi za Taifa Saanane na Kilimanjaro (Hizi zina zawadi kwa utaratibu tofauti).

Ukitembelea hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara moja utajipatia DVD yenye wanyama mbalimbali.

Ukitembelea hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara mbili utapata DVD ya wanyama na fulana ya TANAPA, Kofia au Tai.

Ukitembelea hifadhi ya Taifa yoyote zaidi ya mara tatu utajipatia DVD yenye wanyama mbalimbali, fulana, Kofia, Tai na Kitabu cha wanyama.

Ukitembelea hifadhi zaidi ya mara nne utapata zawadi zote hapo juu pamoja na zawadi ya juu kabisa ambapo, utapelekwa kutalii katika Hifadhi ya Taifa Serengeti au Gombe (kuangalia sokwe) na kulala katika hotel yenye hadhi ya nyota tano kwa muda wa siku TATU kwa gharama za TANAPA.

Kwa hifadhi za Kilimanjaro na Saanane: Itazawadiwa taasisi au mtu itakayo peleka wageni wengi zaidi kipindi cha kampeni hii Julai- Disemba, 2015.

Saanane-Mtu atakayepeleka watalii wasiopungua 1500 atapewa zawadi ya juu kabisa

Kilimanjaro -Taasisi itakayopeleka watalii wasiopungua 150 kwa kipindi chote cha kampeni itajipatia zawadi ya juu kabisa.

MUDA WA KAMPENI 
Kampeni hii itakuwa ya miezi sita (6). Kuanzia Julai 1 hadi Disemba 31, 2015

VITUO VYA KUJIANDIKISHA NA KULIPIA 
Vituo vipo mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Iringa, Morogoro na Mbeya Wadau wa utalii wote (tour operators) wanakaribishwa kushiriki.

Muhimu kwa watalii wetu:

Kujiandikisha jina na namba ya kitambulisho cha aina moja kila aingiapo hifadhini ili tumtambue kwa ajili ya zawadi.

Wenye usafiri binafsi wanaweza tembelea hifadhi bila kupitia vituo vilivyotajwa hapo juu.Wazingatie kujiandikisha katika kitabu maalum kilichopo katika lango la kuingilia hifadhini.

Huduma za malazi ya bei nafuu ndani ya hifadhi zinapatikana. Vituo vyetu vilivyotajwa hapo juu vitatoa taarifa zote kwa aina ya utalii wowote unaohitaji ndani ya hifadhi.

Sheria na taratibu za hifadhi ziendelee kuzingatiwa wa kutoa elimu ya uhifadhi ili kuhakikisha jamii inanufaika na shughuli za uhifadhi katika maeneo yanayozunguka hifadhi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...