Skip to main content

Malunde: Wanawake msikubali kurubuniwa kuuza shahada za kupigiakura


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi (DED), Saada Malunde



ZIKIWAZIMEBAKIA siku chache kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka huu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi (DED), Saada Malunde amewataka wanawake kudhibiti shahada zao za kupigiakura na wasikubali kurubuniwa kuuza shahada hizo.

Alisema kuwa katika hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu oktoba mwaka huu wanawake mara nyingi wanatumika kisiasa na wanasiasa kwa rubuniwa kwa vitu vidogo.

DED huyo alisema hayo wakati akifungua semina ya uongozi wa mwanamke katika kilimo, upatikanaji wa huduma za ugani na pembejeo za kilimo kwa wanawake wakulima mjini Mafinga jana.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Shirika la Land O' Lakes chini ya ufadhili wa Shirika la Misaada la watu wa Marekani (USAID) kupitia Mradi wa Ubunifu katika Masuala ya Kijinsia na kuimarisha Uhakika wa Chakula katika ngazi ya kaya. 

“Mujue kuwa mukizitoa shahada zena itakuwa mumeuza utu wenu kwa kipindi cha miaka mitano ijayo”, alisema Malunde.

Alisema kuwa wanaweza kuja watu wakataka muwape shahada zenu za kupigia kura, nakunasihini hata kuwaonesha musiwaoneshe achilia mbali kuwapa.

Hata hivyo, mkurugenzi huyo wa halmashauri ya mufindi walisahi wanawake hao kuzingatia mafunzo hayo kwa kuyatumia kuboresha maisha kwa kulima kilimo cha biashara.

Aliongeza kuwa wanawake mara nyingi wanakabiliwa na upatikanaji mdogo wa, ardhi ya kutosha, zana za kilimo na pembejeo, mikopo, huduma za ugani na ushauri wa kitaalamu na Miundombinu bora na teknolojia mpya.

Naye, Mkurugenzi wa Mradi wa Ubunifu katika Masuala ya Kijinsia na kuimarisha Uhakika wa Chakula katika ngazi ya kaya, Dkt. Rose Kingamkono wanawake ni mali muhimu katika maendeleo ya kilimo duniani kote. 

Alisema kuwa katika nchi nyingi za Afrika hadi asilimia 80 ya kazi za shamba hufanywa na wanawake. 

Pia kaya nyingi zinazojihusisha na kilimo katika nchi zinazoendelea zinaongozwa na wanawake.

“Wanawake wangeweza kuongeza uzalishaji kwenye mashamba yao kwa asilimia 20–30 kama wangekuwa na upatikanaji sawa wa zana za kilimo, pembejeo, na huduma za ugani kama wanaume,” alisema. 

Jumla ya washiriki 45 kutoka wilaya za iringa, Mufindi na kilolo wamepatiwa mafunzo ya uongozi wa mwanamke katika kilimo, upatikanaji wa huduma za ugani na pembejeo za kilimo kwa wanawake wakulima.



mwisho

Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...