Skip to main content

Waliojitoa Chadema wapeta ACT Wazalendo


Mwanahamisi Muyinga


Iringa. Makada wa Wawili wa Chadema Mbunge viti maalumu anayemaliza muda wake Chuki Abwao na aliyekuwa mmoja wa watia nia Jimbo la Kalenga aliyeshindwa kwenye kura za maoni wameibuka kidedea kwenye kura za maoni kuwania ubunge kupitia chama cha ACT Wazalendo.

Makada hao waliibuka washindi kwenye uchaguzi uliofanyika juzi Chuki Abwao akishinda jimbo la Iringa mjini na Mwanahamisi Jimbo la Kalenga.

Makada hao sasa wanasubiri vikao vya juu vya chama ili kuidininisha kuwania ubunge na ikiwa vikao hivyo vitabiri Chuki atapambana na Mbunge wa Iringa Mjini anayemaliza muda wake Mchungaji Peter Msigwa, Mgombea ubunge kupitia CCM anayesubiri vikao vya juu vya chama hicho Frederick Mwakalebela na wagombei wa vyama vingine ikiwa watajitokeza.

Wakati Chuki akitarajia kupambana na wagombea hao Mwanahamisi anatarajia kupambana na Mbunge wa sasa anayemaliza muda wake Godfrey Mgimwa ambaye pia ni mshindi wa kura za maoni na kada mmoja kati ya Lucas Mwenda na Mussa Mdede wote kutoa Chadema ambao walipata kura 64 kila mmoja.

Katika uchaguzi uliofanyika kwenye ofisi za ACT Wazalendo Mkoa wa Iringa Chuki aliwashinda washindani wake Daud Masasi na Dk Ben Kapwani kwa baada ya kupata kura 23 akimuacha Masasi kwa kura mbili baad aya kupata kura 21 huku Dk Kapwani aliyetangaza kujitoa akipata kura tatu.

Katika uchaguzi uliofanyika kwenye eneo la Kihodombi kata ya Mlandege Mwanahamisi aliibuka mshindi kwa akupata kura 10 akifuatiwa na Daniel Mwangili aliyepata kura 7 huku Edward Mtakimwa na Kiduo Mgunga wakipata kura 3 kila mmoja.



Hata hivyo matokeo ya Iringa mjini yalipata ukakasi baada ya mmoja wa wagombea ambaye ni katibu Mwenezi wa ACT mkoa wa Iringa akigomea kusaini matokea hayo kwa madai kuwa yaligubikwa na vitendo vya rushwa.

Hata hivyo madai hayo yalipingwa na Mwenyekiti uchaguzi Mjini Iringa Placid Kamonga aliyesema uchaguzi huo ulifanyika kwa uwazi na demokrasia ya kweli kwa kuwa kura zilipigwa na kuhesabiwa kwa uwazi.

Mwenyekiti wa ACT mkoa wa Iringa Kapwani alisema ni vema Masasi akasaini matokeo na kuendelea na mchakato wake kupinga matokeo ambao kwa mujibu wa waraka wa chama hicho mtu anayepinga matokeo atatakiwa kufanya kuwasilisha malalamiko yake ndani ya siku saba tangu kufanyika kwa uchaguzi.

Kwa upande wake Chuki ambaye alishinda uchaguzi huo aliwashukuru wapiga kura kwa akumuaamini na kueleza kuwa atahakikisha anafanya kazi ya kukijenga chama hicho kichanga kinachoingia katika uchaguzi mkuu kwa mara ya kwanza tangu kusajiliwa kwake.

Naye Mwanahamsi aliwashukuru wapigakura kwa kumuamini na kufafanua kuwa atahakiksha anatumia taalamu yake ya kilimo kuinua maisha ya wakazi wa Kalenga.

Katibu wa chama hicho Mkoa wa Iringa Aram Mbilinyi aliwataka makada wote wa ACT Wazalendo kuungana pamoja kushirikiana na aliyeshinda ili kutafuta ushindi kwenye uchaguzi kwa kuwa ushindi wa matokeo yaliyotokana na kura za maoni na y a watu wote.

“Hapa hakuna mshindi sisi sote tumeshinda wito wangu kwenu tuungane pamoja kuhakikisha tunawaunga mkono hawa mama zetu katika kipindi chote cha kampeni tukiwa na imani kuwa wakishinda wao tumeshinda sote”alisema Mbilinyi.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...