Skip to main content

LOWASSA AKIWA JIMBO LA MTAMA, AZOA WANACHAMA WA CCM KIBAO




AZIMA UTATA WA MAKAIDI

Mgombea urais wa Chadema anayeungwa mkono na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa jana alimwomba mwenyekiti mwenza wa umoja huo, Dk Emmanuel Makaidi kujitoa kugombea ubunge katika Jimbo la Masasi na kumwachia mgombea wa CUF, Ismail Makombe baada ya kukataliwa na wananchi.


Uamuzi huo ulifikiwa katika Uwanja wa Bomani mjini Masasi, baada ya Lowassa kuwasimamisha wagombea hao jukwaani kuwanadi, lakini akapata upinzani mkali kutoka kwa wananchi alipompa nafasi Dk Makaidi.


Lakini kabla Makaidi hajasema chochote aliondoka katika mkutano huo na meza kuu ilijadiliana, ndipo mke wa Makaidi, Modesta aliposhauri waachwe wote wawili wachuane hoja ambayo ilikubaliwa na Lowassa ambaye alitangaza tena kuwa wagombea hao kila mmoja atapambana kivyake.


Awali, Lowassa alipotoa uamuzi wa kumuomba Dk Makaidi amwachie kijana huyo, uwanja mzima ulilipuka kwa nderemo na vifijo huku wananchi wakinyoosha mikono juu kuonyesha kukubaliana na uamuzi huo.


Hata hivyo, alivyobadilisha uamuzi huo, umati huo ulionekana kutomuunga mkono.


Lowassa alifika katika mkutano huo saa 7.28 mchana akitokea Mtwara baada ya kushindwa kufanya mkutano Tunduru kutokana na helikopta kukosa mafuta yaliyokuwa yameagizwa Dar es Salaam na yalipopatikana aliamua kwenda moja kwa moja Masasi.


Ilivyokuwa
Dk Makaidi alipopewa nafasi ya kuzungumza, wananchi walipiga kelele huku wakionyesha mikono juu kumkataa na kukatisha hotuba aliyokuwa ameanza kuitoa.


Lakini aliposimamishwa mgombea wa CUF, Makombe maarufu kama Kundambanda, alishangiliwa huku akimweleza Lowassa kuwa kura zake za urais anazo mfukoni kwa kuwa ndiye wananchi wanayemkubali.


Mgombea wa Chadema katika jimbo hilo, Mussa Sakaredi alijitoa ili kumuunga mkono mgombea aliyepitishwa na Ukawa.


Ndanda yaleyale
Kama ilivyokuwa Masasi, katika Jimbo la Ndanda, pia mgombea mmoja kati ya wawili wa Ukawa waliojitokeza kuwania ubunge alikataliwa na wananchi mbele ya Lowassa na kumfanya alikimbie jukwaa.


Hali hiyo ilijitokeza pale Meneja Kampeni wa Chadema, John Mrema aliposema anafahamu kuna mgogoro wa nani atakayegombea ubunge chini ya mwamvuli wa Ukawa kati ya NLD na Chadema, hivyo akatoa nafasi kwa kila mgombea kueleza matatizo ya jimbo hilo jipya.


Mgombea wa NLD, Angelous Gabriel alipopewa nafasi aliishia kumsifia Lowassa, jambo lililowafanya wananchi kupiga kelele wakisema anapoteza muda.


“Toka unapoteza muda, tokaaaaa,” walisikia wakipaza sauti.


Ilipofika zamu ya mgombea wa Chadema, Cecil Mwambe uwanja mzima ulilipuka huku akieleza kuwa katika jimbo hilo kuna tatizo la bei ya mazao, hivyo kama Lowassa akiingia madarakani, serikali yake iwatatulie matatizo yao.


Baada ya Mwambe kusema hayo wananchi walimshangilia na Lowassa alipopanda jukwaani aliwaita wagombea wote wawili na kuwahoji wananchi wanamtaka nani kati yao ambapo kwa sauti ya pamoja walijibu “Mwambeeeeeeeee”


Jambo hilo lilimfanya Gabriel wa NLD kushuka jukwaani na kuondoka. Alipoulizwa sababu ya kukataliwa alisema: “Kuna watu wameandaliwa na kununuliwa ili nisigombee Ndanda.”


Hata hivyo, wakazi wa Ndanda waliohojiwa walisema hawamjui mgombea huyo na wanashangaa kwa nini anang’ang’ania kugombea huku wakisema hajajiandikisha kupiga kura katika jimbo hilo, jambo ambalo Gabriel alikiri.


Mmoja wa wakazi hao, Charles Mtutu alisema: “Hatumjui hata jina na NLD haina kiongozi katika jimbo hili na hawajawahi kufanya mikutano.”


Mkazi mwingine, Athuman Hassan alisema: “Kwanza hatumjui, pili hajawahi kufanya kampeni zozote tangu Jimbo la Ndanda lilipopatikana.” (FULL HABARI BLOG)

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...