Skip to main content

CCM WAPANIA KULIGOMBOA JIMBO LA IRINGA MJINI


Katibu wa CCM Mkoa wa Iringa, Hassan Mtenga (Picha na Maktaba)


KIU ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kukomboa Jimbo la Iringa Mjini kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu, inazidi kuongezeka baada ya mgombea udiwani wa CCM kata ya kihesa kuwataka wananchi kutomchagua mbunge aliyemaliza muda wake kupitia chama cha demokrasia na maendelo (Chadema) Mch. Peter Msigwa kwa kushindwa kutekeleza ahadi zake.

Mgombea huyo wa ata ya Kihesa, Kenani Kihongosi Laban alitoa rai katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za udiwani Kata ya Kihesa uliyofanyika viwanja vya kihesa sokoni jana.

Alisema kuwa mbunge huyo anayemaliza muda wa Jimbo la Iringa mjini Mchungaji Peter Msigwa (Chadema) aliahidi kujenga soko la kisasa la kihesa lakini hadi miaka mitano inakwisha soko hilo halijajengwa.

Aliomba wakazi wa kihesa wamchague katika uchaguzi mkuu wa 2015 iliakafanishe ujenzi wa soko hilo pamoja na mambo mengine ikiwemo masuala ya afya na elimu.

Alisema kuwa watangulizi wake waliopita hawajatekeleza ahadi walizoahidi lakini ni wakati kwa wananchi wa kata ya kihesa kumtuma yeye akatekeleze majukumu yao.

Kuhusu baadhi ya wananchi waliojenga milimani hususani eneo la mafifi mgombea huyo alisema akichaguliwa atakwenda kuwatetea ili wasibomolewe nyumba zao na Halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

Aliongeza kuwa ili kufanisha azima hiyo aliwaomba wananchi wamchague kusimamia kata hiyo pamoja nakumchagua mgombea ubunge kupitia chama cha mapinduzi (CCM) Frederick mwakalebela na mgombea urais kupitia chama hico Dkt John pombe magufuli ifikapo tarehe 25 oktoba mwaka huu.

Kenani Kihongosi aliwahi kuwa Katibu wa TAHALISO na  Waziri Mkuu wa Chuo Kikuu cha Iringa avitaja vipaumbele vyake ambavyo atakwenda kusimamia atakapochaguliwa kuwa diwani ni pamojana afya na elimu.

Mkutano huo wa uzinduzi wa kampeni ulihudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chama akiwemo katibu wa ccm mkoa wa iringa Hassan Mtenga pamoja na mwenyekiti wa wilaya ya Kilolo Seth Mwamoto.

Kwa upande wake, katibu wa ccm mkoa wa iringa Hassan mtenga ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo alisema kuwa moja ya ahadi ya CCM ni kuipandisha timu ya lipuli iliweze kuipandisha hadhi kutokana mbunge aliyemaliza muda wake kuitelekeza timu hiyo.

Alisema katika pitapita yake amegundua kuwa vijana wengi wanapenda michezo na kuwataka wananchi wa jimbo la iringa mijini kuchagua mgombea wa CCM Frederick Mwakalebela ili aweze kutimiza azma hiyo.

Alisema kuwa anauhakika kuwa mgombea urais Dkt John Pombe Magufuli atashinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu oktoba mwaka huu kwa sababu amefanikiwa kutembea vijiji zaidi ya 1,885 tangu kuanza kwa kampeni wakati mgombea urais kupitia UKAWA mpaka sasa ametembelea zaidi ya vijiji 420.

CCM ililipoteza jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu wa 2010 baada ya kuchukuliwa na Mchungaji Peter Msigwa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayemaliza muda wake.

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...