Skip to main content

LOWASSA AIBUKA KIDEDEA URAIS, UTAFITI MWENGINE



Taasisi ya Tanzania Development Initiative (TADIP) itakutana na waandishi wa habari Hotel ya Regency, Mikocheni, Dar es Salaam, leo saa 10.30 jioni kwa ajili ya kutoa matokeo ya utafiti wa kura ya maoni kuhusu Uchaguzi Mkuu.

Ngoja tuwasikilize na hawa kuwa watazungumza nini juu ya uchaguzi Mkuu.

======================

Kinachoendelea hapa Regency Hoteli muda huu ni George Shembusho Mkurugenzi wa Bodi ya TADIP, anazungumza na waandishi wa habari anasema walifanya mchakato wa utafiti kutokana na mahitaji na mazingira kuelekea Uchaguzi Mkuu 2015.

-TADIP ilifanya utafiti mwezi wa 5 na wa 6, anasema matokeo yaliharibika kutokana na mambo kuingiliana na bodi ya ukurugenzi iliukemea kutokana na baadhi ya watu kuuchukua na kuuchapisha kwenye gazeti Agosti 4.

-Anasema katika siku za karibuni kumetokea kasumba ya umma kutafsiri utafiti unaotolewa siku za hivi karibuni kwa njia tofauti kutokana na mazingira jinsi yalivyo.




Kushoto ni Kostastin Deus,Mtafiti Mwelekezi akiwa na George Shembusho Mkurugenzi wa Bodi ya TADIP

Anamkaribisha Kostastin Deus, Mtafiti Mwelekezi kueleza jinsi walivyofanya hadi kupata matokeo ya utafiti, TADIP ni kifupi cha maneno Tanzania Development Ini7a7ves Program. Ni taasisi isiyokuwa ya kiserikali iliyosajiliwa mwaka 2006.

-Tangu kuanzishwa kwake, TADIP imekuwa ikileta chachu katika maendeleo ya Tanzania kupitia programu yake ya “Maendeleo Dialogue”.
-
Anasema kupitia tafiti na midahalo, TADIP imekuwa ikiwaunganisha wananchi, wanataaluma, asasi za kiraia na watunga sera katika kushawishi michakato mbalimbali ya maendeleo.

-Tangu mwaka 2010, TADIP imekuwa ikijishughulisha na tafiti za kura ya maoni ya wananchi kuelekea uchaguzi mkuu.

Tafiti za kura ya maoni pamoja na mambo mengine hulenga kujua maoni ya wapiga kura juu ya utayari wao wa kupiga kura, kukubalika kwa wanasiasa katika nafasi ya Urais, Ubunge na Udiwani, na mitzamo ya wananchi juu ya taasisi na mifumo ya usimamizi wa uchaguzi.

-Katika hatua ya Kura ya Maoni anasema huu ni utafiti wa pili wa kura ya maoni kufanywa na TADIP kuelekea 25 Oktoba, wa kwanza ulifanyika mwezi Mei na Juni 2015. Utafiti huu umefanyika ndani ya wiki tatu za mwanzo za mwezi Septemba.

-Utafiti huu ulilenga wananchi waliojiandikisha kupiga kura katika mikoa 12 ya Tanzania. Lengo la utafiti lilikuwa mikoa ambayo ina idadi kubwa ya wananchi waliojiandikisha kupiga kura ka7ka daSari la kudumu la Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Kwa sababu zilizokuwa nje ya Taasisi, taarifa za mikoa 2 hazikuweza kupatikana kwa wakati (Tabora na Kagera)

-Watu 2500 walilengwa kupewa madodoso huku watu 2040 pekee ndo waliweza kushiriki kwa maana ya kurejesha dodoso. utaratibu wa kuchagua washiriki ulifanyika kwa njia ya nasibu (simple randomisation) huku kwa kila mkoa, walengwa wakigawanyika katika makundi matatu ya maeneo, mijini, miji midogo na maeneo ya pembezoni. Methodolojia...

-Aidha, wakusanya taarifa walichagua washiriki kwa kuzingatia uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kijamii kama vile elimu, jinsia, umri, kiwango cha elimu ya washiriki na kadhalika.

-Wahojiwa walipewa madodoso ya wazi (Open ended questionnaire) kwa ajili ya kujaza majibu ya maswali yaliyokuwa yanaulizwa na wale waliokuwa hawawezi kusoma na kuandika walisaidiwa kujaza taarifa na wakusanya taarifa.

-Jendwali na 1 hapo linaonyesha mgawanyo wa sampuli katika mikoa husika. Moja ya kigezo kilichotumika kuhoji ilikuwa ni mhusika kuwa amejiandikisha kupiga kura kwenye dasari maalum kwa mfumo wa kielekroniki yaani BVR.



George anatoa matokeo ya utafiti, na kusema matokeo haya yamempa Edward Lowassa kuwa mtu wa kwanza ambaye angechaguliwa kuwa Rais na pia anaelezea jinsi wafuasi wa vyama vya siasa wanavyopenda vyama hivyo ambapo CCM kimeonekana kuwa na wafuasi kwa asilimia 35, Chadema 32, CUF 2, NCCR Mageuzi 1, ACT 3, Vingine 2 na ambao hawana chama walikuwa ni asilimia 25




Pia utafiti uliangalia namna ya jinsi wagombea urais wanavyokubalika.

-Wananchi wangependa serikali ijayo iboreshe hali ya huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya, na maji.
Kujenga uchumi imara utakaoboresha hali ya sekta za kilimo na viwanda ili kuleta 7ja ka7ka utoaji wa ajira.
Kusimamia rasilimali za umma na mapambano dhidi ya rushwa .

-Asilimia 97% ya wanachi wana utayari wa kushiriki zoezi la upigaji kura CCM kinaongoza kwa wanachama ama wafuasi kwa asilimia 35% ikifuatiwa na CHADEMA (32%) huku wananchi wasiokuwa na vyama wala ufuasi wakiwa 25%.

-Vyama vingine ni pamoja na ACT 3%, CUF 2%, NCCR-Mageuzi 1% qEdward Lowassa anaungwa mkono zaidi katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha huku Dr John Magufuli akiungwa mkono zaidi na wananchi wa mikoa ya Dodoma na Morogoro John Magufuli anakubalika zaidi miongoni mwa wapiga kura wenye umri wa zaidi ya miaka 48 huku Edward Lowassa anakubalika zaidi miongoni mwa wapiga kura wenye umri wa chini ya miaka 47.

-Edward Lowassa angepigiwa kura na wanaume kwa uwingi kuliko wanawake huku Dr. Magufuli na Anna Mghwira wakiwa na uwezekano wa kupigiwa kura zaidi na wanawake ikilinganishwa na wanaume katika nafasi ya Ubunge, 53% ya wahojiwa walisema kuwa wangemchagua mgombea kutoka miongoni mwa vyama vinavyounda UKAWA (CHADEMA, NLD, CUF, NCCR), huku asilimia 40% wakisema wangechagua mgombea kutoka CCM qAsilimia 55 ya wananchi wangechagua mgombea anayetoka ka7ka vyama vya UKAWA ikifua7wa na CCM (37%).

-Vyama vingine ni pamoja ACT (3%), TLP (2%), UDP (0.6%) na asilimia (2.3) hawajafanya maamuzi qEdward Lowassa angeweza kupigiwa kura kwa asilimia 54.5 akifuatiwa na Dr. John Mafuguli 40% ambaye angefuatiwa Anna Mghwira 2.

George, anasema madodoso yao yalifanyika kwa lugha ya Kiswahili na kwamba utafiti utafiti huo waliudhamini wenyewe.

-Anasema bajeti ya utafiti huo ilikuwa Sh. Milioni 10 tu


Wamemaliza kuongea.
Attached Thumbnails

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...