Skip to main content

Mabadiliko makubwa ya kisera kuinua wajasiriamali wadogo na wa kati



Mkuu wa utafiti na machapisho ESRF, Profesa Fortunata Makene akifungua warsha.


Mwasilishaji wa mada Hossana Mpango akizungumza na washiriki (hawapo pichani) kwenye warsha hiyo.


Washiriki wa warsha ya siku moja ya ujasiriamali mdogo na wa kati katika muktadha wa fedha iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF).

Na Mwandishi wetu

SERIKALI imetakiwa kufanya mabadiliko makubwa ya kisera kuwezesha kukua kwa viwanda vidogo na vya kati nchini.

Kauli hiyo imo katika utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) kuhusu ukuaji wa sekta hiyo katika muktadha wa upatikanaji wa fedha.

Akiwasilisha utafiti huo mmoja wa watafiti Hossana Mpango alisema kwamba kwenye utafiti wao wamebaini mgongano mkubwa wa kisera na utendaji, unaosababisha kukwama kwa maendeleo ya sekta hiyo.

Alisema ingawa kuna tatizo kubwa la ajira ambalo limefanya watu wengi kukimbilia kujiajiri wenyewe, kuna changamoto kubwa katika sekta hiyo hasa sera na uwapo wa mlolongo wa taasisi zinazopishana mamlaka na huku wakiwa ndio wanatoa leseni.

Alizitaja taasisi hizo zinazopishana mamlaka kama Shirika la Viwango nchini (TBS), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) mamlaka ya kodi (TRA) halmashauri mbalimbali nakadhalika.

Alisema mabadiliko ya kisera yatawezesha kutengeneza muundo unaojali ukuaji wa sekta hiyo hasa kwa kuangalia kodi zinazolipwa ambazo kwa sasa ni za aina moja bila kuangalia uwekezaji unaohusika.

Sekta hiyo ya wajasirimali wadogo na wa kati yenye watu milioni 3 kwa mujibu wa utafiti wa mwaka 2012 inakabiliwa na tatizo la kutokua kutokana na vikwazo mbalimbali vikiwemo pia kukosekana kwa mafunzo ya ujasirimali na uwezo wa kupata fedha za mtaji.

"Ni dhahiri upatikanaji wa fedha kutoka nje ili kuendeleza mtaji ni tatizo. Lakini tatizo hili linakuwagumu zaidi kutokana na riba kubwa, uchelewefu wa kupata mikopo, rushwa katika utoaji na ukosefu wa nidhamu ya fedha kwa wakopaji” alisema Hossana.

Alisema pamoja na mambo hayo kuna matatizo mengine makubwa yanayokwamisha ukuaji wa sekta hiyo. Matatizo hayo mengine ni gharama kubwa zinaootokana na haja ya kukidhi masharti ya uendeshaji wa viwanda hivyo vidogo na vya kati, tozo zinazojirudia, ukosefu wa soko na elimu ndogo ya wajasirimali.

Alisema mabadiliko ya kisera yatasaidia kuimarisha sheria na kuweka sawa mwelekeo wa sekta hiyo kwa kuzingatia kwamba inahitaji mchango mkubwa wa nje ili kukua.

Alisema mathalani ingawa kuna SACCOS, taasisi hizo zinashindwa kwenda kukopa kutokana na riba kubwa na kuwapo kwa mfumo wa kodi na makato mengine yakiwemo ya tozo usiokuwa na tija.

Alisema suluhu nyingine inayostahili kufanywa ni kwa taasisi za kifedha kufuata tabia njema za kimataifa za utoaji wa mikopo unaozingatia pamoja na mambo mengine ukubwa wa mikopo na malipo kwa kuangalia manufaa ya kiuchumi.

"Ili viwanda hivi vya chini na kati kukua masuala ya kifedha na yasiyo ya kifedha ni lazima yaangaliwe na kushughulikiwa..." alisema.

Matatizo mengine ni pamoja na sekta hiyo kukosa msaada huku taasisi mbalimbali zinazohitaji kushirikiana zikifanya vitu kila mmoja na wake.

Taasisi hizo ni SIDO, TRA, WDF, YDF, BRELA na pia miundombinu inayokera katika maeneo hasa ya vijijini.

Pia ili kukuza sekta hiyo ni vyema serikali ikatengeneza miundombinu inayojkidhi haja ya ukuaji wa sekta hiyo kama maghala, masoko, barabara, maji, umeme kwa lengo la kupunguza gharama za kufanya biashara.

Pia utafiti huo ulishauri kwamba serikali ni lazima kutenga fungu ambalo litatumiwa na taasisi kama SIDO, NEEC na hata maofisa biashara wa wilaya kwa ajili ya mafunzo ya ujasirimali na uendeshaji wa biashara.

Mapema Mkuu wa idara ya utafiti na machapisho wa ESRF Profesa Fortunata Makene, aliwataka washiriki wa warsha hiyo kutoa michango katika kuboresha uelewa ili serikali iweze kutatua kizungumkuti cha ukuaji wa sekta hiyo.




KAWAIDA


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...