Skip to main content

WANACHAMA zaidi ya 18, 000 wa CCM jimbo la Iringa Mjini kuamua leo

Katibu wa CCM wa Manispaa ya Iringa, Elisha Mwampashi (kulia) akiongea na wanahabari kuhusu mchakato upigajikura za maoni kwa waombaji 13 waliojitokeza kutafuta ridhaa ya chama hicho ili wapeperushe bendera ya ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini jana. Kushoto ni Mweneyekiti wa CCM wa Manispaa ya Iringa, Abeid Kiponza.

WANACHAMA zaidi ya 18, 000 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Iringa Mjini leo wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi wao kuwapigia kura waombaji 13 waliojitokeza kutafuta ridhaa ya chama hicho ili wapeperushe bendera ya ubunge katika Jimbo la Iringa Mjini.

Kura hizo za maoni zinafanyika baada ya wagombea hao kutumia siku 12 kuzunguka katika matawi 81 ya chama hicho kunadi sera zao ikiwa ni azma ya kila mgombea kutafuta kuungwa mkono ili achaguliwe kuwania ubunge katika jimbo hilo.

Ama zao ama zangu ya kura hizo inatarajiwa kujitokeza kwa wagombea hao ambao ni pamoja na Dk Augustino Maiga, Frederick Mwakalebela, Jesca Msambatavangu, Mahamudu Madenge, Nuru Hepautwa, Dk Yahaya Msigwa, Michael Mlowe, Addo Mwasongwe, Aidan Kiponda, Fales Kibasa, Frank Kibiki na Peter Mwanilwa.

Akizungumza na wanahabari hii leo, Katibu wa CCM wa Manispaa ya Iringa, Elisha Mwampashi alisema vituo 88 vitatumika kupigia kura hizo za maoni na matokeo ya kila kituo yatatangazwa vituoni ili kuepuka hofu ya kuwepo kwa mizengwe.

“Kila mgombea ameteua wakala wake ambao pamoja na wasimamizi wa kila kituo leo tumewapa mafunzo elekezi ya namna ya kuendesha kura hizo za maoni,” alisema.

Alisema vifaa kwa ajili ya kura hizo za maoni vimekamilika na kwamba vituo vyote vitafunguliwa kuanzia saa 2.00 asubuhi hadi saa 10 jioni,” alisema.

Alisema wanachama watakaoruhusiwa kupiga kura ni wale watakaokwenda katika vituo hivyo wakiwa na kadi zao za uanachama na kitambulisho cha mpiga kura.

“Tunahitaji pia kitambulisho cha mpiga sio kwa maana ya kukichukua, ni kwa maana ya kujiridhisha kwamba mwanachama anayeshiriki kuchagua mgombea ubunge atapiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25,” alisema.

Alisema matokeo ya jumla ya kura hizo za maoni yatatangazwa rasmi Jumapili asubuhi katika zoezi litakaloshirikisha waalikwa mbalimbali wakiwemo wazee wastaafu wa chama hicho, makada mashuhuri, viongozi wa taasisi mbalimbali za chama na waalikwa wengine.

Alisema kuibuka mshindi katika kura hizo hakumuhalalishii mgombea kwamba ameteuliwa na CCM kupeperusha bendera ya chama hicho mpaka pale vikao halali vya uteuzi vitakapothibitisha kwamba ushindi wake haukuwa na hila yoyote.

Kwa miaka mitano iliyopita Jimbo la Iringa Mjini limekuwa likiongozwa na Mchungaji Peter Msigwa aliyechaguliwa katika uchaguzi mkuu wa 2010 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...