Skip to main content

MO DEWJI ANYAKUA TUZO YA MWAKA YA MFANYABIASHARA ANAYESAIDIA ZAIDI JAMII



Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker akimkabidhi tuzo ya '2015 Philanthropist of the year-East Africa' Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika sherehe zilizofanyika hoteli ya DusitD2 jijini Nairobi.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog).


Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akizungumza kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 (AABLA). Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akipozi katika picha ya kumbukumbu na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akiwa ameshikilia tuzo yake.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akibadilishana mawazo na baadhi ya wafanyabiashara wakubwa jijini Nairobi ambapo pia walimpongeza.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji katika picha ya kumbukumbu na mmoja wa wageni waalikwa kwenye hafla ya tuzo za All Africa Business Leaders Awards 2015 zilizofanyika kwenye hoteli ya Dusit D2 jijini Nairobi.


Mohammed Dewji, CEO of MeTL Group....2015 Philanthropist of the Year-East Africa.

Na Mwandishi Wetu

BILIONEA anayemiliki kampuni kubwa ya Mohammed Enterprises nchini (MeTL), Mohammed Dewji `Mo’ ameshinda Tuzo ya Mfanyabiashara wa Mwaka anayejitoa zaidi kuisaidia jamii kunufaika kutokana na biashara zake, akiwa mshindi wa Afrika, Kanda ya nchi za Afrika Mashariki katika tuzo zilizofanyika juzi jijini Nairobi, Kenya.

Katika tuzo hiyo ya heshima kwa wafanyabiashara Afrika inayoratibiwa na Kituo cha Biashara cha Televisheni ya CNBC Afrika, Dewji alishindanishwa na mabilionea raia wa Kenya, Ashok Shah wa kampuni ya Apollo Investment Limited na Damaris Too-Kimondo anayemilikia kampuni ya Shrand Promotions.

Katika sherehe hizo zilizofana, Dewji alikabidhiwa tuzo yake na Mkurugenzi Mtendaji wa CNBC Africa, Roberta Naicker.

Ushindi wake umechangiwa kwa kiasi kikubwa na kitendo cha Dewji ambaye pia ni mwanasiasa aliyekuwa mbunge wa Singida Mjini kwa miaka kumi, kujihusisha na misaada yenye lengo la kupambana na umasikini kupitia sekta mbalimbali kama elimu, maji, watu wenye ulemavu na pia uwezeshaji kiuchumi, matukio ambayo yamelenga na kubadili hali ya watu maskini zaidi katika jamii.

Washindi hao wa Kanda ya Afrika Mashariki watashindanishwa na washindi wengine kutoka Kanda ya Kusini mwa Afrika na Afrika Magharibi Novemba 13, mwaka huu huko Sandton, Johannesburg nchini Afrika Kusini ili kupata mshindi wa jumla wa bara la Afrika.

Akizungumza mara baada ya kutunukiwa tuzo yake hiyo yenye heshima kubwa, aliwashukuru waandaaji, jarida la Forbes na majaji kwa kumuona anastahili kwa tuzo hiyo ya kipekee.

Alisema, kwake ni faraja kubwa kupata heshima huyo na amekuwa na ndoto za kusaidia watu wa Tanzania kukabiliana na changamoto wa kasi ya maendeleo barani Afrika na kwamba ili kuendana na kasi hiyo, miongoni mwa juhudi zinazotakiwa ni kuwawezesha kupata elimu bora, hasa wa maeneo ya vijijini.

“Ninaamini tukiunganisha nguvu, nchi za Afrika zina nafasi kubwa ya kuwa na wataalamu wake watakaosaidia kusukuma gurudumu la kiuchumi Afrika na hivyo kuboresha hali za maisha za watu wa bara hili,” alisema bilionea huyo kijana aliyeanzishwa taasisi yake ya Mo Dewji Foundation kwa lengo la kuisaidia jamii.

Alisema kwamba hilo ni tukio kubwa sana kwake na kumnukuu Maya Angelou, akisema: “Ukisoma, fundisha. Ukipata, toa.” Aliongeza kuwa, kwa kuwa amebarikiwa na Mungu kupata vyote, anakusudia kuendelea kuuelimisha umma juu ya kufanya mapinduzi ya kielimu, afya, na maeneo mengine ya ustawi wa jamii, huku akiahidi kusaidia kwa kila atakachojaliwa.

Dewji mwenye umri wa 40 ambaye kwa sasa ndiye bilionea kijana zaidi Afrika kwa vijana wasiozidi umri huo, akiwa pia miongoni mwa mabilionea 55 wanaoongoza kwa utajiri Afrika, anaongoza kampuni yenye makampuni yaliyojikita katika sekta za kilimo, fedha, uzalishaji, usambazaji wa bidhaa na kadhalika, huku akitajwa kuajiri zaidi ya watu 20,000.


Comments

Popular posts from this blog

Four Armed Robbery Suspects Killed In Shootout With Police In Songwe

  “This is Vwawa Bus Stand, where the incident occurred in which armed robbers shot and killed a security guard before fleeing with various items.” Songwe. Four suspected armed robbers have been shot dead following a confrontation with police in Songwe Region after allegedly being involved in a violent raid on a mobile phone and financial services shop in Vwawa town, Mbozi District, in which a security guard was killed. According to a statement issued today, December 30, 2025, by the Songwe Regional Police Commander, Senior Assistant Commissioner of Police (SACP) Augustino Senga, the incident occurred at around 3:30 a.m. The suspects reportedly stormed the shop, owned by businessman Gabriel Msemwa, at the Vwawa main bus stand, killed the guard, William Mwampashi (45), and fled with assorted items. The deceased suspects have been identified as Bruce Mwasenga, Eliuta Mapunda, Abdul Chiba, and Justine, known by a single name. SACP Senga said police immediately launched intensive, inte...

JAB Yawasogeza Huduma Waandishi Iringa, Yaomba Ushirikiano Kudhibiti Waandishi Wasioidhinishwa

Iringa. Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imeendelea na jitihada za kusogeza huduma zake kwa waandishi wa habari nchini, safari hii ikifika katika Klabu ya Waandishi wa Habari Iringa (Iringa Press Club – IPC), ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha tasnia ya habari na kulinda taaluma ya uandishi wa habari. Akizungumza wakati wa kikao na waandishi wa habari mkoani Iringa, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB), Wakili Patrick Kipangula, amesema lengo la ziara hiyo ni kutoa elimu kuhusu majukumu ya bodi, mchakato wa ithibati pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili waandishi wa habari ngazi ya mikoa. Wakili Kipangula amesema bado kuna changamoto ya uwepo wa watu wanaojihusisha na shughuli za uandishi wa habari bila kuwa na ithibati halali, hali inayochafua tasnia na kuhatarisha maadili ya kazi hiyo nyeti. “Tunawaomba waandishi wa habari kushirikiana na Bodi kwa kuwafichua watu wanaojitambulisha kama waandishi bila kuwa na ithiba...

MUCE IMPLEMENTS SH18.6 BILLION PROJECT IN HONOUR OF FATHER OF THE NATION’S VISION

Iringa. As Tanzania marks 26 years since the passing of the Father of the Nation, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere — a passionate advocate for education — Mkwawa University College of Education (MUCE), a constituent college of the University of Dar es Salaam (UDSM), continues to successfully implement the Higher Education for Economic Transformation (HEET) Project worth over Sh18.6 billion. Speaking to journalists in Iringa, MUCE Principal Prof Method Samwel Semiono said the project, implemented by the government through the Ministry of Education, Science and Technology, aims to reform the higher education system so it can directly contribute to the country’s economic transformation. “The five-year project (2021/2022–2025/2026) is funded by the World Bank and focuses on curriculum improvement, infrastructure development, human resource capacity building, inclusive education and gender equality, as well as promoting the use of ICT and digital learning,” explained Prof Semiono. He no...